Tafsiri ya Sura An-Takwir kwa السواحلية kutoka Ali Muhsin Al - Swahili translation
Verse 1
ﭙﭚﭛ
ﭜ
An-Takwir
Jua litakapo kunjwa,
Verse 2
ﭝﭞﭟ
ﭠ
Na nyota zikazimwa,
Verse 3
ﭡﭢﭣ
ﭤ
Na milima ikaondolewa,
Verse 4
ﭥﭦﭧ
ﭨ
Na ngamia wenye mimba pevu watakapo achwa wasishughulikiwe,
Verse 5
ﭩﭪﭫ
ﭬ
Na wanyama wa mwituni wakakusanywa,
Verse 6
ﭭﭮﭯ
ﭰ
Na bahari zikawaka moto,
Verse 7
ﭱﭲﭳ
ﭴ
Na nafsi zikaunganishwa,
Verse 8
ﭵﭶﭷ
ﭸ
Na msichana aliye zikwa hai atapo ulizwa,
Verse 9
ﭹﭺﭻ
ﭼ
Kwa kosa gani aliuliwa?
Verse 10
ﭽﭾﭿ
ﮀ
Na madaftari yatakapo enezwa,
Verse 11
ﮁﮂﮃ
ﮄ
Na mbingu itapo tanduliwa,
Verse 12
ﮅﮆﮇ
ﮈ
Na Jahannamu itapo chochewa,
Verse 13
ﮉﮊﮋ
ﮌ
Na Pepo ikasogezwa,
Verse 14
ﮍﮎﮏﮐ
ﮑ
Kila nafsi itajua ilicho kihudhurisha.
Verse 15
ﮒﮓﮔ
ﮕ
Naapa kwa nyota zinapo rejea nyuma,
Verse 16
ﮖﮗ
ﮘ
Zinazo kwenda, kisha zikajificha,
Verse 17
ﮙﮚﮛ
ﮜ
Na kwa usiku unapo pungua,
Verse 18
ﮝﮞﮟ
ﮠ
Na kwa asubuhi inapo pambazuka,
Verse 19
ﮡﮢﮣﮤ
ﮥ
Kwamba hakika bila ya shaka hii ni kauli ya Mjumbe mtukufu,
Verse 20
ﮦﮧﮨﮩﮪﮫ
ﮬ
Mwenye nguvu na mwenye cheo kwa huyo Mwenye Kiti cha Enzi,
Verse 21
ﮭﮮﮯ
ﮰ
Anaye t'iiwa, tena muaminifu.
Verse 22
ﮱﯓﯔ
ﯕ
Na wala huyu mwenzenu hana wazimu.
Verse 23
ﯖﯗﯘﯙ
ﯚ
Na hakika yeye alimwona kwenye upeo wa macho ulio safi.
Verse 24
ﯛﯜﯝﯞﯟ
ﯠ
Wala yeye si bakhili kwa mambo ya ghaibu.
Verse 25
ﯡﯢﯣﯤﯥ
ﯦ
Wala hii si kauli ya Shetani maluuni.
Verse 26
ﯧﯨ
ﯩ
Basi mnakwenda wapi?
Verse 27
ﯪﯫﯬﯭﯮ
ﯯ
Haikuwa hii ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.
Verse 28
ﯰﯱﯲﯳﯴ
ﯵ
Kwa yule miongoni mwenu anaye taka kwenda sawa.
Verse 29
Wala nyinyi hamtataka isipo kuwa atake Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.
تقدم القراءة