فَمَكَثَ غَيۡرَ بَعِيدٖ فَقَالَ أَحَطتُ بِمَا لَمۡ تُحِطۡ بِهِۦ وَجِئۡتُكَ مِن سَبَإِۭ بِنَبَإٖ يَقِينٍ
Basi (Hud-hud) akakaa si mbali na akasema: Nimegundua usilo gundua wewe, na ninakujia hivi kutoka nchi ya Sabai, na nakuletea khabari za yakini.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Akakaa hud-hud muda usio mrefu kisha akahudhuria, na Sulaymān akamlaumu juu ya kughibu kwake na kutokuwako kwake. Hud-hud akamwambia, «Nimejua jambo usilolijuwa kikamilifu, na nimekujia kutoka mji wa Saba’ na habari ya jambo muhimu sana, na mimi nina yakina nalo.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس