مَا سَمِعۡنَا بِهَٰذَا فِي ٱلۡمِلَّةِ ٱلۡأٓخِرَةِ إِنۡ هَٰذَآ إِلَّا ٱخۡتِلَٰقٌ
Sisi hatukusikia haya katika mila hii ya mwisho. Haya si chochote ila ni uzushi tu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hatujasikia hili analolingania katika dini ya baba zetu wa Kikureshi wala katika Unaswara; halikuwa hili isipokuwa ni urongo na uzushi.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس