Tafsiri ya Sura Al-Kalam kwa السواحلية kutoka Ali Muhsin Al - Swahili translation
Verse 1
ﮉﮊﮋﮌﮍ
ﮎ
Al-Kalam
Nuun. Naapa kwa kalamu na yale wayaandikayo,
Verse 2
ﮏﮐﮑﮒﮓ
ﮔ
Kwa neema ya Mola wako Mlezi wewe si mwendawazimu.
Verse 3
ﮕﮖﮗﮘﮙ
ﮚ
Na kwa hakika wewe una malipo yasiyo katika.
Verse 4
ﮛﮜﮝﮞ
ﮟ
Na hakika wewe una tabia tukufu.
Verse 5
ﮠﮡ
ﮢ
Karibu utaona, na wao wataona,
Verse 6
ﮣﮤ
ﮥ
Ni nani kati yenu aliye pandwa na wazimu.
Verse 7
Hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye ajuaye zaidi nani aliye ipotea Njia yake, na Yeye ndiye anaye wajua zaidi walio ongoka.
Verse 8
ﯓﯔﯕ
ﯖ
Basi usiwat'ii wanao kadhibisha.
Verse 9
ﯗﯘﯙﯚ
ﯛ
Wanatamani lau unge lainisha ili nao wakulainishie.
Verse 10
ﯜﯝﯞﯟﯠ
ﯡ
Wala usimt'ii kila mwingi wa kuapa wa kudharauliwa,
Verse 11
ﯢﯣﯤ
ﯥ
Mtapitapi, apitaye akifitini,
Verse 12
ﯦﯧﯨﯩ
ﯪ
Mwenye kuzuia kheri, dhaalimu, mwingi wa madhambi,
Verse 13
ﯫﯬﯭﯮ
ﯯ
Mkavu, na juu ya hayo, mshari, amejipachika tu.
Verse 14
ﯰﯱﯲﯳﯴ
ﯵ
Ati kwa kuwa ana mali na watoto!
Verse 15
Anapo somewa Aya zetu, husema: Hizi ni simulizi za uwongo za watu wa zamani!
Verse 16
ﯾﯿﰀ
ﰁ
Tutamtia kovu juu ya pua yake.
Verse 17
Hakika tumewajaribu hawa kama tulivyo wajaribu wale wenye shamba, walipo apa kwamba watayavuna mazao yake itakapo kuwa asubuhi.
Verse 18
ﭜﭝ
ﭞ
Wala hawakusema: Mungu akipenda!
Verse 19
Basi lilitokea tukio juu yake kutoka kwa Mola wako Mlezi, nao wamelala!
Verse 20
ﭧﭨ
ﭩ
Likawa kama usiku wa giza.
Verse 21
ﭪﭫ
ﭬ
Asubuhi wakaitana.
Verse 22
Ya kwamba nendeni kondeni mwenu ikiwa mnataka kuvuna.
Verse 23
ﭵﭶﭷ
ﭸ
Basi walikwenda na huku wakinong'onezana,
Verse 24
ﭹﭺﭻﭼﭽﭾ
ﭿ
Ya kuwa leo hata masikini mmoja asikuingilieni.
Verse 25
ﮀﮁﮂﮃ
ﮄ
Na walikwenda asubuhi, nao wameshikilia azimio hilo.
Verse 26
ﮅﮆﮇﮈﮉ
ﮊ
Basi walipo liona, wakasema: Hakika tumepotea!
Verse 27
ﮋﮌﮍ
ﮎ
Bali tumenyimwa!
Verse 28
Mbora wao akasema: Sikukwambieni, kwa nini hamumtakasi Mwenyezi Mungu?
Verse 29
ﮗﮘﮙﮚﮛﮜ
ﮝ
Wakasema: Ametakasika Mola wetu Mlezi! Hakika sisi tulikuwa wenye kudhulumu.
Verse 30
ﮞﮟﮠﮡﮢ
ﮣ
Basi wakakabiliana kulaumiana wao kwa wao.
Verse 31
ﮤﮥﮦﮧﮨ
ﮩ
Wakasema: Ole wetu! Tulikuwa tumeikiuka mipaka!
Verse 32
Asaa Mola wetu Mlezi akatubadilishia lilio bora kuliko hili. Hakika sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.
Verse 33
Namna hivi yanakuwa mateso, na bila ya shaka mateso ya Akhera ni makubwa zaidi, laiti wangeli jua!
Verse 34
ﯡﯢﯣﯤﯥﯦ
ﯧ
Hakika wachamngu watakuwa na Bustani za neema kwa Mola wao Mlezi.
Verse 35
ﯨﯩﯪ
ﯫ
Kwani tutawafanya Waislamu kama wakosefu?
Verse 36
ﯬﯭﯮﯯ
ﯰ
Mna nini? Mnahukumu vipi?
Verse 37
ﯱﯲﯳﯴﯵ
ﯶ
Au mnacho kitabu ambacho ndani yake mnasoma?
Verse 38
ﯷﯸﯹﯺﯻ
ﯼ
Kuwa mtapata humo mnayo yapenda?
Verse 39
Au mnazo ahadi za viapo juu yetu za kufika Siku ya Kiyama ya kuwa hakika mtapata kila mnayo jihukumia?
Verse 40
ﰊﰋﰌﰍ
ﰎ
Waulize: Ni nani miongoni mwao dhamini wa haya?
Verse 41
Au wanao washirika? Basi wawalete washirika wao wakiwa wanasema kweli.
Verse 42
Siku utakapo wekwa wazi mundi, na wataitwa kusujudu, lakini hawataweza,
Verse 43
Macho yao yatainama chini, fedheha itawafunika. Na hakika walikuwa wakiitwa wasujudu walipo kuwa wazima -
Verse 44
Basi niache na wanao kadhibisha maneno haya! Tutawavutia kidogo kidogo kwa mahali wasipo pajua.
Verse 45
ﭪﭫﭬﭭﭮﭯ
ﭰ
Na ninawapururia muhula; hakika hila zangu ni imara.
Verse 46
Au unawaomba ujira, na wao wanaemewa na gharama hiyo?
Verse 47
ﭹﭺﭻﭼﭽ
ﭾ
Au iko kwao siri, basi wao wanaiandika?
Verse 48
Basi ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi, wala usiwe kama mmezwa na samaki, alipo nadi naye kazongwa.
Verse 49
Kama isingeli mfikia neema kutoka kwa Mola wake Mlezi, bila ya shaka angeli tupwa ufukweni naye ni mwenye kulaumiwa.
Verse 50
ﮖﮗﮘﮙﮚ
ﮛ
Lakini Mola wake Mlezi alimteua na akamfanya miongoni mwa watu wema.
Verse 51
Na walio kufuru hukaribia kukutelezesha kwa macho yao, wanapo sikia mawaidha, na wanasema: Hakika yeye ni mwendawazimu.
Verse 52
ﮩﮪﮫﮬﮭ
ﮮ
Na hayakuwa haya, ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.
تقدم القراءة