سورة الطارق

الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس

Tafsiri ya Sura At-Tarik kwa السواحلية kutoka الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس

الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس

Verse 1
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa mbingu na nyota yenye kuchomoza usiku.
Verse 3
Hiyo ni nyota ing’arao na kuzagaa.
Hakuna nafsi yoyote isipokuwa amewakilishwa kwayo Malaika mwenye kuchunguza na kusjili amali zake ili ihesabiwe Siku ya Kiyama.
Verse 5
Basi aangalie binadamu mwenye kukanusha kufufuliwa ameumbwa kwa kitu gani? Ili ajue kuwa kurudisha umbo lake mara ya pili si vigumu kama kuumbwa mara ya kwanza.
Verse 6
Aliumbwa kwa manii yenye kupenyeza ndani ya uzao kwa haraka.
Verse 8
Hakika yule Aliyemuumba binadamu kwa maji haya ni muweza wa kumrudisha kwenye uhai baada ya kufa.
Verse 9
Siku zitakapofunuliwa wazi siri ziliofichwa na nafsi na kupambanuliwa njema na mbovu.
Binadamu hatakuwa na nguvu ya kuitetea nafsi yake wala hatakuwa na mtetezi wa kumwepushia adhabu ya Mwenyezi Mungu.
Verse 11
Na Anaapa kwa mbingu yenye mvua ya kukaririka.
Verse 12
Na ardhi yenye pasuko za kufanya mimea ichipuke.
Verse 13
Hakika Qur’ani ni neno lenye kupambanua baina ya haki na batili.
Verse 14
Na si upuuzi. Haifai kiumbe kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu. Akifanya hivyo atakuwa amemshirikisha Mwenyezi Mungu.
Verse 15
Hakika wenye kumkanusha Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na Qur’ani wanafanya vitimbi na mipango ili kuipinga haki na kuitilia nguvu batili.
Verse 16
Na Mimi nafanya vitimbi kuidhihirisha haki ingawa makafiri wanatukia.Usiwe na haraka nao, ewe Mtume, kutaka wateremshiwe adhabu.
Verse 17
Wape muhula uwangojee muda mchache wala usiwafanyie haraka, utaona adhabu itakayowafikia, mateso na maangamivu.
تقدم القراءة