سورة التكوير

الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس

Tafsiri ya Sura An-Takwir kwa السواحلية kutoka الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس

الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس

Verse 1
Pindi jua litakapokunjwa, na mwangaza wake ukaondoka.
Verse 2
Na pindi nyota zitakapopuputika na nuru yake ikafutika.
Verse 3
Na pindi majabali yatakapoondoshawa kwenye uso wa ardhi yakawa ni vumbi linaloenea.
Verse 4
Na pindi ngamia wenye mimba watakapoachwa na kupuuzwa.
Verse 5
Na pindi wanyama mwitu watakapokusanywa na kutangamanishwa, ili Mwenyezi Mungu Awape nafasi ya kulipizana wao kwa wao.
Verse 6
Na pindi bahari zitakapowashwa moto zikawa ni moto unaowaka.
Verse 7
Na pindi nafsi zitakapokutanishwa na mfano wake na sampuli yake.
Verse 8
Na pindi mtoto wa kike aliyezikwa akiwa hai atakapoulizwa, Siku ya Kiyama, suala la kumbembeleza na kumkejeli aliyemzika:
Verse 11
Na pindi mbingu zitakapong’olewa na kuondoshwa zilipokuwa.
Verse 13
Na pindi Pepo , Nyumba ya Neema, itakaposongezewa watu wake wachamungu.
Verse 14
Litakapotokea hilo, itayakinisha kila nafsi na kujua kile ilichokitanguliza cha kheri au shari.
Verse 15
Anaapa Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa nyota zinazofichika nuru yake mchana,
Verse 16
zinazotembea na zinazoghibu katika anga zake.
Verse 17
Na Anaapa kwa usiku unapojitokeza na giza lake.
Verse 19
Hakika Qur’ani ni ujumbe wa mjumbe mtukufu , naye ni Jibrili, amani imshukike.
Mwenye nguvu katika kuyapitisha yale anayoamrishwa. Mwenye cheo cha juu kwa Mwenyezi Mungu. Anayesikilizwa na Malaika.
Verse 23
Na kwa hakika Muhammad alimuona Jibrili anayemjia na utume katika pambizo kubwa.
Wala haikuwa hii Qur’ani ni neno la Shetani aliyefukuzwa na kutolewa kwenye rehema ya Mwenyezi Mungu. Lakini Qur’ani hii ni maneno ya Mwenyezi Mungu na ni Wahyi wake.
Verse 26
Akili zenu zawapeleka wapi katika kukanusha baada ya hoja hizi zilizo wazi na zenye nguvu?
Hayakuwa haya isipokuwa ni mawaidha kutoka kwa Mwenyezi Mungu yanapewa watu wote.
تقدم القراءة