Tafsiri ya Sura At-Tarik kwa السواحلية kutoka Ali Muhsin Al - Swahili translation
Verse 1
ﭑﭒ
ﭓ
At-Tarik
Naapa kwa mbingu na Kinacho kuja usiku!
Verse 2
ﭔﭕﭖﭗ
ﭘ
Na nini kitakacho kujuulisha ni nini hicho Kinacho kuja usiku?
Verse 3
ﭙﭚ
ﭛ
Ni Nyota yenye mwanga mkali.
Verse 4
ﭜﭝﭞﭟﭠﭡ
ﭢ
Hapana nafsi ila inayo mwangalizi.
Verse 5
ﭣﭤﭥﭦ
ﭧ
Hebu naajitazame mwanaadamu ameumbwa kwa kitu gani?
Verse 6
ﭨﭩﭪﭫ
ﭬ
Ameumbwa kwa maji yatokayo kwa kuchupa,
Verse 7
ﭭﭮﭯﭰﭱ
ﭲ
Yatokayo baina ya mifupa ya mgongo na mbavu.
Verse 8
ﭳﭴﭵﭶ
ﭷ
Hakika Yeye ana uweza wa kumrudisha.
Verse 9
ﭸﭹﭺ
ﭻ
Siku zitakapo dhihirishwa siri.
Verse 10
ﭼﭽﭾﭿﮀﮁ
ﮂ
Basi hatakuwa na nguvu wala msaidizi.
Verse 11
ﮃﮄﮅ
ﮆ
Naapa kwa mbingu yenye marejeo!
Verse 12
ﮇﮈﮉ
ﮊ
Na kwa ardhi inayo pasuka!
Verse 13
ﮋﮌﮍ
ﮎ
Hakika hii ni kauli ya kupambanua.
Verse 14
ﮏﮐﮑ
ﮒ
Wala si mzaha.
Verse 15
ﮓﮔﮕ
ﮖ
Hakika wao wanapanga mpango.
Verse 16
ﮗﮘ
ﮙ
Na Mimi napanga mpango.
Verse 17
ﮚﮛﮜﮝ
ﮞ
Basi wape muhula makafiri - wape muhula pole pole.
تقدم القراءة