Tafsiri ya Sura Al-Fajr kwa السواحلية kutoka Ali Muhsin Al - Swahili translation
Verse 1
ﭤ
ﭥ
Al-Fajr
Naapa kwa alfajiri,
Verse 2
ﭦﭧ
ﭨ
Na kwa masiku kumi,
Verse 3
ﭩﭪ
ﭫ
Na kwa viwili viwili na kimoja kimoja,
Verse 4
ﭬﭭﭮ
ﭯ
Na kwa usiku unapo pita,
Verse 5
ﭰﭱﭲﭳﭴﭵ
ﭶ
Je! Hapana katika haya kiapo kwa mwenye akili?
Verse 6
ﭷﭸﭹﭺﭻﭼ
ﭽ
Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo wafanya kina A'di?
Verse 7
ﭾﭿﮀ
ﮁ
Wa Iram, wenye majumba marefu?
Verse 8
ﮂﮃﮄﮅﮆﮇ
ﮈ
Ambao haukuumbwa mfano wake katika nchi?
Verse 9
ﮉﮊﮋﮌﮍ
ﮎ
Na Thamudi walio chonga majabali huko bondeni?
Verse 10
ﮏﮐﮑ
ﮒ
Na Firauni mwenye vigingi?
Verse 11
ﮓﮔﮕﮖ
ﮗ
Ambao walifanya jeuri katika nchi?
Verse 12
ﮘﮙﮚ
ﮛ
Wakakithirisha humo ufisadi?
Verse 13
ﮜﮝﮞﮟﮠ
ﮡ
Basi Mola wako Mlezi aliwapiga mjeledi wa adhabu.
Verse 14
ﮢﮣﮤ
ﮥ
Hakika Mola wako Mlezi yupo kwenye mavizio anawavizia.
Verse 15
Ama mtu anapo jaribiwa na Mola wake Mlezi, akamkirimu na akamneemesha, husema: Mola wangu Mlezi amenikirimu!
Verse 16
Na ama anapo mjaribu akampunguzia riziki yake, husema: Mola wangu Mlezi amenitia unyonge!
Verse 17
ﯞﯟﯠﯡﯢﯣ
ﯤ
Sivyo hivyo! Bali nyinyi hamuwakirimu mayatima,
Verse 18
ﯥﯦﯧﯨﯩ
ﯪ
Wala hamhimizani kulisha masikini;
Verse 19
ﯫﯬﯭﯮ
ﯯ
Na mnakula urithi kwa ulaji wa pupa,
Verse 20
ﯰﯱﯲﯳ
ﯴ
Na mnapenda mali pendo la kupita kiasi.
Verse 21
Sivyo hivyo! Itakapo vunjwa ardhi vipande vipande,
Verse 22
ﯽﯾﯿﰀﰁ
ﰂ
Na akaja Mola wako Mlezi na Malaika safu safu,
Verse 23
Na ikaletwa Jahannamu siku hiyo, siku hiyo mtu atakumbuka! Lakini kukumbuka huko kutamfaa nini?
Verse 24
ﭜﭝﭞﭟ
ﭠ
Atasema: Laiti ningeli jitangulizia kwa uhai wangu!
Verse 25
ﭡﭢﭣﭤﭥ
ﭦ
Basi siku hiyo hataadhibu yeyote namna ya kuadhibu kwake.
Verse 26
ﭧﭨﭩﭪ
ﭫ
Wala hatafunga yeyote kama kufunga kwake.
Verse 27
ﭬﭭﭮ
ﭯ
Ewe nafsi iliyo tua!
Verse 28
ﭰﭱﭲﭳﭴ
ﭵ
Rejea kwa Mola wako Mlezi umeridhika, na umemridhisha.
Verse 29
ﭶﭷﭸ
ﭹ
Basi ingia miongoni mwa waja wangu,
Verse 30
ﭺﭻ
ﭼ
Na ingia katika Pepo yangu.
تقدم القراءة