Tafsiri ya Sura Ar-Rahman kwa السواحلية kutoka الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس
Verse 1
ﭷ
ﭸ
mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema
Verse 2
ﭹﭺ
ﭻ
Amemfundisha binadamu Qur’ani kwa kurahisisha kuisoma, kuihifadhi na kuelewa maana yake.
Verse 3
ﭼﭽ
ﭾ
Amemuumba binadamu,
Verse 4
ﭿﮀ
ﮁ
Amemfundisha ufasaha wa kujieleza ili kumtenganisha na wengine.
Verse 5
ﮂﮃﮄ
ﮅ
Jua na mwezi zinatembea kwa kufuatana, moja baada ya nyingine, kwa hesabu madhubuti isiyotafautiana wala kugongana.
Verse 6
ﮆﮇﮈ
ﮉ
Na nyota iliyo mbinguni na miti ya ardhini, vinamjua Mola wao, vinamsujudia na vinanyosha shingo zao kufuata vile ambavyo vimepangiwa vifuate vya maslahi ya waja Wake na manufaa yao.
Verse 7
ﮊﮋﮌﮍ
ﮎ
Na mbingu Ameiinua na kuifanya iwe juu ya ardhi, Na Ameweka kwenye ardhi uadilifu Aliouamrisha na kuulazimisha kwa waja Wake.
Verse 8
ﮏﮐﮑﮒ
ﮓ
Ili msipite mipaka na msimfanyie hiyana mnayempimia.
Verse 9
ﮔﮕﮖﮗﮘﮙ
ﮚ
Na simamisheni upimaji kwa usawa na msipunguze mizani mnapowapimia watu.
Verse 10
ﮛﮜﮝ
ﮞ
Na ardhi Ameiweka na Ameitayarisha, ili viumbe vitulie juu yake.
Verse 11
ﮟﮠﮡﮢﮣ
ﮤ
Humo mna matunda na mitende yenye makarara ya matunda. Na humo kuna nafaka zenye maganda, vikiwa ni chakula chenu na wanyama wenu.
Verse 12
ﮥﮦﮧﮨ
ﮩ
Na humo mna kila mmea wenye harufu nzuri.
Verse 13
ﮪﮫﮬﮭ
ﮮ
Bas ni neema gani za Mola wenu, za kidini na za kidunia, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha? Na ni jawabu nzuri ilioje ya majini alipowasomea wao Nabii, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, sura hii, kila akipita kwenye aya hii walikuwa wakisema, «Hakuna chochote miongoni mwa neema zako, ewe Mola wetu, tunachokanusha. Sifa njema zote ni zako.» Na hivi ndivyo inavyotakiwa kwa mja anapoelezewa neema za Mwenyezi Mungu na mema Yake akubali na amshukuru Mwenyezi Mungu kwa neema hizo.
Verse 14
ﮯﮰﮱﯓﯔ
ﯕ
Amemuumba baba wa wanadamu, naye ni Ādam, kwa udongo mkavu kama vyungu.
Verse 15
ﯖﯗﯘﯙﯚﯛ
ﯜ
Na Amemuumba Iblisi, naye ni katika majini, kwa mroromo wa moto uliochanganyika.
Verse 16
ﯝﯞﯟﯠ
ﯡ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
Verse 17
ﯢﯣﯤﯥ
ﯦ
Mola wa pande mbili za Mashariki ya jua, katika kusi na kaskazi, na Mola wa pande mbili za Magharibi ya jua, katika kusi na kaskazi, kwani vyote viko chini ya uendeshaji Wake na ulezi Wake..
Verse 18
ﯧﯨﯩﯪ
ﯫ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
Verse 19
ﭑﭒﭓ
ﭔ
Mwenyezi Mungu Ameyachanganya maji ya bahari mbili, tamu na chumvi, yanakutana, baina yake kuna kizuizi,
Verse 20
ﭕﭖﭗﭘ
ﭙ
mojawapo haiingii sehemu ya nyingine na kuiondoa sifa yake, bali ya tamu inasalia kuwa tamu na ya chumvi inasalia kuwa chumvi pamoja na kukutana kwake.
Verse 21
ﭚﭛﭜﭝ
ﭞ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
Verse 22
ﭟﭠﭡﭢ
ﭣ
Inatoka kwenye bahari mbili hizo, kwa uweza wa Mwenyezi Mungu, lulu na marjani.
Verse 23
ﭤﭥﭦﭧ
ﭨ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
Verse 24
ﭩﭪﭫﭬﭭﭮ
ﭯ
Ni Yake Yeye, Aliyetakasika na kutukuka, mamlaka ya kuyaendesha majahazi makubwa yanayotembea baharini kwa manufaa ya watu, yenye kusimamisha juu milongoti yake na matanga yake kama vile majabali.
Verse 25
ﭰﭱﭲﭳ
ﭴ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu mnazikanusha?
Verse 26
ﭵﭶﭷﭸ
ﭹ
Kila aliye juu ya uso wa ardhi miongoni mwa viumbe ni mwenye kuangamia,
Verse 27
ﭺﭻﭼﭽﭾﭿ
ﮀ
na utasalia uso wa Mola wako Mwenye utukufu, ubora, kheri nyingi na upaji. Katika aya hii pana kuthibitisha sifa ya uso kwa Mwenyezi Mungu kwa namna inavyonasibiana na Yeye, kutakasika ni Kwake, bila kufananisha wala kueleza namna ulivyo.
Verse 28
ﮁﮂﮃﮄ
ﮅ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
Verse 29
Wanamuomba Yeye walioko mbinguni na ardhini haja zao. Hakuna yoyote anayejitosheleza kutomhitajia Yeye, kutakasika ni Kwake. Kila siku Yeye Yuko kwenye jambo: Anatukuza na Anatweza, Anatoa na Anazuia.
Verse 30
ﮒﮓﮔﮕ
ﮖ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
Verse 31
ﮗﮘﮙﮚ
ﮛ
Nitawatengea kipindi cha kuwahesabu na kuwalipa kwa matendo yenu mliyoyafanya, enyi vizito viwili:-majini na binadamu-, tuwatese watu wa maasia na tuwape malipo mema watu wa utiifu.
Verse 32
ﮜﮝﮞﮟ
ﮠ
Ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
Verse 33
Enyi mkusanyiko wa majini na binadamu! Mkiweza kuihepa amri ya Mwenyezi Mungu na uamuzi Wake kwa kukimbia kwenye pambe za mbingu na ardhi basi fanyeni, na hamuwezi kufanya hivyo isipokuwa kwa nguvu na hoja na amri inayotoka kwa Mwenyezi Mungu Aliyetukuka. (Na vipi mtaweza kufanya hivyo na hali nyinyi hamzimilikii nafsi zenu manufaa yoyote wala madhara?).
Verse 34
ﯔﯕﯖﯗ
ﯘ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
Verse 35
Mtatumiwa mroromo wa moto na shaba iliyoyayushwa, mmiminiwe juu ya vichwa vyenu msiweze kusaidiana.
Verse 36
ﯢﯣﯤﯥ
ﯦ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazukanusha?
Verse 37
ﯧﯨﯩﯪﯫﯬ
ﯭ
Na pindi mbingu itakapopasuka na kuachana Siku ya Kiyama, ikawa nyekundu kama rangi ya waridi na kama mafuta yaliyochemshwa na risasi iliyoyayushwa, kutokana na mambo magumu na vituko vya Siku ya Kiyama.
Verse 38
ﯮﯯﯰﯱ
ﯲ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
Verse 39
Katika Siku hiyo Malaika hawatawauliza wale wahalifu, miongoni mwa binadamu na majini, kuhusu dhambi zao.
Verse 40
ﯼﯽﯾﯿ
ﰀ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
Verse 41
ﰁﰂﰃﰄﰅﰆ
ﰇ
Malaika watawajua wahalifu kwa alama zao, hapo wawashike kwenye paa za vichwa vyao na nyayo zao wawarushe Motoni.
Verse 42
ﭑﭒﭓﭔ
ﭕ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
Verse 43
ﭖﭗﭘﭙﭚﭛ
ﭜ
Wataambiwa hao wahalifu kwa njia ya kulaumiwa na kudhalilishwa, «Huu ndio moto wa Jahanamu ambao wahalifu duniani walikuwa wakiukanusha:
Verse 44
ﭝﭞﭟﭠﭡ
ﭢ
mara wanaadhibiwa kwenye Jaḥīm, na mara nyingine wananyweshwa Hāmīm, nacho ni kinywaji kilichofikia upeo wa ukali wa moto, kinakata tumbo na sehemu za ndani ya mbavu.
Verse 45
ﭣﭤﭥﭦ
ﭧ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu mnazikanusha?
Verse 46
ﭨﭩﭪﭫﭬ
ﭭ
Na anayemcha Mwenyezi Mungu, miongoni mwa waja Wake binadamu na majini, akaogopa kusimama kwake mbele Yake, akamtii na akaacha kumuasi atakuwa na mabustani mawili ya Pepo.
Verse 47
ﭮﭯﭰﭱ
ﭲ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
Verse 48
ﭳﭴ
ﭵ
Mabustani mawili hayo ya Pepo yana matawi yaliyostawi kwa matunda ya kila aina.
Verse 49
ﭶﭷﭸﭹ
ﭺ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
Verse 50
ﭻﭼﭽ
ﭾ
Katika Pepo mbili hizo kuna chemchemi mbili za maji zinazopita katikati yake.
Verse 51
ﭿﮀﮁﮂ
ﮃ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
Verse 52
ﮄﮅﮆﮇﮈ
ﮉ
Katika mabustani hayo mawili ya Pepo kuna sampuli mbili za kila aina ya matunda.
Verse 53
ﮊﮋﮌﮍ
ﮎ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
Verse 54
Na wale wanaoogopa kusimama mbele ya Mola Wao watakuwa na mabustani mawili ya Pepo, ambayo ndani yake watastarehe, hali ya kutegemea juu ya matandiko yaliyojazwa dibaji nzito. Na matunda ya mabustani mawili hayo ya pepo yako karibu nao.
Verse 55
ﮚﮛﮜﮝ
ﮞ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mtazikanusha?
Verse 56
Katika matandiko hayo wapo wake macho yao yanawatazama waume zao tu, hawawatazami wengineo, wamefungamana na wao. Hakuna aliyewaingilia, kabla ya hao waume zao, binadamu yoyote wala jini.
Verse 57
ﮩﮪﮫﮬ
ﮭ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadanu, mnazikanusha?
Verse 58
ﮮﮯﮰ
ﮱ
Kama kwamba hawa wake wa kihurulaini ni yakuti na marijani katika sifa zao na uzuri wao.
Verse 59
ﯓﯔﯕﯖ
ﯗ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa najini na binadamu , mnazikanusha?
Verse 60
ﯘﯙﯚﯛﯜ
ﯝ
Je atakuwa na malipo yoyote, huyu aliyekuwa mwema wa matendo duniani, isipokuwa ni afanyiwe wema kwa kupewa Pepo huko Akhera?
Verse 61
ﯞﯟﯠﯡ
ﯢ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
Verse 62
ﯣﯤﯥ
ﯦ
Na chini ya mabustani ya Pepo mawili yaliyotangulia kuna mabustani ya Pepo mawili mengine.
Verse 63
ﯧﯨﯩﯪ
ﯫ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
Verse 64
ﯬ
ﯭ
Mabustani haya mawili ni rangi ya kijani. Ujani wake umeiva sana mapaka umeingia kwenye weusi.
Verse 65
ﯮﯯﯰﯱ
ﯲ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
Verse 66
ﯳﯴﯵ
ﯶ
Ndani ya mabustani mawili hayo ya Peponi kuna chemchemi mbili zenye kububujika maji daima bila kukatika.
Verse 67
ﯷﯸﯹﯺ
ﯻ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
Verse 68
ﯼﯽﯾﯿ
ﰀ
Kwenye mabustani hayo mawili kuna aina za matunda, mitende na mikomamanga.
Verse 69
ﰁﰂﰃﰄ
ﰅ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
Verse 70
ﭑﭒﭓ
ﭔ
Ndani ya mabustani haya manne ya Pepo kuna wake walio wema wa tabia na wazuri wa nyuso.
Verse 71
ﭕﭖﭗﭘ
ﭙ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
Verse 72
ﭚﭛﭜﭝ
ﭞ
Mahurulaini wakunjufu wa macho, waliositiriwa na kuhifadhiwa mahemani.
Verse 73
ﭟﭠﭡﭢ
ﭣ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
Verse 74
ﭤﭥﭦﭧﭨﭩ
ﭪ
Hawajaingiliwa Mahurulaini hawa na binadamu yoyote wala jini kabla ya waume zao.
Verse 75
ﭫﭬﭭﭮ
ﭯ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
Verse 76
ﭰﭱﭲﭳﭴﭵ
ﭶ
Hali ya kuwa wametegemea kwenye mito yenye mifuko rangi ya kijani na matandiko mazuri.
Verse 77
ﭷﭸﭹﭺ
ﭻ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
Verse 78
ﭼﭽﭾﭿﮀﮁ
ﮂ
Zimekithiri mno baraka za Jina la Mola wako, na kheri Zake zimekuwa nyingi, Mwenye haiba kubwa, utukufu wenye kukamilika na takrima kwa wenye kumtegemea Yeye.
تقدم القراءة