ثُمَّ عَفَوۡنَا عَنكُم مِّنۢ بَعۡدِ ذَٰلِكَ لَعَلَّكُمۡ تَشۡكُرُونَ
Kisha tukakusameheni baada ya hayo, ili mpate kushukuru.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Kisha tukawasamehe kitendo hiki kibaya, tukakubali toba yenu baada ya kurudi Musa kwa kutarajia kuwa mtamshukuru Mwenyezi Mungu kwa neema Zake na fadhila Zake juu yenu, na hamtaendelea kwenye ukafiri na uasi.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس