Tafsiri ya Sura Ali-Humazah kwa السواحلية kutoka الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس
Verse 1
ﭢﭣﭤﭥ
ﭦ
Shari na maangamivu yatampata kila mwenye kusengenya watu na kuwatukana.
Verse 2
ﭧﭨﭩﭪ
ﭫ
Ambaye hamu yake ni kukusanya mali na kuyahesabu.
Verse 3
ﭬﭭﭮﭯ
ﭰ
Akidhani kuwa mali yake ambayo ameyakusanya yatampa dhamana ya kuishi milele duniani na kuhepa kuhesabiwa.
Verse 4
ﭱﭲﭳﭴﭵ
ﭶ
Anavyodhania sivyo. Atatiwa ndani ya Moto ambao huvunjavunja kila kinachotiwa.
Verse 5
ﭷﭸﭹﭺ
ﭻ
Lipi lililokujulisha, ewe Mtume, ni upi huo Moto unaovunjavunja?
Verse 6
ﭼﭽﭾ
ﭿ
Huo ni Moto wa Mwenyezi Mungu uliowashwa.
Verse 7
ﮀﮁﮂﮃ
ﮄ
Ambao kwa ukali wake hupenyeza miilini ukafikia kwenye nyoyo.
Verse 8
ﮅﮆﮇ
ﮈ
Moto huo umefungiwa juu yao wakiwa wametiwa minyororo
Verse 9
ﮉﮊﮋ
ﮌ
na pingu ndefu ili wasitoke.
تقدم القراءة