Tafsiri ya Sura Az-Zariyat kwa السواحلية kutoka Ali Muhsin Al - Swahili translation
Verse 1
ﯤﯥ
ﯦ
Az-Zariyat
Naapa kwa pepo zinazo tawanya,
Verse 2
ﯧﯨ
ﯩ
Na zinazo beba mizigo,
Verse 3
ﯪﯫ
ﯬ
Na zinazo kwenda kwa wepesi.
Verse 4
ﯭﯮ
ﯯ
Na zinazo gawanya kwa amri,
Verse 5
ﯰﯱﯲ
ﯳ
Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka ni kweli,
Verse 6
ﯴﯵﯶ
ﯷ
Na kwa hakika malipo bila ya shaka yatatokea.
Verse 7
ﭑﭒﭓ
ﭔ
Naapa kwa mbingu zenye njia,
Verse 8
ﭕﭖﭗﭘ
ﭙ
Hakika nyinyi bila ya shaka mmo katika kauli inayo khitalifiana.
Verse 9
ﭚﭛﭜﭝ
ﭞ
Anageuzwa kutokana na haki mwenye kugeuzwa.
Verse 10
ﭟﭠ
ﭡ
Wazushi wameangamizwa.
Verse 11
ﭢﭣﭤﭥﭦ
ﭧ
Ambao wameghafilika katika ujinga.
Verse 12
ﭨﭩﭪﭫ
ﭬ
Wanauliza: Ni lini hiyo siku ya malipo?
Verse 13
ﭭﭮﭯﭰﭱ
ﭲ
Hiyo ni siku watakayo adhibiwa Motoni.
Verse 14
Onjeni adhabu yenu! Haya ndiyo mliyo kuwa mkiyahimiza.
Verse 15
ﭻﭼﭽﭾﭿ
ﮀ
Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na chemchem.
Verse 16
Wanapokea aliyo wapa Mola wao Mlezi. Kwa hakika hao walikuwa kabla ya haya wakifanya mema.
Verse 17
ﮌﮍﮎﮏﮐﮑ
ﮒ
Walikuwa wakilala kidogo tu usiku.
Verse 18
ﮓﮔﮕ
ﮖ
Na kabla ya alfajiri wakiomba maghfira.
Verse 19
ﮗﮘﮙﮚﮛ
ﮜ
Na katika mali yao ipo haki ya mwenye kuomba na asiye omba.
Verse 20
ﮝﮞﮟﮠ
ﮡ
Na katika ardhi zipo Ishara kwa wenye yakini.
Verse 21
ﮢﮣﮤﮥﮦ
ﮧ
Na pia katika nafsi zenu - Je! Hamwoni?
Verse 22
ﮨﮩﮪﮫﮬ
ﮭ
Na katika mbingu ziko riziki zenu na mliyo ahidiwa.
Verse 23
Basi naapa kwa Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, hakika haya ni kweli kama ilivyo kweli kuwa nyinyi mnasema.
Verse 24
ﯙﯚﯛﯜﯝﯞ
ﯟ
Je! Imekufikia hadithi ya wageni wa Ibrahim wanao hishimiwa?
Verse 25
Walipo ingia kwake wakasema: Salama! Na yeye akasema: Salama! Nyinyi ni watu nisio kujueni.
Verse 26
ﯫﯬﯭﯮﯯﯰ
ﯱ
Akenda kwa ahali yake na akaja na ndama aliye nona.
Verse 27
ﯲﯳﯴﯵﯶ
ﯷ
Akawakaribisha, akasema: Mbona hamli?
Verse 28
Akahisi kuwaogopa katika nafsi yake. Wakasema: Usiwe na khofu, nao wakambashiria kupata kijana mwenye ilimu.
Verse 29
Ndipo mkewe akawaelekea, na huku anasema na akijipiga usoni kwa mastaajabu, na kusema: Mimi ni kikongwe na tasa!
Verse 30
Wakasema: Ndivyo vivyo hivyo alivyo sema Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye hikima na Mwenye kujua.
Verse 31
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖ
ﭗ
AKASEMA: Basi ujumbe wenu ni nini, enyi mlio tumwa?
Verse 32
ﭘﭙﭚﭛﭜﭝ
ﭞ
Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwa watu wakosefu,
Verse 33
ﭟﭠﭡﭢﭣ
ﭤ
Tuwatupie mawe ya udongo,
Verse 34
ﭥﭦﭧﭨ
ﭩ
Yaliyo tiwa alama kutoka kwa Mola wako Mlezi kwa ajili ya wanao pindukia mipaka.
Verse 35
ﭪﭫﭬﭭﭮﭯ
ﭰ
Kwa hivyo tutawatoa katika hao wale walio amini.
Verse 36
Lakini hatukupata humo ila nyumba moja tu yenye Waislamu!
Verse 37
Na tukaacha humo Ishara kwa ajili ya wanao iogopa adhabu chungu.
Verse 38
Na katika khabari za Musa, tulipo mtuma kwa Firauni na hoja wazi.
Verse 39
ﮊﮋﮌﮍﮎﮏ
ﮐ
Lakini alipuuza kwa sababu ya nguvu zake na akasema: Huyu ni mchawi au mwendawazimu!
Verse 40
Basi tukamkamata yeye na majeshi yake na tukawatupa baharini, na yeye ndiye wa kulaumiwa.
Verse 41
Na katika khabari za A'di tulipo wapelekea upepo wa kukata uzazi.
Verse 42
Haukuacha chochote ulicho kifikia ila ulikifanya kama kilio nyambuka.
Verse 43
Na katika khabari za Thamudi walipo ambiwa: Jifurahisheni kwa muda mdogo tu.
Verse 44
Wakaasi amri ya Mola wao Mlezi. Basi uliwanyakua moto wa radi nao wanaona.
Verse 45
Basi hawakuweza kusimama wala hawakuwa wenye kujitetea.
Verse 46
Na kaumu ya Nuhu hapo mbele. Hakika hao walikuwa watu wapotovu.
Verse 47
ﯰﯱﯲﯳﯴ
ﯵ
Na mbingu tumezifanya kwa nguvu na uwezo na hakika Sisi bila ya shaka ndio twenye uwezo wa kuzitanua.
Verse 48
ﯶﯷﯸﯹ
ﯺ
Na ardhi tumeitandaza; basi watandazaji wazuri namna gani Sisi!
Verse 49
Na katika kila kitu tumeumba kwa jozi ili mzingatie.
Verse 50
Basi kimbilieni kwa Mwenyezi Mungu, hakika mimi ni mwonyaji kwenu wa kubainisha nitokae kwake.
Verse 51
Wala msifanye kuwa kuna mungu mwengine pamoja na Mwenyezi Mungu. Hakika mimi ni mwonyaji kwenu wa kubainisha nitokae kwake.
Verse 52
Basi ndio hivyo hivyo, hakuwajia kabla yao Mtume ila walisema: Huyu ni mchawi au mwendawazimu.
Verse 53
Je! Wameambizana kwa haya? Bali hawa ni watu waasi.
Verse 54
ﭧﭨﭩﭪﭫ
ﭬ
Basi waachilie mbali, nawe hulaumiwi.
Verse 55
ﭭﭮﭯﭰﭱ
ﭲ
Na kumbusha, kwani ukumbusho huwafaa Waumini.
Verse 56
ﭳﭴﭵﭶﭷﭸ
ﭹ
Nami sikuwaumba majini na watu ila waniabudu Mimi.
Verse 57
Na sitaki kwao riziki, wala sitaki wanilishe.
Verse 58
Hakika Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kuruzuku, Mwenye nguvu, Madhubuti.
Verse 59
Hakika walio dhulumu wana fungu lao la adhabu kama fungu la wenzao. Basi wasinihimize.
Verse 60
Ole wao walio ikanusha siku yao waliyo ahidiwa.
تقدم القراءة