Tafsiri ya Sura Al'Alak kwa السواحلية kutoka الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس
Verse 1
ﮕﮖﮗﮘﮙ
ﮚ
Soma, ewe Nabii, Qur’ani uliyoteremshiwa ukianza kwa Jina la Mola wako Aliyepwekeka kwa kuumba.
Verse 2
ﮛﮜﮝﮞ
ﮟ
Aliyemuumba kila binadamu kwa pande la damu nzito nyekundu.
Verse 3
ﮠﮡﮢ
ﮣ
Soma, ewe Nabii, kile ulichoteremshiwa, na Mola wako ni Mwingi wa wema, Mwingi wa ukarimu.
Verse 4
ﮤﮥﮦ
ﮧ
Aliyewafundisha viumbe vyake kuandika kwa kalamu.
Verse 5
ﮨﮩﮪﮫﮬ
ﮭ
Alimfundisha binadamu vitu ambavyo hakuwa akivijua. Akamtoa kwenye giza la ujinga, Akampeleka kwenye nuru ya elimu.
Verse 6
ﮮﮯﮰﮱ
ﯓ
Kweli, binadamu hukiuka mipaka ya Mwenyezi Mungu
Verse 7
ﯔﯕﯖ
ﯗ
akijiona ametosheka kwa utajiri wake.
Verse 8
ﯘﯙﯚﯛ
ﯜ
Basi, ajue kila mwenye kutupa mipaka kuwa mwisho atarudi kwa Mwenyezi Mungu Ambaye Atamlipa kila binadamu kwa alilolitenda.
Verse 9
ﯝﯞﯟ
ﯠ
Je, umeona ujeuri wa ajabu zaidi kuliko wa mtu huyu, Abu jahl,
Verse 10
ﯡﯢﯣ
ﯤ
Anayemkataza mja wetu, Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, anapomsalia Mola wake?
Verse 11
ﯥﯦﯧﯨﯩ
ﯪ
Waonaje iwapo mwenye kukatazwa kusali yuko uongofuni, vipi anamkataza?
Verse 12
ﯫﯬﯭ
ﯮ
Au iwapo anaamrisha mwigine kumcha Mungu, vipi anamkataza hilo?
Verse 13
ﭑﭒﭓﭔ
ﭕ
Waonaje iwapo huyu mwenye kukataza anakanusha lile alinganiwalo kwalo na kulipa mgongo,
Verse 14
ﭖﭗﭘﭙﭚ
ﭛ
hajui kuwa Mwenyezi Mungu anaona kila analolifanya?
Verse 15
ﭜﭝﭞﭟﭠﭡ
ﭢ
Basi mambo si kama anvyodai Abu Jahl. Na asipokomeka na ushindani alionao na udhia wake, Tutamshika upaa wake kwa nguvu na kumtia Motoni.
Verse 16
ﭣﭤﭥ
ﭦ
Upaa wake ni upaa wenye maneno ya urongo na vitendo vya makosa.
Verse 17
ﭧﭨ
ﭩ
Basi na awalete, mtupaji mipaka huyu, watu wa baraza ili wamsaidiye.
Verse 18
ﭪﭫ
ﭬ
Sisi Tutawaita Malaika wa adhabu.
Verse 19
ﭭﭮﭯﭰﭱﭲ
ﭳ
Mambo si kama Abu Jahl anavyoyadhania. Yeye, ewe Mtume, hawezi kukufanya lolote la kukudhuru Usimfuate kwa lile alilokuitia la kuwa uache Swala, bali msujudie Mola wako na uwe karibu na Yeye kwa kujipendekeza Kwake kwa kumtii.
تقدم القراءة