Tafsiri ya Sura Sad kwa السواحلية kutoka Ali Muhsin Al - Swahili translation
Verse 1
ﭑﭒﭓﭔﭕ
ﭖ
Sad
S'ad, Naapa kwa Qur'ani yenye mawaidha.
Verse 2
ﭗﭘﭙﭚﭛﭜ
ﭝ
Lakini walio kufuru wamo katika majivuno na upinzani
Verse 3
Mataifa mangapi tumeyaangamiza kabla yao, na wakapiga kelele, lakini wakati wa kuokoka ulikwisha pita.
Verse 4
Na walistaajabu kuwajia mwonyaji anaye tokana nao wenyewe, na makafiri wakasema: Huyu ni mchawi, mwongo.
Verse 5
Amewafanya miungu wote kuwa ni Mungu Mmoja tu? Hakika hili ni jambo la ajabu.
Verse 6
Na wakaondoka wakubwa wao wakiwaambia: Nendeni zenu na dumuni na miungu yenu, kwani hili ni jambo lililo pangwa.
Verse 7
Sisi hatukusikia haya katika mila hii ya mwisho. Haya si chochote ila ni uzushi tu.
Verse 8
Ati yeye tu ndiye aliye teremshiwa mawaidha peke yake katika sisi? Lakini hao wana shaka na mawaidha yangu, bali hawajaionja adhabu yangu.
Verse 9
Au wanazo wao khazina za rehema za Mola wako Mlezi, Mwenye nguvu, Mpaji?
Verse 10
Au wao wana ufalme wa mbingu na ardhi na viliomo kati yao? Basi nawazipande njia za kwendea huko!
Verse 11
ﯟﯠﯡﯢﯣﯤ
ﯥ
Hao ni askari watao shindwa miongoni mwa makundi yatayo shindwa.
Verse 12
Walikanusha kabla yao kaumu ya Nuhu, na kina A'adi na Firauni mwenye majengo.
Verse 13
Na Thamud na kaumu Lut'i na watu wa Machakani. Hayo ndiyo makundi.
Verse 14
Hao wote waliwakadhibisha Mitume; basi wakastahiki adhabu yangu.
Verse 15
Na hawa hawangojei ila ukelele mmoja tu usio na muda.
Verse 16
Na wao husema: Mola wetu Mlezi! Tuletee upesi sehemu yetu ya adhabu kabla ya Siku ya Hisabu.
Verse 17
Subiri kwa hayo wayasemayo, na umkumbuke mja wetu Daudi, mwenye nguvu. Hakika yeye alikuwa mwingi wa kutubia.
Verse 18
Hakika tuliidhalilisha milima pamoja naye ikisabihi jioni na asubuhi pamoja naye.
Verse 19
ﭦﭧﭨﭩﭪﭫ
ﭬ
Na pia ndege walio kusanywa makundi kwa makundi; wote walikuwa wanyenyekevu kwake.
Verse 20
ﭭﭮﭯﭰﭱﭲ
ﭳ
Na tukautia nguvu ufalme wake, na tukampa hikima, na kukata hukumu.
Verse 21
Na je! Imekufikia khabari ya wagombanao walipo pindukia ukuta kuingia chumbani?
Verse 22
Walipo muingilia Daudi, naye akawaogopa. Wakasema: Usiogope! Sisi ni wagombanao wawili, mmoja wetu amemdhulumu mwenziwe. Basi tuhukumu kwa haki, wala usipendelee. Na utuongoe kwenye njia iliyo sawa.
Verse 23
Hakika huyu ndugu yangu ana kondoo wa kike tisiini na tisa; na mimi ninaye kondoo mke mmoja. Akasema: Nipe huyo nikufugie! Na amenishinda kwa maneno.
Verse 24
Akasema: Kweli amekudhulumu kwa kumtaka kondoo wako mmoja kuongezea kwenye kondoo wake. Na hakika washirika wengi hudhulumiana wao kwa wao, isipo kuwa walio amini na wakatenda mema. Na hao ni wachache. Na Daudi akajua kuwa tumemfanyia mtihani. Basi akamwomba msamaha Mola wake Mlezi, na akaanguka kusujudu na kutubia.
Verse 25
Basi tukamsamehe kwa hayo. Naye kwa hakika anao mkaribisho mkubwa na marejeo mazuri kwetu.
Verse 26
Ewe Daudi! Hakika Sisi tumekufanya wewe uwe Khalifa katika nchi. Basi wahukumu watu kwa haki, wala usifuate matamanio yakakupoteza kwenye Njia ya Mwenyezi Mungu. Hakika wanao ipotea Njia ya Mwenyezi Mungu wakaiacha, watapata adhabu kali kwa sababu ya kusahau kwao Siku ya Hisabu.
Verse 27
Na hatukuziumba mbingu na ardhi na viliomo ndani yao bure. Hiyo ni dhana ya walio kufuru. Ole wao walio kufuru kwa Moto utao wapata.
Verse 28
Je! Tuwafanye walio amini na wakatenda mema kama wafanyao uharibifu katika nchi? Au tuwafanye wachamngu kama waovu?
Verse 29
Na hiki Kitabu, tumekuteremshia wewe, kimebarikiwa, ili wazizingatie Aya zake, na wawaidhike wenye akili.
Verse 30
Na Daudi tukamtunukia Suleiman. Alikuwa mja mwema. Na hakika alikuwa mwingi wa kutubia.
Verse 31
ﮅﮆﮇﮈﮉﮊ
ﮋ
Alipo pelekewa jioni farasi wasimamao kidete, tayari kutoka shoti;
Verse 32
Basi akasema: Navipenda vitu vizuri kwa kumkumbuka Mola wangu Mlezi. Kisha wakafichikana nyuma ya boma.
Verse 33
(Akasema:) Nirudishieni! Akaanza kuwapapasa miguu na shingo.
Verse 34
Na tulimtia mtihanini Suleiman, na tukauweka mwili juu ya kiti chake, kisha akarejea kwa kutubu.
Verse 35
Akasema: Mola wangu Mlezi! Nisamehe na unipe ufalme usio mwelekea yeyote baada yangu. Hakika Wewe ndiye Mpaji.
Verse 36
Basi tukaufanya upepo umtumikie, ukenda kwa amri yake, popote alipo taka kufika.
Verse 37
ﯥﯦﯧﯨ
ﯩ
Na tukayafanya mashet'ani yamtumikie, wote wajenzi na wapiga mbizi.
Verse 38
ﯪﯫﯬﯭ
ﯮ
Na wengine wafungwao kwa minyororo.
Verse 39
Hichi ndicho kipawa chetu. Basi toa au zuia, bila ya hisabu.
Verse 40
ﯷﯸﯹﯺﯻﯼ
ﯽ
Na hakika yeye kwetu Sisi ana cheo cha kukaribishwa kwetu, na pahala pazuri pa kurejea.
Verse 41
Na mkumbuke mja wetu Ayubu alipo mwita Mola wake Mlezi akasema: Kwa hakika Shet'ani amenifikishia udhia na adhabu.
Verse 42
(Akaambiwa:) Piga-piga ardhi kwa mguu wako! Basi haya maji baridi ya kuogea na ya kunywa.
Verse 43
Na tukampa ahali zake na wengine kama wao pamoja nao, kuwa ni rehema itokayo kwetu, na iwe kumbusho kwa watu wenye akili.
Verse 44
Na shika kicha cha vijiti tu mkononi mwako, kisha ndio upigie nacho, wala usivunje kiapo. Hakika tulimkuta mwenye subira, mbora wa waja, kwa hakika alikuwa mwingi wa kutubu.
Verse 45
Na wakumbuke waja wetu, Ibrahim na Is-haqa na Yaa'qubu walio kuwa na nguvu na busara.
Verse 46
ﭶﭷﭸﭹﭺ
ﭻ
Sisi tumewakhusisha wao kwa sifa ya ukumbusho wa Akhera.
Verse 47
ﭼﭽﭾﭿﮀ
ﮁ
Na hakika wao kwetu sisi ni wateuliwa walio bora.
Verse 48
Na mkumbuke Ismail na Alyasaa na Dhulkifli, na wote hao ni katika walio bora.
Verse 49
Huu ni ukumbusho. Na hakika wachamngu wana marudio mazuri.
Verse 50
ﮔﮕﮖﮗﮘ
ﮙ
Bustani za milele zitazo funguliwa milango yao kwa ajili yao.
Verse 51
Humo wataegemea matakia, wawe wanaagiza humo matunda mengi na vinywaji.
Verse 52
ﮢﮣﮤﮥﮦ
ﮧ
Na pamoja nao wake zao wenye kutuliza macho, hirimu zao.
Verse 53
ﮨﮩﮪﮫﮬ
ﮭ
Haya ndiyo mliyo ahidiwa kwa Siku ya Hisabu.
Verse 54
Hakika hii ndiyo riziki yetu isiyo malizika.
Verse 55
ﯗﯘﯙﯚﯛﯜ
ﯝ
Ndio hivi! Na hakika wenye kuasi bila ya shaka watapata marudio maovu kabisa;
Verse 56
ﯞﯟﯠﯡ
ﯢ
Nayo ni Jahannamu! Wataingia humo. Nacho hicho ni kitanda kiovu mno cha kulalia.
Verse 57
ﯣﯤﯥﯦ
ﯧ
Ndio hivi! Basi na wayaonje maji ya moto na ya usaha!
Verse 58
ﯨﯩﯪﯫ
ﯬ
Na adhabu nyenginezo za namna hii.
Verse 59
Hili ndilo kundi litakalo ingia pamoja nanyi. Hapana makaribisho mema kwao. Hakika hao wanaingia Motoni.
Verse 60
Waseme: Lakini nyinyi! Hamna mapokezi mazuri! Nyinyi ndio mlio tusabibisha haya, napo ni pahala paovu kabisa!
Verse 61
Waseme: Mola wetu Mlezi! Aliye tusabibisha haya mzidishie adhabu mara mbili Motoni.
Verse 62
Watasema: Tuna nini hata hatuwaoni wale watu ambao tukiwahisabu ndio katika waovu?
Verse 63
ﭜﭝﭞﭟﭠﭡ
ﭢ
Tulikosea tulipo wafanyia maskhara, au macho yetu tu hayawaoni?
Verse 64
ﭣﭤﭥﭦﭧﭨ
ﭩ
Hakika hayo bila ya shaka ndiyo makhasimiano ya watu wa Motoni.
Verse 65
Sema: Hakika mimi ni mwonyaji tu; na hapana mungu ila Mwenyezi Mungu Mmoja, Mtenda nguvu,
Verse 66
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na viliomo baina yake, Mwenye nguvu, Mwenye kusamehe.
Verse 67
ﭿﮀﮁﮂ
ﮃ
Sema: Hii ni khabari kubwa kabisa.
Verse 68
ﮄﮅﮆ
ﮇ
Ambayo nyinyi mnaipuuza.
Verse 69
Sikuwa na ilimu ya mambo ya viumbe wakuu watukufu walipo kuwa wakishindana.
Verse 70
Haikufunuliwa kwangu isipo kuwa ya kwamba hakika mimi ni mwonyaji dhaahiri.
Verse 71
Mola wako Mlezi alipo waambia Malaika: Hakika Mimi nitaumba mtu kutokana na udongo.
Verse 72
Na nitakapo mkamilisha na kumpulizia roho inayo tokana nami, basi muangukieni kwa kumt'ii.
Verse 73
ﮯﮰﮱﯓ
ﯔ
Basi Malaika wakat'ii wote pamoja.
Verse 74
ﯕﯖﯗﯘﯙﯚ
ﯛ
Isipo kuwa Iblisi; alijivuna na akawa katika makafiri.
Verse 75
Mwenyezi Mungu akamwambia: Ewe Iblisi! Kipi kilicho kuzuia kumt'ii yule niliye muumba kwa mikono yangu? Je! Umejiona mkubwa, au umekuwa katika wakuu kweli?
Verse 76
Akasema: Mimi ni bora kuliko yeye. Umeniumba kwa moto, na yeye umemuumba kwa udongo.
Verse 77
ﯷﯸﯹﯺﯻ
ﯼ
Akasema: Basi toka humo, kwani hakika wewe umelaanika.
Verse 78
ﯽﯾﯿﰀﰁﰂ
ﰃ
Na hakika laana yangu itakuwa juu yako mpaka Siku ya Malipo.
Verse 79
ﰄﰅﰆﰇﰈﰉ
ﰊ
Akasema: Mola wangu Mlezi! Nipe muhula mpaka siku watayo fufuliwa viumbe.
Verse 80
ﰋﰌﰍﰎ
ﰏ
Mwenyezi Mungu akasema: Basi umekwisha kuwa miongoni mwa walio pewa muhula,
Verse 81
ﰐﰑﰒﰓ
ﰔ
Mpaka siku ya wakati maalumu.
Verse 82
ﰕﰖﰗﰘ
ﰙ
Akasema (Iblisi): Naapa kwa utukufu wako, bila ya shaka nitawapoteza wote,
Verse 83
ﰚﰛﰜﰝ
ﰞ
Isipo kuwa wale waja wako miongoni mwao walio khitariwa.
Verse 84
ﭑﭒﭓﭔ
ﭕ
Akasema: Haki! Na haki ninaisema.
Verse 85
Bila ya shaka nitaijaza Jahannamu kwa wewe na kwa hao wote wenye kukufuata miongoni mwao.
Verse 86
Sema (Ewe Mtume): Sikuombeni ujira juu ya haya, wala mimi si katika wadanganyifu.
Verse 87
ﭩﭪﭫﭬﭭ
ﭮ
Hayakuwa haya ila ni mawaidha kwa walimwengu wote.
Verse 88
ﭯﭰﭱﭲ
ﭳ
Na bila ya shaka mtajua khabari zake baada ya muda.
تقدم القراءة