Tafsiri ya Sura Al'A'alah kwa السواحلية kutoka Ali Muhsin Al - Swahili translation
Verse 1
ﮟﮠﮡﮢ
ﮣ
Al'A'alah
Litakase jina la Mola wako Mlezi aliye juu kabisa,
Verse 2
ﮤﮥﮦ
ﮧ
Aliye umba, na akaweka sawa,
Verse 3
ﮨﮩﮪ
ﮫ
Na ambaye amekadiria na akaongoa,
Verse 4
ﮬﮭﮮ
ﮯ
Na aliye otesha malisho,
Verse 5
ﮰﮱﯓ
ﯔ
Kisha akayafanya makavu, meusi.
Verse 6
ﯕﯖﯗ
ﯘ
Tutakusomesha wala hutasahau,
Verse 7
Ila akipenda Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye anayajua yaliyo dhaahiri na yaliyo fichikana.
Verse 8
ﯤﯥ
ﯦ
Na tutakusahilishia yawe mepesi.
Verse 9
ﯧﯨﯩﯪ
ﯫ
Basi kumbusha, kama kukumbusha kunafaa.
Verse 10
ﯬﯭﯮ
ﯯ
Atakumbuka mwenye kuogopa.
Verse 11
ﭑﭒ
ﭓ
Na atajitenga mbali nayo mpotovu,
Verse 12
ﭔﭕﭖﭗ
ﭘ
Ambaye atauingia Moto mkubwa.
Verse 13
ﭙﭚﭛﭜﭝﭞ
ﭟ
Tena humo hatakufa wala hawi hai.
Verse 14
ﭠﭡﭢﭣ
ﭤ
Hakika amekwisha fanikiwa aliye jitakasa.
Verse 15
ﭥﭦﭧﭨ
ﭩ
Na akakumbuka jina la Mola wake Mlezi, na akasali.
Verse 16
ﭪﭫﭬﭭ
ﭮ
Lakini nyinyi mnakhiari maisha ya dunia!
Verse 17
ﭯﭰﭱ
ﭲ
Na Akhera ni bora na yenye kudumu zaidi.
Verse 18
ﭳﭴﭵﭶﭷ
ﭸ
Hakika haya yamo katika Vitabu vya mwanzo,
Verse 19
ﭹﭺﭻ
ﭼ
Vitabu vya Ibrahimu na Musa.
تقدم القراءة