Tafsiri ya Sura As-Saffat kwa السواحلية kutoka Ali Muhsin Al - Swahili translation
Verse 1
ﭑﭒ
ﭓ
As-Saffat
Naapa kwa wanao jipanga kwa safu.
Verse 2
ﭔﭕ
ﭖ
Na kwa wenye kukataza mabaya.
Verse 3
ﭗﭘ
ﭙ
Na kwa wenye kusoma Ukumbusho.
Verse 4
ﭚﭛﭜ
ﭝ
Hakika Mungu wenu bila ya shaka ni Mmoja.
Verse 5
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na yaliyomo kati yao, na ni Mola Mlezi wa mashariki zote.
Verse 6
ﭦﭧﭨﭩﭪﭫ
ﭬ
Hakika Sisi tumeipamba mbingu ya karibu kwa pambo la nyota.
Verse 7
ﭭﭮﭯﭰﭱ
ﭲ
Na kulinda na kila shet'ani a'si.
Verse 8
Wasiweze kuwasikiliza viumbe watukufu. Na wanafukuzwa huko kila upande.
Verse 9
ﭽﭾﭿﮀﮁ
ﮂ
Wakifurushwa. Na wanayo adhabu ya kudumu.
Verse 10
Isipo kuwa anaye nyakua kitu kidogo, na mara humfwatia kimondo kinacho ng'ara.
Verse 11
Hebu waulize: Je! Wao ni wenye umbo gumu zaidi au hao wengine tulio waumba. Hakika Sisi tuliwaumba wao kwa udongo unao nata.
Verse 12
ﮙﮚﮛ
ﮜ
Bali unastaajabu, na wao wanafanya maskhara.
Verse 13
ﮝﮞﮟﮠ
ﮡ
Na wanapo kumbushwa hawakumbuki.
Verse 14
ﮢﮣﮤﮥ
ﮦ
Na wanapo ona Ishara, wanafanya maskhara.
Verse 15
ﮧﮨﮩﮪﮫﮬ
ﮭ
Na husema: Haya si chochote ila ni uchawi tu ulio dhaahiri.
Verse 16
Ati tukisha kufa na tukawa udongo na mifupa ndio kweli tutafufuliwa?
Verse 17
ﯗﯘ
ﯙ
Hata baba zetu wa zamani?
Verse 18
ﯚﯛﯜﯝ
ﯞ
Sema: Naam! Hali nanyi ni madhalili.
Verse 19
Huko utapigwa ukelele mmoja tu! Na hapo ndio wataona!
Verse 20
ﯧﯨﯩﯪﯫ
ﯬ
Watasema: Ole wetu! Hii ndiyo Siku ya Malipo.
Verse 21
Hii ndiyo Siku ya Hukumu mliyo kuwa mkiikadhibisha.
Verse 22
Wakusanyeni walio dhulumu, na wake zao, na hao walio kuwa wakiwaabudu -
Verse 23
Badala ya Mwenyezi Mungu. Waongozeni njia ya Jahannamu!
Verse 24
ﰆﰇﰈﰉ
ﰊ
Na wasimamisheni. Hakika hao watasailiwa:
Verse 25
ﭑﭒﭓﭔ
ﭕ
Mna nini? Mbona hamsaidiani?
Verse 26
ﭖﭗﭘﭙ
ﭚ
Bali hii leo, watasalimu amri.
Verse 27
ﭛﭜﭝﭞﭟ
ﭠ
Watakabiliana wao kwa wao kuulizana.
Verse 28
ﭡﭢﭣﭤﭥﭦ
ﭧ
Watasema: Kwa hakika nyinyi mlikuwa mkitujia upande wa kulia.
Verse 29
ﭨﭩﭪﭫﭬ
ﭭ
Watasema (wakubwa): Bali nyinyi wenyewe hamkuwa Waumini.
Verse 30
Sisi hatukuwa na mamlaka juu yenu, bali nyinyi wenyewe mlikuwa wapotovu.
Verse 31
Basi hukumu ya Mola wetu Mlezi imekwisha tuthibitikia. Hakika bila ya shaka tutaonja tu adhabu.
Verse 32
ﮂﮃﮄﮅ
ﮆ
Tulikupotezeni kwa sababu sisi wenyewe tulikuwa wapotovu.
Verse 33
ﮇﮈﮉﮊﮋ
ﮌ
Basi wao kwa hakika siku hiyo watashirikiana katika adhabu pamoja.
Verse 34
ﮍﮎﮏﮐ
ﮑ
Hivyo ndivyo tutakavyo wafanyia wakosefu.
Verse 35
Wao walipo kuwa wakiambiwa La ilaha illa 'Llahu Hapana mungu ila Mwenyezi Mungu tu, wakijivuna.
Verse 36
ﮝﮞﮟﮠﮡﮢ
ﮣ
Na wakisema: Hivyo sisi tuiache miungu yetu kwa ajili ya huyu mtunga mashairi mwendawazimu?
Verse 37
ﮤﮥﮦﮧﮨ
ﮩ
Bali huyu amekuja kwa Haki, na amewasadikisha Mitume.
Verse 38
ﮪﮫﮬﮭ
ﮮ
Hakika nyinyi bila ya shaka mtaionja adhabu chungu.
Verse 39
ﮯﮰﮱﯓﯔﯕ
ﯖ
Wala hamlipwi ila hayo mliyo kuwa mkiyafanya.
Verse 40
ﯗﯘﯙﯚ
ﯛ
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa.
Verse 41
ﯜﯝﯞﯟ
ﯠ
Hao ndio watakao pata riziki maalumu,
Verse 42
ﯡﯢﯣ
ﯤ
Matunda, nao watahishimiwa.
Verse 43
ﯥﯦﯧ
ﯨ
Katika Bustani za neema.
Verse 44
ﯩﯪﯫ
ﯬ
Wako juu ya viti wamekabiliana.
Verse 45
ﯭﯮﯯﯰﯱ
ﯲ
Wanazungushiwa kikombe chenye kinywaji cha chemchem
Verse 46
ﯳﯴﯵ
ﯶ
Kinywaji cheupe, kitamu kwa wanywao.
Verse 47
Hakina madhara, wala hakiwaleweshi.
Verse 48
ﯿﰀﰁﰂ
ﰃ
Na watakuwa nao wanawake wenye macho ya staha mazuri.
Verse 49
ﰄﰅﰆ
ﰇ
Hao wanawake kama mayai yaliyo hifadhika.
Verse 50
ﰈﰉﰊﰋﰌ
ﰍ
Waingie kuulizana wenyewe kwa wenyewe.
Verse 51
Aseme msemaji mmoja miongoni mwao: Hakika mimi nalikuwa na rafiki
Verse 52
ﭑﭒﭓﭔ
ﭕ
Aliye kuwa akinambia: Hivyo wewe ni katika wanao sadiki
Verse 53
Ati tukisha kufa tukawa udongo na mafupa, ndio tutalipwa na kuhisabiwa?
Verse 54
ﭞﭟﭠﭡ
ﭢ
Atasema: Je! Nyie mnawaona?
Verse 55
ﭣﭤﭥﭦﭧ
ﭨ
Basi atachungulia amwone katikati ya Jahannamu.
Verse 56
ﭩﭪﭫﭬﭭ
ﭮ
Atasema: Wallahi! Ulikaribia kunipoteza.
Verse 57
ﭯﭰﭱﭲﭳﭴ
ﭵ
Na lau kuwa si neema ya Mola wangu Mlezi bila ya shaka ningeli kuwa miongoni mwa walio hudhurishwa.
Verse 58
ﭶﭷﭸ
ﭹ
Je! Sisi hatutakufa,
Verse 59
ﭺﭻﭼﭽﭾﭿ
ﮀ
Isipo kuwa kifo chetu cha kwanza? Wala sisi hatutaadhibiwa.
Verse 60
ﮁﮂﮃﮄﮅ
ﮆ
Hakika huku bila ya shaka ndiko kufuzu kukubwa.
Verse 61
ﮇﮈﮉﮊ
ﮋ
Kwa mfano wa haya nawatende watendao.
Verse 62
ﮌﮍﮎﮏﮐﮑ
ﮒ
Je! Kukaribishwa hivi si ndio bora, au mti wa Zaqqum?
Verse 63
ﮓﮔﮕﮖ
ﮗ
Hakika Sisi tumeufanya huo kuwa ni mateso kwa walio dhulumu.
Verse 64
ﮘﮙﮚﮛﮜﮝ
ﮞ
Hakika huo ni mti unao toka katikati ya Jahannamu.
Verse 65
ﮟﮠﮡﮢ
ﮣ
Mashada ya matunda yake kama kwamba vichwa vya mashet'ani.
Verse 66
ﮤﮥﮦﮧﮨﮩ
ﮪ
Basi hakika bila ya shaka hao watayala hayo, na wajaze matumbo.
Verse 67
Kisha juu yake wanyweshwe mchanganyo wa maji yamoto yaliyo chemka.
Verse 68
ﯔﯕﯖﯗﯘ
ﯙ
Kisha hakika marejeo yao bila ya shaka yatakuwa kwenye Jahannamu.
Verse 69
ﯚﯛﯜﯝ
ﯞ
Hakika waliwakuta baba zao wamepotea.
Verse 70
ﯟﯠﯡﯢ
ﯣ
Na wao wakafanya haraka kufuata nyayo zao.
Verse 71
ﯤﯥﯦﯧﯨ
ﯩ
Na bila ya shaka walikwisha potea kabla yao wengi wa watu wa zamani.
Verse 72
ﯪﯫﯬﯭ
ﯮ
Na Sisi hakika tuliwapelekea waonyaji.
Verse 73
ﯯﯰﯱﯲﯳ
ﯴ
Basi hebu angalia ulikuwaje mwisho wa walio onywa.
Verse 74
ﯵﯶﯷﯸ
ﯹ
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa.
Verse 75
ﯺﯻﯼﯽﯾ
ﯿ
Na hakika Nuhu alitwita, na Sisi ni bora wa waitikiaji.
Verse 76
ﰀﰁﰂﰃﰄ
ﰅ
Na tulimwokoa yeye na ahali zake kutokana na msiba mkubwa.
Verse 77
ﭑﭒﭓﭔ
ﭕ
Na tuliwajaalia dhuriya zake ndio wenye kubakia.
Verse 78
ﭖﭗﭘﭙ
ﭚ
Na tukamwachia (sifa njema) kwa walio kuja baadaye.
Verse 79
ﭛﭜﭝﭞﭟ
ﭠ
Iwe salama kwa Nuhu ulimwenguni kote!
Verse 80
ﭡﭢﭣﭤ
ﭥ
Kwa hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema.
Verse 81
ﭦﭧﭨﭩ
ﭪ
Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.
Verse 82
ﭫﭬﭭ
ﭮ
Kisha tukawazamisha wale wengine.
Verse 83
ﭯﭰﭱﭲﭳ
ﭴ
Na hakika Ibrahim alikuwa katika kundi lake,
Verse 84
ﭵﭶﭷﭸﭹ
ﭺ
Alipo mjia Mola wake Mlezi kwa moyo mzima.
Verse 85
ﭻﭼﭽﭾﭿﮀ
ﮁ
Alimwambia baba yake na watu wake: Mnaabudu nini?
Verse 86
ﮂﮃﮄﮅﮆ
ﮇ
Kwa kuzua tu mnataka miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu?
Verse 87
ﮈﮉﮊﮋ
ﮌ
Mnamdhania nini Mola Mlezi wa walimwengu wote?
Verse 88
ﮍﮎﮏﮐ
ﮑ
Kisha akapiga jicho kutazama nyota.
Verse 89
ﮒﮓﮔ
ﮕ
Akasema: Hakika mimi ni mgonjwa!
Verse 90
ﮖﮗﮘ
ﮙ
Nao wakamwacha, wakampa kisogo.
Verse 91
ﮚﮛﮜﮝﮞﮟ
ﮠ
Basi akaiendea miungu yao kwa siri, akaiambia: Mbona hamli?
Verse 92
ﮡﮢﮣﮤ
ﮥ
Mna nini hata hamsemi?
Verse 93
ﮦﮧﮨﮩ
ﮪ
Kisha akaigeukia kuipiga kwa mkono wa kulia.
Verse 94
ﮫﮬﮭ
ﮮ
Basi wakamjia upesi upesi.
Verse 95
ﮯﮰﮱﯓ
ﯔ
Akasema: Hivyo mnaviabudu vitu mnavyo vichonga wenyewe?
Verse 96
ﯕﯖﯗﯘ
ﯙ
Na hali Mwenyezi Mungu ndiye aliye kuumbeni nyinyi na hivyo mnavyo vifanya!
Verse 97
Wakasema: Mjengeeni jengo, na kisha mtupeni motoni humo!
Verse 98
ﯢﯣﯤﯥﯦ
ﯧ
Basi walitaka kumfanyia vitimbi, lakini tukawafanya wao ndio wa chini.
Verse 99
ﯨﯩﯪﯫﯬﯭ
ﯮ
Na akasema: Hakika mimi nahama, nakwenda kwa Mola wangu Mlezi; Yeye ataniongoa.
Verse 100
ﯯﯰﯱﯲﯳ
ﯴ
Ewe Mola wangu Mlezi! Nitunukie aliye miongoni mwa watenda mema.
Verse 101
ﯵﯶﯷ
ﯸ
Basi tukambashiria mwana aliye mpole.
Verse 102
Basi alipo fika makamo ya kwenda na kurudi pamoja naye, alimwambia: Ewe mwanangu! Hakika mimi nimeona usingizini kuwa ninakuchinja. Basi angalia wewe, waonaje? Akasema: Ewe baba yangu! Tenda unavyo amrishwa, utanikuta mimi, Inshallah, katika wanao subiri.
Verse 103
ﭑﭒﭓﭔ
ﭕ
Basi wote wawili walipo jisalimisha, na akamlaza juu ya kipaji.
Verse 104
ﭖﭗﭘ
ﭙ
Tulimwita: Ewe Ibrahim!
Verse 105
Umekwisha itimiliza ndoto. Hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao tenda mema.
Verse 106
ﭣﭤﭥﭦﭧ
ﭨ
Hakika haya ni majaribio yaliyo dhaahiri.
Verse 107
ﭩﭪﭫ
ﭬ
Basi tukamtolea fidia kwa dhabihu mtukufu.
Verse 108
ﭭﭮﭯﭰ
ﭱ
Na tukamwachia (sifa njema) kwa watu walio kuja baadaye.
Verse 109
ﭲﭳﭴ
ﭵ
Iwe salama kwa Ibrahim!
Verse 110
ﭶﭷﭸ
ﭹ
Hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema.
Verse 111
ﭺﭻﭼﭽ
ﭾ
Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.
Verse 112
ﭿﮀﮁﮂﮃ
ﮄ
Na tukambashiria kuzaliwa Is-haqa, naye ni Nabii miongoni mwa watu wema.
Verse 113
Na tukambarikia yeye na Is-haqa. Na miongoni mwa dhuriya zao walitokea wema na wenye kudhulumu nafsi zao waziwazi.
Verse 114
ﮑﮒﮓﮔﮕ
ﮖ
Na kwa hakika tuliwafanyia hisani Musa na Haruni.
Verse 115
ﮗﮘﮙﮚﮛ
ﮜ
Na tukawaokoa wao na watu wao kutokana na dhiki kubwa.
Verse 116
ﮝﮞﮟﮠ
ﮡ
Na tukawanusuru; na wakawa wao ndio wenye kushinda.
Verse 117
ﮢﮣﮤ
ﮥ
Na tukawapa wawili hao Kitabu kinacho bainisha.
Verse 118
ﮦﮧﮨ
ﮩ
Na tukawaongoa kwenye Njia Iliyo Nyooka.
Verse 119
ﮪﮫﮬﮭ
ﮮ
Na tukawaachia (sifa njema) katika watu walio kuja baadaye.
Verse 120
ﮯﮰﮱﯓ
ﯔ
Iwe salama kwa Musa na Haruni!
Verse 121
ﯕﯖﯗﯘ
ﯙ
Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio wema.
Verse 122
ﯚﯛﯜﯝ
ﯞ
Hakika wawili hao ni katika waja wetu walio amini.
Verse 123
ﯟﯠﯡﯢ
ﯣ
Na hakika Ilyas bila ya shaka alikuwa miongoni mwa Mitume.
Verse 124
ﯤﯥﯦﯧﯨ
ﯩ
Alipo waambia watu wake: Hamwogopi?
Verse 125
ﯪﯫﯬﯭﯮ
ﯯ
Mnamwomba Baa'li na mnamwacha Mbora wa waumbaji,
Verse 126
ﯰﯱﯲﯳﯴ
ﯵ
Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa zamani?
Verse 127
ﭑﭒﭓ
ﭔ
Wakamkadhibisha. Basi kwa hakika watahudhurishwa;
Verse 128
ﭕﭖﭗﭘ
ﭙ
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa.
Verse 129
ﭚﭛﭜﭝ
ﭞ
Na tumemwachia (sifa nzuri) kwa walio kuja baadaye.
Verse 130
ﭟﭠﭡﭢ
ﭣ
Iwe salama kwa Ilyas.
Verse 131
ﭤﭥﭦﭧ
ﭨ
Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio wema.
Verse 132
ﭩﭪﭫﭬ
ﭭ
Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.
Verse 133
ﭮﭯﭰﭱ
ﭲ
Na hakika Lut'i bila ya shaka ni miongoni mwa Mitume.
Verse 134
ﭳﭴﭵﭶ
ﭷ
Tulipo mwokoa yeye na ahali zake wote,
Verse 135
ﭸﭹﭺﭻ
ﭼ
Isipo kuwa mwanamke mkongwe katika wale walio bakia nyuma.
Verse 136
ﭽﭾﭿ
ﮀ
Kisha tukawaangamiza wale wengineo.
Verse 137
ﮁﮂﮃﮄ
ﮅ
Na hakika nyinyi mnawapitia wakati wa asubuhi,
Verse 138
ﮆﮇﮈﮉ
ﮊ
Na usiku. Basi je! Hamyatii akilini?
Verse 139
ﮋﮌﮍﮎ
ﮏ
Na hakika Yunus alikuwa miongoni mwa Mitume.
Verse 140
ﮐﮑﮒﮓﮔ
ﮕ
Alipo kimbia katika jahazi lilio sheheni.
Verse 141
ﮖﮗﮘﮙ
ﮚ
Akaingia katika kupigiwa kura, na akawa katika walio shindwa.
Verse 142
ﮛﮜﮝﮞ
ﮟ
Samaki akammeza hali ya kuwa ni mwenye kulaumiwa.
Verse 143
ﮠﮡﮢﮣﮤ
ﮥ
Na ingeli kuwa hakuwa katika wanao mtakasa Mwenyezi Mungu,
Verse 144
ﮦﮧﮨﮩﮪﮫ
ﮬ
Bila ya shaka angeli kaa ndani yake mpaka siku ya kufufuliwa.
Verse 145
ﮭﮮﮯﮰﮱ
ﯓ
Lakini tulimtupa ufukweni patupu, hali yu mgonjwa.
Verse 146
ﯔﯕﯖﯗﯘ
ﯙ
Na tukauotesha juu yake mmea wa kabila ya mung'unye.
Verse 147
ﯚﯛﯜﯝﯞﯟ
ﯠ
Na tulimtuma kwa watu laki moja au zaidi.
Verse 148
ﯡﯢﯣﯤ
ﯥ
Basi wakaamini, na tukawastarehesha kwa muda.
Verse 149
ﯦﯧﯨﯩﯪ
ﯫ
Basi waulize: Ati Mola wako Mlezi ndiye mwenye watoto wa kike, na wao wanao watoto wa kiume?
Verse 150
ﯬﯭﯮﯯﯰﯱ
ﯲ
Au tumewaumba Malaika kuwa ni wanawake, na wao wakashuhudia?
Verse 151
ﯳﯴﯵﯶﯷ
ﯸ
Ati ni kwa uzushi wao ndio wanasema:
Verse 152
ﯹﯺﯻﯼ
ﯽ
Mwenyezi Mungu amezaa! Ama hakika bila ya shaka hao ni waongo!
Verse 153
ﯾﯿﰀﰁ
ﰂ
Ati amekhiari watoto wa kike kuliko wanaume?
Verse 154
ﭑﭒﭓﭔ
ﭕ
Mna nini? Mnahukumu vipi nyinyi?
Verse 155
ﭖﭗ
ﭘ
Hamkumbuki?
Verse 156
ﭙﭚﭛﭜ
ﭝ
Au mnayo hoja iliyo wazi?
Verse 157
ﭞﭟﭠﭡﭢ
ﭣ
Basi leteni Kitabu chenu kama mnasema kweli.
Verse 158
Na wameweka makhusiano ya nasaba baina yake na majini; na majini wamekwisha jua bila ya shaka kuwa wao watahudhurishwa.
Verse 159
ﭰﭱﭲﭳ
ﭴ
Subhana 'Llah Ametakasika Mwenyezi Mungu na hayo wanayo msingizia.
Verse 160
ﭵﭶﭷﭸ
ﭹ
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa.
Verse 161
ﭺﭻﭼ
ﭽ
Basi hakika nyinyi na mnao waabudu
Verse 162
ﭾﭿﮀﮁ
ﮂ
Hamwezi kuwapoteza
Verse 163
ﮃﮄﮅﮆﮇ
ﮈ
Isipo kuwa yule atakaye ingia Motoni.
Verse 164
ﮉﮊﮋﮌﮍﮎ
ﮏ
Na hapana katika sisi ila anapo mahali pake maalumu.
Verse 165
ﮐﮑﮒ
ﮓ
Na hakika bila ya shaka sisi ndio wajipangao safu.
Verse 166
ﮔﮕﮖ
ﮗ
Na hakika sisi ndio wenye kusabihi kutakasa.
Verse 167
ﮘﮙﮚ
ﮛ
Na walikuwapo walio kuwa wakisema:
Verse 168
ﮜﮝﮞﮟﮠﮡ
ﮢ
Tungeli kuwa na Ukumbusho kama wa watu wa zamani,
Verse 169
ﮣﮤﮥﮦ
ﮧ
Bila ya shaka tungeli kuwa ni waja wa Mwenyezi Mungu wenye ikhlasi.
Verse 170
ﮨﮩﮪﮫﮬ
ﮭ
Lakini waliukataa. Basi watakuja jua.
Verse 171
ﮮﮯﮰﮱﯓ
ﯔ
Na bila ya shaka neno letu lilikwisha tangulia kwa waja wetu walio tumwa.
Verse 172
ﯕﯖﯗ
ﯘ
Ya kuwa wao bila ya shaka ndio watakao nusuriwa.
Verse 173
ﯙﯚﯛﯜ
ﯝ
Na kwamba jeshi letu ndilo litakalo shinda.
Verse 174
ﯞﯟﯠﯡ
ﯢ
Basi waachilie mbali kwa muda.
Verse 175
ﯣﯤﯥ
ﯦ
Na watazame, nao wataona.
Verse 176
ﯧﯨ
ﯩ
Je! Wanaihimiza adhabu yetu?
Verse 177
ﯪﯫﯬﯭﯮﯯ
ﯰ
Basi itakapo shuka uwanjani kwao, itakuwa asubuhi mbaya kwa walio onywa.
Verse 178
ﯱﯲﯳﯴ
ﯵ
Na waache kwa muda.
Verse 179
ﯶﯷﯸ
ﯹ
Na tazama, na wao wataona.
Verse 180
ﯺﯻﯼﯽﯾﯿ
ﰀ
Subhana Rabbi'l'Izzat Ametakasika Mola Mlezi Mwenye enzi na yale wanayo mzulia.
Verse 181
ﰁﰂﰃ
ﰄ
Na Salamu juu ya Mitume.
Verse 182
ﰅﰆﰇﰈ
ﰉ
Na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.
تقدم القراءة