Tafsiri ya Sura Al-Hakkah kwa السواحلية kutoka Ali Muhsin Al - Swahili translation
Verse 1
ﮯ
ﮰ
Al-Hakkah
Tukio la haki.
Verse 2
ﮱﯓ
ﯔ
Nini hilo Tukio la haki?
Verse 3
ﯕﯖﯗﯘ
ﯙ
Na nini kitakujuulisha nini hilo Tukio la haki?
Verse 4
ﯚﯛﯜﯝ
ﯞ
Thamudi na A'di waliukadhibisha Msiba unao situsha.
Verse 5
ﯟﯠﯡﯢ
ﯣ
Basi Thamudi waliangamizwa kwa balaa kubwa mno.
Verse 6
ﯤﯥﯦﯧﯨﯩ
ﯪ
Na ama A'di waliangamizwa kwa upepo mkali usio zuilika.
Verse 7
Alio wapelekea masiku saba, na siku nane, mfululizo bila ya kusita. Utaona watu wamepinduka kama kwamba ni magongo ya mitende yalio wazi ndani.
Verse 8
ﯼﯽﯾﯿﰀ
ﰁ
Basi je! Unamwona mmoja wao aliye baki?
Verse 9
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖ
ﭗ
Na Firauni na walio mtangulia, na miji iliyo pinduliwa chini juu, walileta khatia.
Verse 10
ﭘﭙﭚﭛﭜﭝ
ﭞ
Wakamuasi Mtume wa Mola wao Mlezi, ndipo Yeye Mola akawakamata kwa mkamato ulio zidi nguvu.
Verse 11
Maji yalipo furika Sisi tulikupandisheni katika safina,
Verse 12
ﭧﭨﭩﭪﭫﭬ
ﭭ
Ili tuyafanye hayo kuwa ni waadhi kwenu na kila sikio linalo sikia liyahifadhi.
Verse 13
ﭮﭯﭰﭱﭲﭳ
ﭴ
Na litapo pulizwa barugumu mpulizo mmoja tu,
Verse 14
ﭵﭶﭷﭸﭹﭺ
ﭻ
Na ardhi na milima ikaondolewa, na ikavunjwa kwa mvunjo mmoja,
Verse 15
ﭼﭽﭾ
ﭿ
Siku hiyo ndio Tukio litatukia.
Verse 16
ﮀﮁﮂﮃﮄ
ﮅ
Na mbingu zitapasuka, kwani siku hiyo zitakuwa dhaifu kabisa.
Verse 17
Na Malaika watakuwa pembezoni mwa mbingu; na wanane juu ya hawa watakuwa wamebeba Kiti cha Enzi cha Mola wako Mlezi.
Verse 18
ﮑﮒﮓﮔﮕﮖ
ﮗ
Siku hiyo mtahudhurishwa - haitafichika siri yoyote yenu.
Verse 19
Basi ama atakaye pewa kitabu chake kwa mkono wake wa kulia, atasema: Haya someni kitabu changu!
Verse 20
ﮢﮣﮤﮥﮦ
ﮧ
Hakika nalijua ya kuwa nitapokea hisabu yangu.
Verse 21
ﮨﮩﮪﮫ
ﮬ
Basi yeye atakuwa katika maisha ya kupendeza,
Verse 22
ﮭﮮﮯ
ﮰ
Katika Bustani ya juu,
Verse 23
ﮱﯓ
ﯔ
Matunda yake yakaribu.
Verse 24
Waambiwe: Kuleni na mnywe kwa furaha kwa sababu ya mlivyo tanguliza katika siku zilizo pita.
Verse 25
Na ama atakaye pewa kitabu chake katika mkono wake wa kushoto, basi yeye atasema: Laiti nisingeli pewa kitabu changu!
Verse 26
ﯩﯪﯫﯬ
ﯭ
Wala nisingeli jua nini hisabu yangu.
Verse 27
ﯮﯯﯰ
ﯱ
Laiti mauti ndiyo yangeli kuwa ya kunimaliza kabisa.
Verse 28
ﯲﯳﯴﯵﯶ
ﯷ
Mali yangu hayakunifaa kitu.
Verse 29
ﯸﯹﯺ
ﯻ
Madaraka yangu yamenipotea.
Verse 30
ﯼﯽ
ﯾ
(Pasemwe): Mshikeni! Mtieni pingu!
Verse 31
ﯿﰀﰁ
ﰂ
Kisha mtupeni Motoni!
Verse 32
Tena mtatizeni katika mnyororo wenye urefu wa dhiraa sabiini!
Verse 33
ﰋﰌﰍﰎﰏﰐ
ﰑ
Kwani huyo hakika alikuwa hamuamini Mwenyezi Mungu Mtukufu,
Verse 34
ﰒﰓﰔﰕﰖ
ﰗ
Wala hahimizi kulisha masikini.
Verse 35
ﰘﰙﰚﰛﰜ
ﰝ
Basi leo hapa hana jamaa wa kumwonea uchungu,
Verse 36
ﭑﭒﭓﭔﭕ
ﭖ
Wala hana chakula ila usaha wa watu wa Motoni.
Verse 37
ﭗﭘﭙﭚ
ﭛ
Chakula hicho hawakili ila wakosefu.
Verse 38
ﭜﭝﭞﭟ
ﭠ
Basi naapa kwa mnavyo viona,
Verse 39
ﭡﭢﭣ
ﭤ
Na msivyo viona,
Verse 40
ﭥﭦﭧﭨ
ﭩ
Kwa hakika hii ni kauli iliyo letwa na Mjumbe mwenye hishima.
Verse 41
Wala si kauli ya mtunga mashairi. Ni machache sana mnayo yaamini.
Verse 42
Wala si kauli ya kuhani. Ni machache mnayo yakumbuka.
Verse 43
ﭻﭼﭽﭾ
ﭿ
Ni uteremsho utokao kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Verse 44
ﮀﮁﮂﮃﮄ
ﮅ
Na lau kama angeli tuzulia baadhi ya maneno tu,
Verse 45
ﮆﮇﮈ
ﮉ
Bila ya shaka tungeli mshika kwa mkono wa kulia,
Verse 46
ﮊﮋﮌﮍ
ﮎ
Kisha kwa hakika tungeli mkata mshipa mkubwa wa moyo!
Verse 47
ﮏﮐﮑﮒﮓﮔ
ﮕ
Na hapana yeyote katika nyinyi ambaye angeli weza kutuzuia.
Verse 48
ﮖﮗﮘ
ﮙ
Kwa hakika hii ni mawaidha kwa wachamngu.
Verse 49
ﮚﮛﮜﮝﮞ
ﮟ
Na hakika Sisi bila ya shaka tunajua kwamba miongoni mwenu wapo wanao kadhibisha.
Verse 50
ﮠﮡﮢﮣ
ﮤ
Na hakika bila ya shaka itakuwa ni majuto kwa wanao kataa.
Verse 51
ﮥﮦﮧ
ﮨ
Na hakika hii bila ya shaka ni haki ya yakini.
Verse 52
ﮩﮪﮫﮬ
ﮭ
Basi litakase jina la Mola wako Mlezi Mtukufu.
تقدم القراءة