Tafsiri ya Sura Az-Zukhruf kwa السواحلية kutoka Ali Muhsin Al - Swahili translation
Verse 1
ﮀ
ﮁ
Az-Zukhruf
H'a Mim
Verse 2
ﮂﮃ
ﮄ
Naapa kwa Kitabu kinacho bainisha.
Verse 3
ﮅﮆﮇﮈﮉﮊ
ﮋ
Hakika Sisi tumeifanya Qur'ani kwa Kiarabu ili mfahamu.
Verse 4
Na hakika hiyo imo katika Asili ya Maandiko yalioko kwetu, ni tukufu na yenye hikima.
Verse 5
Je! Tuache kukukumbusheni kabisa kwa kuwa nyinyi ni watu mlio pita mipaka kwa ukafiri?
Verse 6
ﮝﮞﮟﮠﮡﮢ
ﮣ
Na Manabii wangapi tuliwatuma kwa watu wa zamani!
Verse 7
Na hawajii Nabii yeyote ila walikuwa wakimkejeli.
Verse 8
Na tuliwaangamiza walio kuwa na nguvu kushinda wao. Na mfano wa watu wa zamani umekwisha pita.
Verse 9
Na ukiwauliza: Nani aliye ziumba mbingu na ardhi? Bila ya shaka watasema: Kaziumba Mwenye nguvu, Mjuzi,
Verse 10
Ambaye amekufanyieni ardhi kama tandiko, na akakufanyieni ndani yake njia mpate kuongoka.
Verse 11
Na ambaye ndiye aliye teremsha kutoka mbinguni maji kwa kiasi, na kwa hayo tukaifufua nchi iliyo kufa. Na namna hivi ndivyo mtakavyo tolewa.
Verse 12
Na ambaye ndiye aliye umba katika kila kitu jike na dume, na akakufanyieni marikebu na wanyama mnao wapanda.
Verse 13
Ili mkae vizuri migongoni mwao, kisha mkumbuke neema za Mola wenu Mlezi mnapokaa sawa sawa juu yao na mseme: Ametakasika aliye mfanya huyu atutumikie, na tusingeli weza kufanya haya wenyewe.
Verse 14
ﮀﮁﮂﮃ
ﮄ
Na hakika sisi tutarudi kwa Mola wetu Mlezi.
Verse 15
Na wanamfanyia katika waja wake fungu. Kwa hakika mwanaadamu ni mtovu wa fadhila aliye dhaahiri.
Verse 16
Au amejichukulia watoto wanawake katika vile alivyo viumba, na akakuteulieni nyinyi watoto wanaume?
Verse 17
Na anapo bashiriwa mmoja wao kwa yale aliyo mpigia mfano Mwenyezi Mungu, uso wake husawijika na hujaa hasira.
Verse 18
Ati aliye lelewa katika mapambo, na katika mabishano hawezi kusema kwa bayana...?
Verse 19
Na wakawafanya Malaika, ambao ni waja wa Mwingi wa Rehema, ni wanawake! Kwani wameshuhudia kuumbwa kwao? Ushahidi wao utaandikwa na wao watahojiwa!
Verse 20
Nao husema: Angeli penda Mwingi wa Rehema tusingeli waabudu sisi. Hawana ujuzi wowote wa hayo! Hawana ila kusema uwongo tu!
Verse 21
Kwani tuliwapa Kitabu kabla ya hichi, na ikawa wao wanakishikilia hicho?
Verse 22
Bali wanasema: Hakika sisi tuliwakuta baba zetu wanashika dini makhsusi, basi na sisi tunaongoza nyayo zao.
Verse 23
Na kadhaalika hatukumtuma mwonyaji kwenye mji wowote ila watu wake walio deka kwa starehe walisema: Hakika sisi tuliwakuta baba zetu wanashika dini makhsusi, na sisi tunafuata nyayo zao.
Verse 24
Akasema (Mwonyaji): Hata nikikuleteeni yenye uwongofu bora kuliko mlio wakuta nao baba zenu? Wakasema: Sisi tunayakataa tu hayo mliyo tumwa.
Verse 25
Basi tukawalipizia. Angalia ulikuwaje mwisho wa walio kadhibisha!
Verse 26
Na pale Ibrahim alipo mwambia baba yake na kaumu yake: Hakika mimi ninajitenga mbali na hayo mnayo yaabudu,
Verse 27
ﮋﮌﮍﮎﮏ
ﮐ
Isipo kuwa yule aliye niumba, kwani Yeye ataniongoa.
Verse 28
Na akalifanya hili liwe neno lenye kubaki katika vizazi vyake ili warejee.
Verse 29
Bali tuliwastarehesha hawa na baba zao mpaka ikawafikia Haki na Mtume aliye bainisha.
Verse 30
Na ilipo wafikia Haki wakasema: Huu ni uchawi, na sisi hakika tunaukataa.
Verse 31
Na walisema: Kwa nini Qur'ani hii haikuteremshwa kwa mtu mkubwa katika miji miwili hii?
Verse 32
Kwani wao ndio wanao gawa rehema za Mola wako Mlezi? Sisi tumewagawanyia baina yao maisha yao katika uhai wa duniani, na tukawanyanyua baadhi yao juu ya wengine kwa daraja nyingi; kwa hivyo baadhi yao wanawafanya wenginewe wawatumikie. Na rehema za Mwenyezi Mungu ni bora kuliko hayo wanayo yakusanya.
Verse 33
Na lau isinge kuwa watu watakuwa kundi moja tungeli wajaalia wanao mkufuru Rahmani wana nyumba zao zina dari ya fedha, na ngazi zao pia wanazo pandia,
Verse 34
ﭑﭒﭓﭔﭕ
ﭖ
Na milango ya nyumba zao na vitanda wanavyo egemea juu yake,
Verse 35
Na mapambo. Lakini hayo si chochote ila ni starehe ya maisha ya dunia tu, na Akhera iliyoko kwa Mola wako Mlezi ni ya wenye kumchamngu.
Verse 36
Anaye yafanyia upofu maneno ya Rahmani tunamwekea Shet'ani kuwa ndiye rafiki yake.
Verse 37
Na hakika wao wanawazuilia Njia na wenyewe wanadhani kuwa wameongoka.
Verse 38
Hata atakapo tujia atasema: Laiti ungeli kuwako baina yangu na wewe kama umbali baina ya mashariki na magharibi. Rafiki mwovu mno wewe!
Verse 39
Na kwa kuwa mlidhulumu, haitakufaeni kitu leo kwamba nyinyi mnashirikiana katika adhabu.
Verse 40
Je! Unaweza kuwasikilizisha viziwi, au unaweza kuwaongoa vipofu na waliomo katika upotofu ulio wazi?
Verse 41
ﮜﮝﮞﮟﮠﮡ
ﮢ
Na hata tukikuondoa, Sisi tutalipiza kisasi chetu kwao.
Verse 42
Au tutakuonyesha tulio waahidi. Nasi bila ya shaka tuna uweza juu yao.
Verse 43
Basi wewe yashike yaliyo funuliwa kwako. Hakika wewe uko kwenye Njia Iliyo Nyooka.
Verse 44
Na hakika haya ni ukumbusho kwako na kwa kaumu yako. Na mtakuja ulizwa.
Verse 45
Na waulize Mitume wetu tulio watuma kabla yako: Je! Tulifanya miungu mingine iabudiwe badala ya Rah'mani?
Verse 46
Na bila ya shaka tulimtuma Musa kwa Ishara zetu ende kwa Firauni na waheshimiwa wake, na akasema: Hakika mimi ni Mtume wa Mola Mlezi wa walimwengu wote!
Verse 47
Lakini alipo wajia na Ishara zetu wakaingia kuzicheka.
Verse 48
Na hatukuwaonyesha Ishara yoyote ila hiyo ilikuwa kubwa zaidi kuliko nyenginewe. Na tukawakamata kwa adhabu ili warejee.
Verse 49
Na wakasema: Ewe mchawi! Tuombee kwa Mola wako Mlezi kwa ile ahadi aliyo kuahidi; hakika sisi tutakuwa wenye kuongoka.
Verse 50
Basi tulipo waondolea adhabu hiyo, mara wakaingia kuvunja ahadi.
Verse 51
Na Firauni alitangaza kwa watu wake, akisema: Enyi watu wangu! Kwani mimi sinao huu ufalme wa Misri, na hii mito inapita chini yangu? Je! Hamwoni?
Verse 52
Au mimi si bora kuliko huyu aliye mnyonge, wala hawezi kusema waziwazi?
Verse 53
Basi mbona hakuvikwa vikuku vya dhahabu, au hawakuja Malaika pamoja naye wakamwandama?
Verse 54
Basi aliwachezea watu wake, na wakamt'ii. Kwa hakika hao walikuwa watu wapotovu.
Verse 55
ﮨﮩﮪﮫﮬﮭ
ﮮ
Walipo tukasirisha tuliwapatiliza tukawazamisha wote!
Verse 56
ﮯﮰﮱﯓ
ﯔ
Kisha tukawafanya kuwa watangulizi na mfano kwa wa baadaye.
Verse 57
Na alipo pigiwa mfano Mwana wa Mariamu, watu wako waliupiga ukelele.
Verse 58
Wakasema: Miungu yetu kwani si bora kuliko huyu? Hawakukupigia mfano huo ila kwa ubishi tu. Bali hao ni watu wagomvi!
Verse 59
Hakuwa yeye (Isa) ila ni Mtumwa tuliye mneemesha na tukamfanya ni mfano kwa Wana wa Israili.
Verse 60
Na tungeli penda tungeli wafanyia miongoni mwenu Malaika katika ardhi wakifuatana.
Verse 61
Na kwa hakika yeye ni alama ya Saa ya Kiyama. Basi usiitilie shaka, na nifuateni. Hii ndiyo Njia Iliyo Nyooka.
Verse 62
Wala asikuzuilieni Shet'ani. Hakika yeye ni adui yenu wa dhaahiri.
Verse 63
Na alipo kuja Isa na dalili zilizo wazi, alisema: Nimekujieni na hikima, na ili nikuelezeni baadhi ya yale mliyo khitalifiana. Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na mnit'ii mimi.
Verse 64
Kwa hakika Mwenyezi Mungu ni Mola wangu Mlezi, na ni Mola wenu Mlezi. Basi Muabuduni Yeye tu. Hii ndiyo Njia Iliyo Nyooka.
Verse 65
Lakini makundi kwa makundi yao yalikhitalifiana wao kwa wao. Ole wao walio dhulumu kwa adhabu ya siku chungu.
Verse 66
Je! Nini wanangojea ila Saa iwajie kwa ghafla na wala wao hawatambui?
Verse 67
Siku hiyo marafiki watakuwa ni maadui, wao kwa wao, isipo kuwa wachamngu.
Verse 68
Enyi waja wangu! Hamtakuwa na khofu siku hiyo, wala hamtahuzunika.
Verse 69
ﮭﮮﮯﮰﮱ
ﯓ
Ambao waliziamini Ishara zangu na walikuwa Waislamu.
Verse 70
ﯔﯕﯖﯗﯘ
ﯙ
Ingieni Peponi, nyinyi na wake zenu; mtafurahishwa humo.
Verse 71
Watakuwa wanapitishiwa sahani za dhahabu na vikombe; na vitakuwamo ambavyo nafsi zinavipenda na macho yanavifurahia, na nyinyi mtakaa humo milele.
Verse 72
Na hiyo ni Pepo mliyo rithishwa kwa hayo mliyo kuwa mkiyafanya.
Verse 73
ﯴﯵﯶﯷﯸﯹ
ﯺ
Mnayo humo matunda mengi mtakayo yala.
Verse 74
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖ
ﭗ
Kwa hakika wakosefu watakaa katika adhabu ya Jahannamu.
Verse 75
ﭘﭙﭚﭛﭜﭝ
ﭞ
Hawatapumzishwa nayo na humo watakata tamaa.
Verse 76
ﭟﭠﭡﭢﭣﭤ
ﭥ
Wala Sisi hatukuwadhulumu, bali wao ndio walio kuwa madhaalimu.
Verse 77
Nao watapiga kelele waseme: Ewe Malik! Na atufishe Mola wako Mlezi! Naye aseme: Hakika nyinyi mtakaa humo humo!
Verse 78
Kwa yakini tulikuleteeni Haki, lakini wengi katika nyinyi mlikuwa mnaichukia Haki.
Verse 79
ﭸﭹﭺﭻﭼ
ﭽ
Au waliweza kupitisha amri yao? Bali ni Sisi ndio tunao pitisha.
Verse 80
Au wanadhani kwamba hatusikii siri zao na minong'ono yao? Wapi! Na wajumbe wetu wapo karibu nao, wanayaandika.
Verse 81
Sema: Ingeli kuwa Rahmani ana mwana, basi mimi ningeli kuwa wa kwanza kumuabudu.
Verse 82
Ametakasika Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, Mola Mlezi wa A'rshi, na hayo wanayo msifia.
Verse 83
Basi waache wapige porojo wakicheza mpaka wakutwe na hiyo siku yao waliyo ahidiwa.
Verse 84
Na Yeye ndiye Mungu mbinguni, na ndiye Mungu katika ardhi. Naye ndiye Mwenye hikima, Mwenye ujuzi.
Verse 85
Na ametukuka Mwenye ufalme wa mbingu na ardhi na viliomo ndani yake. Na uko kwake ujuzi wa Saa ya Kiyama, na kwake Yeye mtarudishwa.
Verse 86
Wala hao mnao waomba badala yake Yeye hawana uweza wa kumwombea mtu, isipo kuwa anaye shuhudia kwa haki, na wao wanajua.
Verse 87
Na ukiwauliza ni nani aliye waumba? Bila ya shaka watasema: Mwenyezi Mungu! Basi ni wapi wanako geuziwa?
Verse 88
Na usemi wake (Mtume) ni: Ewe Mola wangu Mlezi! Hakika hawa ni watu wasio amini.
Verse 89
Basi wasamehe, na uwambie maneno ya salama. Watakuja jua.
تقدم القراءة