وَلَا يَسۡتَطِيعُونَ لَهُمۡ نَصۡرٗا وَلَآ أَنفُسَهُمۡ يَنصُرُونَ
Wala hawana uwezo wa kuwanusuru wala wenyewe hawajinusuru.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Wala hawawezi kuwanusuru wenye kuwaabudu au kuzilinda nafsi zao na ubaya. Iwapo wao hawaumbi kitu, bali wao wameumbwa na hawawezi kuwalinda wanaowaabudu, wasipatikane na mambo wanayoyachukia, wala kuzilinda nafsi zao. Basi vipi wanafanywa ni waungu? Huu haukuwa isipokuwa ni upeo wa udhalimu na upeo wa uchache wa akili.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس