Tafsiri ya Sura Al-Insan kwa السواحلية kutoka Ali Muhsin Al - Swahili translation
Verse 1
Al-Insan
Hakika kilimpitia binaadamu kipindi katika zama ambacho kwamba hakuwa kitu kinacho tajwa.
Verse 2
Hakika Sisi tumemuumba mtu kutokana na mbegu ya uhai iliyo changanyika, tumfanyie mtihani. Kwa hivyo tukamfanya mwenye kusikia, mwenye kuona.
Verse 3
Hakika Sisi tumembainishia Njia. Ama ni mwenye kushukuru, au mwenye kukufuru.
Verse 4
ﯻﯼﯽﯾﯿﰀ
ﰁ
Hakika Sisi tumewaandalia makafiri minyororo na pingu na Moto mkali.
Verse 5
Hakika watu wema watakunywa katika vinywaji vilivyo changanyika na kafuri,
Verse 6
Ni chemchem watakao inywa waja wa Mwenyezi Mungu, wakiifanya imiminike kwa wingi.
Verse 7
Wanatimiza ahadi, na wanaiogopa siku ambayo shari yake inaenea sana,
Verse 8
Na huwalisha chakula, juu ya kukipenda kwake, masikini, na yatima, na wafungwa.
Verse 9
Hakika sisi tunakulisheni kwa wajihi wa Mwenyezi Mungu. Hatutaki kwenu malipo wala shukrani.
Verse 10
Hakika sisi tunaiogopa kwa Mola wetu Mlezi hiyo siku yenye shida na taabu.
Verse 11
Basi Mwenyezi Mungu atawalinda na shari ya siku hiyo, na atawakutanisha na raha na furaha.
Verse 12
ﮅﮆﮇﮈﮉ
ﮊ
Na atawajazi Bustani za Peponi na maguo ya hariri kwa vile walivyo subiri.
Verse 13
Humo wataegemea juu ya viti vya enzi, hawataona humo jua kali wala baridi kali.
Verse 14
ﮗﮘﮙﮚﮛﮜ
ﮝ
Na vivuli vyake vitakuwa karibu yao, na mashada ya matunda yataning'inia mpaka chini.
Verse 15
Na watapitishiwa vyombo vya fedha na vikombe vya vigae,
Verse 16
ﮧﮨﮩﮪﮫ
ﮬ
Vya fedha safi kama kiyoo, wamevipima kwa vipimo.
Verse 17
ﮭﮮﮯﮰﮱﯓ
ﯔ
Na humo watanyweshwa kinywaji kilicho changanyika na tangawizi.
Verse 18
ﯕﯖﯗﯘ
ﯙ
Hiyo ni chemchem iliyo humo inaitwa Salsabil.
Verse 19
Na watawazungukia kuwatumikia wavulana wasio pevuka, ukiwaona utawafikiri ni lulu zilizo tawanywa.
Verse 20
Na utakapo yaona, utakuwa umeona neema na ufalme mkubwa.
Verse 21
Juu yao zipo nguo za hariri laini za kijani kibichi, na hariri nzito ya at'ilasi. Na watavikwa vikuku vya fedha, na Mola wao Mlezi atawanywesha kinywaji safi kabisa.
Verse 22
Hakika haya ni malipo yenu; na juhudi zenu zimekubaliwa.
Verse 23
ﰅﰆﰇﰈﰉﰊ
ﰋ
Hakika Sisi tumekuteremshia Qur'ani kidogo kidogo.
Verse 24
Basi ngojea hukumu ya Mola wako Mlezi wala usimt'ii miongoni mwao mwenye dhambi au mwenye kufuru.
Verse 25
ﰖﰗﰘﰙﰚ
ﰛ
Na likumbuke jina la Mola wako Mlezi asubuhi na jioni;
Verse 26
Na usiku msujudie Yeye, na umtakase usiku, wakati mrefu.
Verse 27
Kwa hakika watu hawa wanapenda maisha ya kidunia, na wanaiacha nyuma yao siku nzito.
Verse 28
Sisi tumewaumba, na tukavitia nguvu viungo vyao. Na tukitaka tutawabadilisha mfano wao wawe badala yao.
Verse 29
Hakika haya ni mawaidha; basi anaye taka atashika Njia ya kwenda kwa Mola wake Mlezi.
Verse 30
Wala hamwezi kutaka ila atakapo Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye ilimu, Mwenye hikima.
Verse 31
Humuingiza amtakaye katika rehema yake. Na wenye kudhulumu amewawekea adhabu iliyo chungu.
تقدم القراءة