Tafsiri ya Sura Al-Masad kwa السواحلية kutoka الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس
Verse 1
ﮈﮉﮊﮋﮌ
ﮍ
Imehasirika mikono miwili ya Abu Lahab, na yeye mwenyewe ameangamia, kwa kumuudhi Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie. Hasara ya Abu Lahab ilithubutu.
Verse 2
ﮎﮏﮐﮑﮒﮓ
ﮔ
Hayakumfalia kitu mali yake na watoto wake. Kwani hivyo havitamkinga na adhabu ya Mwenyezi Mungu pindi ikimshukia.
Verse 3
ﮕﮖﮗﮘ
ﮙ
Ataingia kwenye Moto wenye kuroroma,
Verse 4
ﮚﮛﮜ
ﮝ
yeye na mke wake ambaye alikuwa akibeba miba na kuiweka kwenye njia anayopita Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, ili kumuudhi.
Verse 5
ﮞﮟﮠﮡﮢ
ﮣ
Kwenye shingo yake patakuwa na kamba imara ya lifu gumu lilio kavu; atabebewa nayo kwenye Moto wa Jahanamu, kisha atarushwa nayo mpaka chini.
تقدم القراءة