Tafsiri ya Sura Al'A'alah kwa السواحلية kutoka الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس
Verse 1
ﮟﮠﮡﮢ
ﮣ
Takasa Jina la Mola wako Aliyetukuka na kuepukana na mshirika na kila sifa pungufu kwa namna inayonasibiana na utukufu Wake na utakatifu Wake.
Verse 2
ﮤﮥﮦ
ﮧ
Aliyeumba viumbe Akalitengeneza umbo lao na kulifanya zuri.
Verse 3
ﮨﮩﮪ
ﮫ
Na Aliyekadiria kila kitu na kukipeleka njia inayonasibiana nacho.
Verse 4
ﮬﮭﮮ
ﮯ
Na Aliyeotesha nyasi mbiti zenye rangi ya kijani,
Verse 5
ﮰﮱﯓ
ﯔ
Akazifanya baadaye kuwa kavu zilizobadilika rangi.
Verse 6
ﯕﯖﯗ
ﯘ
Tutakusomea, ewe Mtume, hii Qur’ani kisomo ambacho hutakisahau.
Verse 7
Isipokuwa iwapo Mwenyezi Mungu Ataka usahau kwa hekima na maslahi anayoyajua Yeye. Kwani Yeye ni Mjuzi wa yaliyo wazi na yaliyofichika, ya maneno na ya vitendo.
Verse 8
ﯤﯥ
ﯦ
Tutakufanyia mapesi mambo yako yote; miongoni mwayo ni kukusahilishia kubeba majukumu ya utume na kuifanya nyepesi Dini uliyokuja nayo.
Verse 9
ﯧﯨﯩﯪ
ﯫ
Basi wawaidhie kaumu zako, ewe Mtume, kwa namna tulivyokutayarishia ufanye kwenye wahyi ulioletewa, uwaongoze njia yenye kheri na wao na uwahusu kwa mawaidha yako wale wanaotarajiwa kuwaidhika nayo. Wala usijisumbue kuwashauri wale ambao mawidha hayawaathiri isipokuwa kuwatia ujeuri na kuwafanya wayakimbie.
Verse 10
ﯬﯭﯮ
ﯯ
Atanufaika kwa mawaidha anayemcha Mola wke,
Verse 11
ﭑﭒ
ﭓ
na atajiepusha na mawaidha aliye mbaya asiyemuogopa Mola wake
Verse 12
ﭔﭕﭖﭗ
ﭘ
atakayeingia kwenye Moto wa Jahanamu akiadhibika kwa ukali wake.
Verse 13
ﭙﭚﭛﭜﭝﭞ
ﭟ
Kisha hatakuwa ni mwenye kufa akapumzika wala ni mwenye kuishi akanufaika.
Verse 14
ﭠﭡﭢﭣ
ﭤ
Hakika amefuzu mwenye kuisafisha nafsi yake na tabia mbovu,
Verse 15
ﭥﭦﭧﭨ
ﭩ
na akamtaja Mwenyezi Mungu, akampwekesha, akamuomba, akafanya vitendo vya kumridhisha na akasimamisha Swala kwa nyakati zake kwa kutaka radhi za Mwenyezi Mungu na kufuata sheria Aliyoiweka.
Verse 16
ﭪﭫﭬﭭ
ﭮ
Hakika yenu, nyinyi watu, mnafadhilisha pambo la maisha ya kilimwengu juu ya starehe za Akhera.
Verse 17
ﭯﭰﭱ
ﭲ
Na hakika ya mambo ni kuwa nyumba ya Akhera na starehe zake ni bora zaidi kuliko ulimwngu na ni yenye kusalia zaidi.
Verse 18
ﭳﭴﭵﭶﭷ
ﭸ
Haya mlioosimuliwa ndani ya Sura hii ni miongoni mwa yaliyotajwa kimaana katika Kurasa zilizotangulia kuteremshwa kabla ya Qur’ani.
Verse 19
ﭹﭺﭻ
ﭼ
Nazo ni Kurasa za Ibrāhīm na Mūsā, amani ziwashukie.
تقدم القراءة