Tafsiri ya Sura Kaaf kwa السواحلية kutoka Ali Muhsin Al - Swahili translation
Verse 1
ﭑﭒﭓﭔ
ﭕ
Kaaf
Qaaf. Naapa kwa Qur'ani tukufu!
Verse 2
Bali wanastaajabu kwamba amewafikia mwonyaji kutoka miongoni mwao, na wakasema makafiri: Hili ni jambo la ajabu!
Verse 3
Ati tukifa na tukawa udongo...? Kurejea huko kuko mbali!
Verse 4
Hakika Sisi tunajua kiasi cha kila kinacho punguzwa na ardhi kutokana nao. Na kwetu kipo Kitabu kinacho hifadhi yote.
Verse 5
Lakini waliikanusha Haki ilipo wajia; kwa hivyo wamo katika mambo ya mkorogo.
Verse 6
Je! Hawaangalii mbingu zilizo juu yao! Vipi tulivyo zijenga, na tukazipamba. Wala hazina nyufa.
Verse 7
Na ardhi tumeitandaza na tukaiwekea milima, na tukaiotesha mimea mizuri ya kila namna.
Verse 8
ﮙﮚﮛﮜﮝ
ﮞ
Yawe haya ni kifumbua macho na ukumbusho kwa kila mja mwenye kuelekea.
Verse 9
Na tumeteremsha kutoka mbinguni maji yaliyo barikiwa, na kwa hayo tukaotesha mabustani na nafaka za kuvunwa.
Verse 10
ﮪﮫﮬﮭﮮ
ﮯ
Na mitende mirefu yenye makole yaliyo zaa kwa wingi,
Verse 11
Ili iwe ni riziki kwa waja wangu. Na tukaifufua kwa maji nchi iliyo kuwa imekufa. Kama hivyo ndivyo utakavyo kuwa ufufuaji.
Verse 12
Kabla yao walikadhibisha kaumu ya Nuhu na wakaazi wa Rassi na Thamudi.
Verse 13
ﯤﯥﯦﯧ
ﯨ
Na A'di na Firauni na kaumu ya Lut'i.
Verse 14
Na wakaazi wa Machakani, na watu wa Tubbaa'. Wote hao waliwakanusha Mitume, kwa hivyo onyo likathibitika juu yao.
Verse 15
Kwani tulichoka kwa kuumba mara ya kwanza. Bali wao wamo katika shaka tu juu ya umbo jipya.
Verse 16
Na hakika tumemuumba mtu, nasi tunayajua yanayo mpitikia katika nafsi yake. Na Sisi tuko karibu naye kuliko mshipa wa shingoni mwake.
Verse 17
Wanapo pokea wapokeaji wawili, wanao kaa kuliani na kushotoni.
Verse 18
Hatamki neno ila karibu yake yupo mwangalizi tayari.
Verse 19
Na uchungu wa kutoka roho utamjia kwa haki. Hayo ndiyo uliyo kuwa ukiyakimbia.
Verse 20
Na litapulizwa baragumu. Hiyo ndiyo Siku ya Miadi.
Verse 21
ﮆﮇﮈﮉﮊﮋ
ﮌ
Na kila nafsi itakuja na pamoja nayo mchungaji na shahidi.
Verse 22
(Aambiwe): Kwa hakika ulikuwa umeghafilika na haya; basi leo tumekuondolea pazia lako, na kwa hivyo kuona kwako leo ni kukali.
Verse 23
ﮚﮛﮜﮝﮞﮟ
ﮠ
Na mwenzake atasema: Huyu niliye naye mimi kesha tayarishwa.
Verse 24
ﮡﮢﮣﮤﮥﮦ
ﮧ
Mtupeni katika Jahannamu kila kafiri mwenye inda,
Verse 25
ﮨﮩﮪﮫ
ﮬ
Akatazaye kheri, arukaye mipaka, mwenye kutia shaka,
Verse 26
Aliye weka mungu mwengine pamoja na Mwenyezi Mungu. Basi mtupeni katika adhabu kali.
Verse 27
Mwenzake aseme: Ee Mola wetu Mlezi! Sikumpoteza mimi, bali yeye mwenyewe alikuwa katika upotovu wa mbali.
Verse 28
(Mwenyezi Mungu) aseme: Msigombane mbele yangu. Nilikuleteeni mbele onyo langu.
Verse 29
Mbele yangu haibadilishwi kauli, wala Mimi siwadhulumu waja wangu.
Verse 30
Siku tutapo iambia Jahannamu: Je! Umejaa? Nayo itasema: Je! Kuna ziada?
Verse 31
ﰁﰂﰃﰄﰅ
ﰆ
Na Pepo italetwa karibu kwa ajili ya wachamngu, haitakuwa mbali.
Verse 32
ﰇﰈﰉﰊﰋﰌ
ﰍ
Haya ndiyo mnayo ahidiwa kwa kila mwenye kurejea kwa Mwenyezi Mungu na akajilinda.
Verse 33
Mwenye kumwogopa Mwingi wa Rehema hali kuwa hamwoni, na akaja kwa moyo ulio elekea-
Verse 34
ﰖﰗﰘﰙﰚﰛ
ﰜ
(Ataambiwa) ingieni kwa salama. Hiyo ndiyo siku ya daima dawamu.
Verse 35
ﰝﰞﰟﰠﰡﰢ
ﰣ
Humo watapata wakitakacho, na kwetu yako ya ziada.
Verse 36
Na kaumu ngapi tuliziangamiza kabla yao walio kuwa na nguvu zaidi kuliko hawa! Nao walitanga tanga katika nchi nyingi. Je! Walipata pa kukimbilia?
Verse 37
Hakika katika hayo upo ukumbusho kwa mwenye moyo au akatega sikio naye yupo anashuhudia.
Verse 38
Na bila ya shaka Sisi tumeziumba mbingu na ardhi na vilio baina yao mnamo siku sita; na wala hayakutugusa machofu.
Verse 39
Basi vumilia kwa hayo wasemayo, na mtakase kwa kumsifu Mola wako Mlezi kabla ya kuchomoza jua na kabla ya kuchwa.
Verse 40
ﮊﮋﮌﮍﮎ
ﮏ
Na katika usiku pia mtakase, na baada ya kusujudu.
Verse 41
Na sikiliza siku atapo nadi mwenye kunadi kutoka pahala karibu.
Verse 42
Siku watakapo sikia ukelele wa haki. Hiyo ndiyo siku ya kufufuka.
Verse 43
ﮡﮢﮣﮤﮥﮦ
ﮧ
Hakika Sisi tunahuisha na tunafisha, na kwetu Sisi ndio marejeo.
Verse 44
Siku itapo wapasukia ardhi mbio mbio! Mkusanyo huo kwetu ni mwepesi.
Verse 45
Sisi tunajua kabisa wayasemayo. Wala wewe si mwenye kuwatawalia kwa ujabari. Basi mkumbushe kwa Qur'ani anaye liogopa onyo.
تقدم القراءة