Tafsiri ya Sura As-Sarhi kwa السواحلية kutoka الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس
Verse 1
ﯝﯞﯟﯠ
ﯡ
Kwani Hatukukunjulia, ewe Mtume, kifua chako kwa sheria za Dini, kulingania watu kwa Mwenyezi Mungu na kujipamba kwa tabia nzuri,
Verse 2
ﯢﯣﯤ
ﯥ
Tukakuondolea mazito yako yaliyoemea mgongo wako
Verse 3
ﭑﭒﭓ
ﭔ
na Tukakuweka, kwa matukufu Tuliyokuneemesha,
Verse 4
ﭕﭖﭗ
ﭘ
kwenye cheo cha juu?
Verse 5
ﭙﭚﭛﭜ
ﭝ
Usirudi nyuma katika kueneza ujumbe uliotumwa nao kwa makero ya maadui zako. Kwani kwenye dhiki kuna faraji.
Verse 6
ﭞﭟﭠﭡ
ﭢ
Hakika kwenye dhiki kuna faraji.
Verse 7
ﭣﭤﭥ
ﭦ
Basi utakapomaliza mambo ya kidunia na shughuli zake jipinde kwa kufanya ibada.
Verse 8
ﭧﭨﭩ
ﭪ
Na kwa Mola wako Peke Yake weka matumaini yako.
تقدم القراءة