وَوَقَعَ ٱلۡقَوۡلُ عَلَيۡهِم بِمَا ظَلَمُواْ فَهُمۡ لَا يَنطِقُونَ
Na kauli itawaangukia juu yao kwa vile walivyo dhulumu. Basi hao hawatasema lolote.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hapo lithibiti juu yao neno la adhabu kwa sababu ya udhalimu wao na ukanushaji wao, na watakuwa hawatamki neno lenye hoja ya wao kujitetea nafsi zao ili kujiepushia adhabu kali iliyowashukia.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس