Tafsiri ya Sura Abasa kwa السواحلية kutoka Ali Muhsin Al - Swahili translation
Verse 1
ﭑﭒ
ﭓ
Abasa
Alikunja kipaji na akageuka,
Verse 2
ﭔﭕﭖ
ﭗ
Kwa sababu alimjia kipofu!
Verse 3
ﭘﭙﭚﭛ
ﭜ
Na nini kitakujuulisha pengine yeye atatakasika?
Verse 4
ﭝﭞﭟﭠ
ﭡ
Au atawaidhika, na mawaidha yamfae?
Verse 5
ﭢﭣﭤ
ﭥ
Ama ajionaye hana haja,
Verse 6
ﭦﭧﭨ
ﭩ
Wewe ndio unamshughulikia?
Verse 7
ﭪﭫﭬﭭ
ﭮ
Na si juu yako kama hakutakasika.
Verse 8
ﭯﭰﭱﭲ
ﭳ
Ama anaye kujia kwa juhudi,
Verse 9
ﭴﭵ
ﭶ
Naye anaogopa,
Verse 10
ﭷﭸﭹ
ﭺ
Ndio wewe unampuuza?
Verse 11
ﭻﭼﭽ
ﭾ
Sivyo hivyo! Huku ni kukumbushana.
Verse 12
ﭿﮀﮁ
ﮂ
Basi anaye penda akumbuke.
Verse 13
ﮃﮄﮅ
ﮆ
Yamo katika kurasa zilizo hishimiwa,
Verse 14
ﮇﮈ
ﮉ
Zilizo inuliwa, zilizo takaswa.
Verse 15
ﮊﮋ
ﮌ
Zimo mikononi mwa Malaika waandishi,
Verse 16
ﮍﮎ
ﮏ
Watukufu, wema.
Verse 17
ﮐﮑﮒﮓ
ﮔ
Ameangamia mwanaadamu! Nini kinacho mkufurisha?
Verse 18
ﮕﮖﮗﮘ
ﮙ
Kwa kitu gani amemuumba?
Verse 19
ﮚﮛﮜﮝ
ﮞ
Kwa tone la manii, akamuumba na akamkadiria.
Verse 20
ﮟﮠﮡ
ﮢ
Kisha akamsahilishia njia.
Verse 21
ﮣﮤﮥ
ﮦ
Kisha akamfisha, akamtia kaburini.
Verse 22
ﮧﮨﮩﮪ
ﮫ
Kisha apendapo atamfufua.
Verse 23
ﮬﮭﮮﮯﮰ
ﮱ
La! Hajamaliza aliyo muamuru.
Verse 24
ﯓﯔﯕﯖ
ﯗ
Hebu mtu na atazame chakula chake.
Verse 25
ﯘﯙﯚﯛ
ﯜ
Hakika Sisi tumemimina maji kwa nguvu,
Verse 26
ﯝﯞﯟﯠ
ﯡ
Tena tukaipasua pasua ardhi kwa nguvu,
Verse 27
ﯢﯣﯤ
ﯥ
Kisha tukaotesha humo nafaka,
Verse 28
ﯦﯧ
ﯨ
Na zabibu, na mimea ya majani,
Verse 29
ﯩﯪ
ﯫ
Na mizaituni, na mitende,
Verse 30
ﯬﯭ
ﯮ
Na bustani zenye miti iliyo songana baraabara,
Verse 31
ﯯﯰ
ﯱ
Na matunda, na malisho ya wanyama;
Verse 32
ﯲﯳﯴ
ﯵ
Kwa manufaa yenu na mifugo yenu.
Verse 33
ﯶﯷﯸ
ﯹ
Basi utakapo kuja ukelele,
Verse 34
ﯺﯻﯼﯽﯾ
ﯿ
Siku ambayo mtu atamkimbia nduguye,
Verse 35
ﰀﰁ
ﰂ
Na mamaye na babaye,
Verse 36
ﰃﰄ
ﰅ
Na mkewe na wanawe -
Verse 37
ﰆﰇﰈﰉﰊﰋ
ﰌ
Kila mtu miongoni mwao siku hiyo atakuwa na lake la kumtosha.
Verse 38
ﰍﰎﰏ
ﰐ
Siku hiyo ziko nyuso zitazo nawiri,
Verse 39
ﰑﰒ
ﰓ
Zitacheka, zitachangamka;
Verse 40
ﰔﰕﰖﰗ
ﰘ
Na nyuso siku hiyo zitakuwa na mavumbi,
Verse 41
ﭑﭒ
ﭓ
Giza totoro litazifunika,
Verse 42
ﭔﭕﭖﭗ
ﭘ
Hao ndio makafiri watenda maovu.
تقدم القراءة