رُدُّوهَا عَلَيَّۖ فَطَفِقَ مَسۡحَۢا بِٱلسُّوقِ وَٱلۡأَعۡنَاقِ
(Akasema:) Nirudishieni! Akaanza kuwapapasa miguu na shingo.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Warudisheni hao farasi walioorodheshwa hivi punde.» Wakarudishwa, na akaingia kuipiga miguu yao na shingo zao kwa upanga kwa kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu, kwa kuwa wao walikuwa ni sababu ya Swala yake kumpita, Na ilikuwa kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu kwa kuchinja farasi yakubaliwa katika Sheria yake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس