Tafsiri ya Sura Al-Buruj kwa السواحلية kutoka Ali Muhsin Al - Swahili translation
Verse 1
ﭛﭜﭝ
ﭞ
Al-Buruj
Naapa kwa mbingu yenye Buruji!
Verse 2
ﭟﭠ
ﭡ
Na kwa siku iliyo ahidiwa!
Verse 3
ﭢﭣ
ﭤ
Na kwa shahidi na kinacho shuhudiwa!
Verse 4
ﭥﭦﭧ
ﭨ
Wameangamizwa watu wa makhandaki
Verse 5
ﭩﭪﭫ
ﭬ
Yenye moto wenye kuni nyingi,
Verse 6
ﭭﭮﭯﭰ
ﭱ
Walipo kuwa wamekaa hapo,
Verse 7
ﭲﭳﭴﭵﭶﭷ
ﭸ
Na wao ni mashahidi wa yale waliyo kuwa wakiwafanyia Waumini.
Verse 8
Nao hawakuona baya lolote kwao ila kuwa wakimuamini Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu, Msifiwa,
Verse 9
Ambaye anao ufalme wa mbingu na ardhi; na Mwenyezi Mungu ni shaahidi wa kila kitu.
Verse 10
Hakika walio wafitini Waumini wanaume na Waumini wanawake, kisha hawakutubu, basi watapata adhabu ya Jahannamu na watapata adhabu ya kuungua.
Verse 11
Hakika walio amini na wakatenda mema watapata Bustani zenye mito ipitayo kati yake. Huko ndiko kufuzu kukubwa.
Verse 12
ﮮﮯﮰﮱ
ﯓ
Hakika kutesa kwa Mola wako Mlezi ni kukali.
Verse 13
ﯔﯕﯖﯗ
ﯘ
Yeye ndiye anaye anzisha na ndiye anaye rejeza tena,
Verse 14
ﯙﯚﯛ
ﯜ
Naye ni Mwenye kusamehe, Mwenye mapenzi,
Verse 15
ﯝﯞﯟ
ﯠ
Mwenye Kiti cha Enzi, Mtukufu,
Verse 16
ﯡﯢﯣ
ﯤ
Atendaye ayatakayo.
Verse 17
ﯥﯦﯧﯨ
ﯩ
Je! Zimekuwasilia khabari za majeshi?
Verse 18
ﯪﯫ
ﯬ
Ya Firauni na Thamudi?
Verse 19
ﯭﯮﯯﯰﯱ
ﯲ
Lakini walio kufuru wamo katika kukadhibisha.
Verse 20
ﯳﯴﯵﯶ
ﯷ
Na Mwenyezi Mungu nyuma yao amewazunguka.
Verse 21
ﯸﯹﯺﯻ
ﯼ
Bali hii ni Qur'ani tukufu
Verse 22
ﯽﯾﯿ
ﰀ
Katika Ubao Ulio Hifadhiwa.
تقدم القراءة