Tafsiri ya Sura An-Takwir kwa السواحلية kutoka الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس
Verse 1
ﭙﭚﭛ
ﭜ
Pindi jua litakapokunjwa, na mwangaza wake ukaondoka.
Verse 2
ﭝﭞﭟ
ﭠ
Na pindi nyota zitakapopuputika na nuru yake ikafutika.
Verse 3
ﭡﭢﭣ
ﭤ
Na pindi majabali yatakapoondoshawa kwenye uso wa ardhi yakawa ni vumbi linaloenea.
Verse 4
ﭥﭦﭧ
ﭨ
Na pindi ngamia wenye mimba watakapoachwa na kupuuzwa.
Verse 5
ﭩﭪﭫ
ﭬ
Na pindi wanyama mwitu watakapokusanywa na kutangamanishwa, ili Mwenyezi Mungu Awape nafasi ya kulipizana wao kwa wao.
Verse 6
ﭭﭮﭯ
ﭰ
Na pindi bahari zitakapowashwa moto zikawa ni moto unaowaka.
Verse 7
ﭱﭲﭳ
ﭴ
Na pindi nafsi zitakapokutanishwa na mfano wake na sampuli yake.
Verse 8
ﭵﭶﭷ
ﭸ
Na pindi mtoto wa kike aliyezikwa akiwa hai atakapoulizwa, Siku ya Kiyama, suala la kumbembeleza na kumkejeli aliyemzika:
Verse 9
ﭹﭺﭻ
ﭼ
ni kwa dhambi gani ilikuwa kuzikwa kwake?
Verse 10
ﭽﭾﭿ
ﮀ
Na pindi kurasa za matendo zitakapoonyeshwa.
Verse 11
ﮁﮂﮃ
ﮄ
Na pindi mbingu zitakapong’olewa na kuondoshwa zilipokuwa.
Verse 12
ﮅﮆﮇ
ﮈ
Na pindi Moto utakapowashwa na ukawaka.
Verse 13
ﮉﮊﮋ
ﮌ
Na pindi Pepo , Nyumba ya Neema, itakaposongezewa watu wake wachamungu.
Verse 14
ﮍﮎﮏﮐ
ﮑ
Litakapotokea hilo, itayakinisha kila nafsi na kujua kile ilichokitanguliza cha kheri au shari.
Verse 15
ﮒﮓﮔ
ﮕ
Anaapa Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa nyota zinazofichika nuru yake mchana,
Verse 16
ﮖﮗ
ﮘ
zinazotembea na zinazoghibu katika anga zake.
Verse 17
ﮙﮚﮛ
ﮜ
Na Anaapa kwa usiku unapojitokeza na giza lake.
Verse 18
ﮝﮞﮟ
ﮠ
Na kwa asubuhi unapojitokeza mwangaza wake.
Verse 19
ﮡﮢﮣﮤ
ﮥ
Hakika Qur’ani ni ujumbe wa mjumbe mtukufu , naye ni Jibrili, amani imshukike.
Verse 20
ﮦﮧﮨﮩﮪﮫ
ﮬ
Mwenye nguvu katika kuyapitisha yale anayoamrishwa. Mwenye cheo cha juu kwa Mwenyezi Mungu. Anayesikilizwa na Malaika.
Verse 21
ﮭﮮﮯ
ﮰ
Anayeaminiwa juu ya Wahyi anaoteremka nao.
Verse 22
ﮱﯓﯔ
ﯕ
Hakuwa Muhammad mnayemjua ni mwendawazimu.
Verse 23
ﯖﯗﯘﯙ
ﯚ
Na kwa hakika Muhammad alimuona Jibrili anayemjia na utume katika pambizo kubwa.
Verse 24
ﯛﯜﯝﯞﯟ
ﯠ
Wala yeye hafanyi ubakhili katika kufikisha Wahyi.
Verse 25
ﯡﯢﯣﯤﯥ
ﯦ
Wala haikuwa hii Qur’ani ni neno la Shetani aliyefukuzwa na kutolewa kwenye rehema ya Mwenyezi Mungu. Lakini Qur’ani hii ni maneno ya Mwenyezi Mungu na ni Wahyi wake.
Verse 26
ﯧﯨ
ﯩ
Akili zenu zawapeleka wapi katika kukanusha baada ya hoja hizi zilizo wazi na zenye nguvu?
Verse 27
ﯪﯫﯬﯭﯮ
ﯯ
Hayakuwa haya isipokuwa ni mawaidha kutoka kwa Mwenyezi Mungu yanapewa watu wote.
Verse 28
ﯰﯱﯲﯳﯴ
ﯵ
Kwa atakaye, kati yenu, kulingana juu ya haki na Imani.
Verse 29
Wala nyinyi hamtotaka isipokuwa kwa matakwa ya Mwenyezi Mungu Mola wa viumbe wote.
تقدم القراءة