Tafsiri ya Sura At-Tarik kwa السواحلية kutoka الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس
Verse 1
ﭑﭒ
ﭓ
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa mbingu na nyota yenye kuchomoza usiku.
Verse 2
ﭔﭕﭖﭗ
ﭘ
Na ni lipi lilokujulisha ni ukubwa gani wa nyota hiyo?
Verse 3
ﭙﭚ
ﭛ
Hiyo ni nyota ing’arao na kuzagaa.
Verse 4
ﭜﭝﭞﭟﭠﭡ
ﭢ
Hakuna nafsi yoyote isipokuwa amewakilishwa kwayo Malaika mwenye kuchunguza na kusjili amali zake ili ihesabiwe Siku ya Kiyama.
Verse 5
ﭣﭤﭥﭦ
ﭧ
Basi aangalie binadamu mwenye kukanusha kufufuliwa ameumbwa kwa kitu gani? Ili ajue kuwa kurudisha umbo lake mara ya pili si vigumu kama kuumbwa mara ya kwanza.
Verse 6
ﭨﭩﭪﭫ
ﭬ
Aliumbwa kwa manii yenye kupenyeza ndani ya uzao kwa haraka.
Verse 7
ﭭﭮﭯﭰﭱ
ﭲ
Yatokayo kwenye mgongo wa mwnamume na kifua cha mwanamke.
Verse 8
ﭳﭴﭵﭶ
ﭷ
Hakika yule Aliyemuumba binadamu kwa maji haya ni muweza wa kumrudisha kwenye uhai baada ya kufa.
Verse 9
ﭸﭹﭺ
ﭻ
Siku zitakapofunuliwa wazi siri ziliofichwa na nafsi na kupambanuliwa njema na mbovu.
Verse 10
ﭼﭽﭾﭿﮀﮁ
ﮂ
Binadamu hatakuwa na nguvu ya kuitetea nafsi yake wala hatakuwa na mtetezi wa kumwepushia adhabu ya Mwenyezi Mungu.
Verse 11
ﮃﮄﮅ
ﮆ
Na Anaapa kwa mbingu yenye mvua ya kukaririka.
Verse 12
ﮇﮈﮉ
ﮊ
Na ardhi yenye pasuko za kufanya mimea ichipuke.
Verse 13
ﮋﮌﮍ
ﮎ
Hakika Qur’ani ni neno lenye kupambanua baina ya haki na batili.
Verse 14
ﮏﮐﮑ
ﮒ
Na si upuuzi. Haifai kiumbe kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu. Akifanya hivyo atakuwa amemshirikisha Mwenyezi Mungu.
Verse 15
ﮓﮔﮕ
ﮖ
Hakika wenye kumkanusha Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na Qur’ani wanafanya vitimbi na mipango ili kuipinga haki na kuitilia nguvu batili.
Verse 16
ﮗﮘ
ﮙ
Na Mimi nafanya vitimbi kuidhihirisha haki ingawa makafiri wanatukia.Usiwe na haraka nao, ewe Mtume, kutaka wateremshiwe adhabu.
Verse 17
ﮚﮛﮜﮝ
ﮞ
Wape muhula uwangojee muda mchache wala usiwafanyie haraka, utaona adhabu itakayowafikia, mateso na maangamivu.
تقدم القراءة