سورة الغاشية

الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس

Tafsiri ya Sura Al-Ghashiyah kwa السواحلية kutoka الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس

الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس

Verse 1
Je, ilikujia,ewe Mtume, habari ya Kiyama chenye vituko venye kuwaenea watu?
Verse 2
Nyuso za Makafiri, Siku hiyo, zitakuwa zimenyongeka kwa adhabu.
Verse 3
Zishughulishie, zimechoka na kutaabika.
Watu wa Motoni hawatakuwa na chakula isipokuwa kinachotoka kwenye mti wa miba ilioshikana na chini. Ni kibaya sana chakula hiko na ni kichafu mno.
Hakimnoneshi mwenye kukila, awapo amekonda, wala hakimuondolei njaa, awapo na njaa.
Verse 8
Nyuso za Waumini, siku ya Kiyama, zitakuwa kwenye neema.
Verse 9
Kwa kuwa zilijishughulisha ulimwenguni kumtii Mwenyezi Mungu na kuridhika na Akhera.
Verse 12
Ndani yake kuna chemchemi yenye kuteremka maji yake.
Verse 14
na vikombe vilivyotayarishwa kwa wenye kunywa,
Verse 15
na mito iliyopangwa, mmoja baada ya mwingine,
Kwani, hawa makafiri wenye kukanusha, hawaangalii ngamia namna walivyoumbwa kiajabu?
Verse 19
Na milima namna iliyoimarishwa ukapatikana uthabiti na utulivu wa ardhi?
Verse 21
Basi wawaidhie, ewe Mtume, wale wenye kupa nyongo yale uliyotumilizwa kwayo wala usihuzunike kwa kupa mgongo kwao.
Verse 22
Kwani wewe ni muwaidhiaji kwao, na si juu yako kuwalazimisha kuamini..
Verse 23
Lakini yule mwenye kuyapa mgongo makumbusho na mawaidha na akawa mkakamavu kwenye ukafiri wake,
تقدم القراءة