وَصَدَّهَا مَا كَانَت تَّعۡبُدُ مِن دُونِ ٱللَّهِۖ إِنَّهَا كَانَتۡ مِن قَوۡمٖ كَٰفِرِينَ
Na yale aliyo kuwa akiyaabudu badala ya Mwenyezi Mungu yalimzuilia. Hakika yeye (Malkia) alikuwa katika kaumu ya makafiri.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na kilimzuia yeye kumuabudu Mwenyezi Mungu Peke Yake kile alichokuwa akikiabudu badala ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka,. Kwa hakika yeye alikuwa ni kafiri na alikulia kati ya watu makafiri na akaendelea kwenye dini yao, isipokuwa hivyo, yeye ana werevu na busara ya kuijua haki na kuipambanua na batili, lakini itikadi za ubatilifu zinaondoa nuru ya moyo.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس