Tafsiri ya Sura A-Hijr kwa السواحلية kutoka Ali Muhsin Al - Swahili translation
Verse 1
A-Hijr
Alif Lam Ra. (A. L. R). Hizi ni Aya za Kitabu na Qur'ani inayo bainisha.
Verse 2
HUENDA ikawa walio kufuru wakatamani wange kuwa Waislamu.
Verse 3
Waache wale, na wastarehe, na iwazuge tamaa. Watakuja jua.
Verse 4
Na hatukuuangamiza mji wowote ule ila ulikuwa na muda wake maalumu.
Verse 5
Hawawezi watu wowote kuitangulia ajali yao, wala kuchelewa.
Verse 6
Na walisema: Ewe uliyeteremshiwa Ukumbusho! Hakika wewe ni mwendawazimu.
Verse 7
Mbona hutuletei Malaika ikiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli?
Verse 8
Sisi hatuwateremshi Malaika ila kwa sababu ya haki, na hapo hawatapewa muhula.
Verse 9
Hakika Sisi ndio tulio teremsha Ukumbusho huu, na hakika Sisi ndio tutao ulinda.
Verse 10
Na hakika tulikwisha watumia Mitume mataifa ya mwanzo.
Verse 11
Na hakuwafikia Mtume ila walimkejeli.
Verse 12
ﮰﮱﯓﯔﯕ
ﯖ
Na kama hivi ndivyo tunavyo ingiza katika nyoyo za wakosefu.
Verse 13
Hawayaamini haya, na hali ya kuwa umekwisha wapitia mfano wa watu wa kale.
Verse 14
Na lau tungeli wafungulia mlango wa mbingu, wakawa wanapanda,
Verse 15
Basi wangeli sema: Macho yetu yamelevywa, bali sisi wenyewe tumerogwa.
Verse 16
Na hakika tumeweka katika mbingu vituo vya sayari, na tumezipamba kwa wenye kuangalia.
Verse 17
ﭙﭚﭛﭜﭝ
ﭞ
Na tumezilinda na kila shetani afukuzwaye.
Verse 18
Isipo kuwa mwenye kusikiliza kwa kuibia, naye hufuatwa na kijinga cha moto kinacho onekana.
Verse 19
Na ardhi tumeitandaza na humo tumeweka milima, na tumeotesha kila kitu kwa kiasi chake.
Verse 20
Na tumekujaalieni humo vitu vya maisha yenu, na ya hao ambao nyinyi sio wenye kuwaruzuku.
Verse 21
Na hakuna chochote ila asili yake inatokana na Sisi; wala hatukiteremshi ila kwa kipimo maalumu.
Verse 22
Na tunazipeleka pepo za kupandishia, na tunateremsha kutoka mbinguni maji, kisha tukakunywesheni maji hayo. Wala si nyinyi mnayo yaweka.
Verse 23
ﮕﮖﮗﮘﮙﮚ
ﮛ
Na Sisi ndio tunao huisha na tunao fisha. Na Sisi ndio Warithi.
Verse 24
Na tunawajua walio tangulia katika nyinyi, na tunawajua walio taakhari.
Verse 25
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye atakaye wakusanya. Hakika Yeye ni Mwenye hikima na Mjuzi.
Verse 26
Na tulimuumba mtu kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yaliyo tiwa sura.
Verse 27
Na majini tuliwaumba kabla kwa moto wa upepo umoto.
Verse 28
Na Mola wako Mlezi alipo waambia Malaika: Hakika Mimi nitamuumba mtu kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yaliyo tiwa sura.
Verse 29
Basi nitakapo mkamilisha na nikampulizia roho yangu, basi mumwangukie kumsujudia.
Verse 30
ﯶﯷﯸﯹ
ﯺ
Basi Malaika wote pamoja walimsujudia,
Verse 31
Isipo kuwa Iblisi. Yeye alikataa kuwa pamoja na walio sujudu.
Verse 32
(Mwenyezi Mungu) akasema: Ewe Iblisi! Una nini hata hukuwa pamoja na walio sujudu?
Verse 33
Akasema: Haiwi mimi nimsujudie mtu uliye muumba kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yenye sura.
Verse 34
ﭦﭧﭨﭩﭪ
ﭫ
(Mwenyezi Mungu) akasema: Basi toka humo, kwani hakika wewe ni maluuni!
Verse 35
ﭬﭭﭮﭯﭰﭱ
ﭲ
Na hakika juu yako ipo laana mpaka Siku ya Malipo.
Verse 36
ﭳﭴﭵﭶﭷﭸ
ﭹ
Akasema (Iblisi): Mola wangu Mlezi! Nipe muhula mpaka siku watapo fufuliwa.
Verse 37
ﭺﭻﭼﭽ
ﭾ
(Mwenyezi Mungu) akasema: Hakika wewe ni katika walio pewa muhula
Verse 38
ﭿﮀﮁﮂ
ﮃ
Mpaka siku ya wakati maalumu.
Verse 39
Akasema: Mola wangu Mlezi! Ilivyo kuwa umenitia makosani, basi nahakikisha nitawazaini hapa duniani na nitawapoteza wote,
Verse 40
ﮏﮐﮑﮒ
ﮓ
Ila waja wako walio safika.
Verse 41
ﮔﮕﮖﮗﮘ
ﮙ
Akasema: Hii Njia ya kujia kwangu Iliyo Nyooka.
Verse 42
Hakika waja wangu, wewe hutakuwa na mamlaka juu yao, isipo kuwa wale wapotofu walio kufuata.
Verse 43
ﮦﮧﮨﮩ
ﮪ
Na bila shaka Jahannamu ndipo pahali pao walipo ahidiwa wote.
Verse 44
Ina milango saba; na kwa kila mlango iko sehemu walio tengewa.
Verse 45
ﯕﯖﯗﯘﯙ
ﯚ
Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na chemchem.
Verse 46
ﯛﯜﯝ
ﯞ
(Wataambiwa:) Ingieni kwa salama na amani.
Verse 47
Na tutaondoa chuki iliyo kuwamo vifuani mwao, wawe ndugu juu ya viti vya enzi wameelekeana.
Verse 48
Humo hayatawagusa machofu, wala hawatatolewa humo.
Verse 49
Waambie waja wangu ya kwamba Mimi ndiye Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu.
Verse 50
ﯻﯼﯽﯾﯿ
ﰀ
Na kwamba adhabu yangu ndio adhabu iliyo chungu!
Verse 51
ﰁﰂﰃﰄ
ﰅ
Na uwape khabari za wageni wa Ibrahim.
Verse 52
Walipo ingia kwake na wakasema: Salama! Yeye akasema: Hakika sisi tunakuogopeni.
Verse 53
Wakasema: Usiogope. Sisi tunakubashiria kijana mwenye ujuzi.
Verse 54
Akasema: Mnanibashiria nami uzee umenishika! Basi kwa njia gani mnanibashiria?
Verse 55
Wakasema: Tunakubashiria kwa haki; basi usiwe miongoni mwa wanao kata tamaa.
Verse 56
Akasema: Na nani anaye kata tamaa na rehema ya Mola wake Mlezi ila wale walio potea?
Verse 57
ﭽﭾﭿﮀﮁ
ﮂ
Akasema: Hebu nini amri yenu, enyi wajumbe?
Verse 58
ﮃﮄﮅﮆﮇﮈ
ﮉ
Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwa kaumu ya wakosefu!
Verse 59
ﮊﮋﮌﮍﮎﮏ
ﮐ
Isipo kuwa walio mfuata Luut'i. Bila ya shaka sisi tutawaokoa hao wote.
Verse 60
ﮑﮒﮓﮔﮕﮖ
ﮗ
Ila mkewe. Tunakadiria huyo atakuwa miongoni watao bakia nyuma.
Verse 61
ﮘﮙﮚﮛﮜ
ﮝ
Basi wale wajumbe walipo fika kwa Luut'i,
Verse 62
ﮞﮟﮠﮡ
ﮢ
Alisema (Luut'i): Hakika nyinyi ni watu msio juulikana.
Verse 63
Wakasema: Bali sisi tumekuletea yale waliyo kuwa wakiyafanyia shaka.
Verse 64
ﮫﮬﮭﮮ
ﮯ
Na tumefika kwako kwa Haki, na hakika sisi tunasema kweli.
Verse 65
Basi ondoka na ahli zako usiku ungalipo, nawe ufuate nyuma yao, wala yeyote kati yenu asigeuke nyuma. Na mwende mnapo amrishwa.
Verse 66
Na tukamfunulia hukumu hiyo, ya kwamba hata wa mwisho wao hao ikifika asubuhi atakuwa kesha katiliwa mbali.
Verse 67
ﯪﯫﯬﯭ
ﯮ
Na wakaja watu wa mji ule nao furahani.
Verse 68
ﯯﯰﯱﯲﯳﯴ
ﯵ
Akasema: Hakika hawa wageni wangu, basi msinifedheheshe.
Verse 69
ﯶﯷﯸﯹ
ﯺ
Na mcheni Mwenyezi Mungu, wala msinihizi.
Verse 70
ﯻﯼﯽﯾﯿ
ﰀ
Wakasema: Sisi hatukukukataza usimkaribishe yeyote?
Verse 71
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖ
ﭗ
Akasema: Hawa binti zangu, ikiwa nyinyi ni watendaji.
Verse 72
ﭘﭙﭚﭛﭜ
ﭝ
Naapa kwa umri wako! Hakika hao walikuwa katika ulevi wao, wakihangaika ovyo.
Verse 73
ﭞﭟﭠ
ﭡ
Ukelele ukawatwaa wakipambaukiwa.
Verse 74
Na tukaigeuza nchi juu chini, na tukawanyeshea mvua ya mawe ya udongo wa Motoni.
Verse 75
ﭫﭬﭭﭮﭯ
ﭰ
Hakika katika hayo zipo ishara kwa waaguzi.
Verse 76
ﭱﭲﭳ
ﭴ
Na miji hii ipo kwenye njia inayo pitiwa.
Verse 77
ﭵﭶﭷﭸﭹ
ﭺ
Hakika katika hayo ipo ishara kwa Waumini.
Verse 78
ﭻﭼﭽﭾﭿ
ﮀ
Na hakika watu wa Kichakani walikuwa wenye kudhulumu.
Verse 79
ﮁﮂﮃﮄﮅ
ﮆ
Kwa hivyo tukawaadhibu. Na nchi mbili hizi ziko kwenye njia ilio wazi.
Verse 80
ﮇﮈﮉﮊﮋ
ﮌ
Na bila ya shaka wakaazi wa Hijr waliwakanusha Mitume.
Verse 81
ﮍﮎﮏﮐﮑ
ﮒ
Na tuliwapa ishara zetu, nao wakazipuuza.
Verse 82
ﮓﮔﮕﮖﮗﮘ
ﮙ
Nao walikuwa wakichonga majumba katika milima kwa amani.
Verse 83
ﮚﮛﮜ
ﮝ
Basi ukelele ukawatwaa asubuhi.
Verse 84
ﮞﮟﮠﮡﮢﮣ
ﮤ
Hayakuwafaa waliyo kuwa wakiyachuma.
Verse 85
Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake ila kwa ajili ya Haki. Na hakika Kiyama kitafika. Basi samehe msamaha mzuri.
Verse 86
ﯗﯘﯙﯚﯛ
ﯜ
Hakika Mola wako Mlezi ndiye Muumbaji Mjuzi.
Verse 87
Na tumekupa Aya saba zinazo somwa mara kwa mara, na Qur'ani Tukufu.
Verse 88
Usivitumbulie macho yako vitu tulivyo waneemesha makundi fulani kati yao, wala usiwahuzunikie. Na wainamishie bawa lako (la huruma) Waumini.
Verse 89
ﯵﯶﯷﯸﯹ
ﯺ
Na sema: Hakika mimi ni mwonyaji mwenye kubainisha.
Verse 90
ﯻﯼﯽﯾ
ﯿ
Kama hivyo tuliwateremshia walio gawa,
Verse 91
ﭑﭒﭓﭔ
ﭕ
Ambao wakaifanya Qur'ani vipande vipande.
Verse 92
ﭖﭗﭘ
ﭙ
Basi Naapa kwa Mola wako Mlezi! Tutawahoji wote,
Verse 93
ﭚﭛﭜ
ﭝ
Kwa waliyo kuwa wakiyatenda.
Verse 94
ﭞﭟﭠﭡﭢﭣ
ﭤ
Basi wewe yatangaze uliyo amrishwa, na jitenge na washirikina.
Verse 95
ﭥﭦﭧ
ﭨ
Hakika Sisi tunatosha kukukinga na wanao kejeli.
Verse 96
Hao wanao fanya kuwa pamoja na Mwenyezi Mungu yupo mungu mwingine. Basi, watakuja jua!
Verse 97
Na Sisi tunajua kwa hakika kuwa wewe kifua chako kinaona dhiki kwa hayo wayasemayo.
Verse 98
ﭻﭼﭽﭾﭿﮀ
ﮁ
Basi mtakase Mola wako Mlezi kwa kumhimidi, na uwe miongoni wanao msujudia.
Verse 99
ﮂﮃﮄﮅﮆ
ﮇ
Na muabudu Mola wako Mlezi mpaka ikufikie Yakini.
تقدم القراءة