Tafsiri ya Sura Al-Ghashiyah kwa السواحلية kutoka الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس
Verse 1
ﭽﭾﭿﮀ
ﮁ
Je, ilikujia,ewe Mtume, habari ya Kiyama chenye vituko venye kuwaenea watu?
Verse 2
ﮂﮃﮄ
ﮅ
Nyuso za Makafiri, Siku hiyo, zitakuwa zimenyongeka kwa adhabu.
Verse 3
ﮆﮇ
ﮈ
Zishughulishie, zimechoka na kutaabika.
Verse 4
ﮉﮊﮋ
ﮌ
Zinachomwa kwa Moto wenye kuwaka kwa ukali.
Verse 5
ﮍﮎﮏﮐ
ﮑ
Zitanyweshwa maji ya chemchemi yenye moto sana.
Verse 6
ﮒﮓﮔﮕﮖﮗ
ﮘ
Watu wa Motoni hawatakuwa na chakula isipokuwa kinachotoka kwenye mti wa miba ilioshikana na chini. Ni kibaya sana chakula hiko na ni kichafu mno.
Verse 7
ﮙﮚﮛﮜﮝﮞ
ﮟ
Hakimnoneshi mwenye kukila, awapo amekonda, wala hakimuondolei njaa, awapo na njaa.
Verse 8
ﮠﮡﮢ
ﮣ
Nyuso za Waumini, siku ya Kiyama, zitakuwa kwenye neema.
Verse 9
ﮤﮥ
ﮦ
Kwa kuwa zilijishughulisha ulimwenguni kumtii Mwenyezi Mungu na kuridhika na Akhera.
Verse 10
ﮧﮨﮩ
ﮪ
Zitakuwa kwenye Pepo ya daraja ya juu.
Verse 11
ﮫﮬﮭﮮ
ﮯ
Hutasikia humo hata neno moja la upuuzi.
Verse 12
ﮰﮱﯓ
ﯔ
Ndani yake kuna chemchemi yenye kuteremka maji yake.
Verse 13
ﯕﯖﯗ
ﯘ
Ndani yake mna vitanda vilioangatika,
Verse 14
ﯙﯚ
ﯛ
na vikombe vilivyotayarishwa kwa wenye kunywa,
Verse 15
ﯜﯝ
ﯞ
na mito iliyopangwa, mmoja baada ya mwingine,
Verse 16
ﯟﯠ
ﯡ
na mazulia mengi yaliyotandikwa.
Verse 17
ﯢﯣﯤﯥﯦﯧ
ﯨ
Kwani, hawa makafiri wenye kukanusha, hawaangalii ngamia namna walivyoumbwa kiajabu?
Verse 18
ﯩﯪﯫﯬ
ﯭ
Na mbingu namna zlizoinuliwa juu kwa namna ya kupendeza?
Verse 19
ﯮﯯﯰﯱ
ﯲ
Na milima namna iliyoimarishwa ukapatikana uthabiti na utulivu wa ardhi?
Verse 20
ﯳﯴﯵﯶ
ﯷ
Na ardhi namna ilivyotandikwa na kutayarishwa?
Verse 21
ﯸﯹﯺﯻ
ﯼ
Basi wawaidhie, ewe Mtume, wale wenye kupa nyongo yale uliyotumilizwa kwayo wala usihuzunike kwa kupa mgongo kwao.
Verse 22
ﯽﯾﯿ
ﰀ
Kwani wewe ni muwaidhiaji kwao, na si juu yako kuwalazimisha kuamini..
Verse 23
ﭑﭒﭓﭔ
ﭕ
Lakini yule mwenye kuyapa mgongo makumbusho na mawaidha na akawa mkakamavu kwenye ukafiri wake,
Verse 24
ﭖﭗﭘﭙ
ﭚ
Mwenyezi Mungu Atamuadhibu adhabu kali Motoni.
Verse 25
ﭛﭜﭝ
ﭞ
Hakika wao watarudi kwetu baada ya kufa.
Verse 26
ﭟﭠﭡﭢ
ﭣ
Kisha ni juu yetu kuwalipa kwa waliyoyafanya.
تقدم القراءة