Tafsiri ya Sura Al-Muminu kwa السواحلية kutoka Ali Muhsin Al - Swahili translation
Verse 1
ﭑﭒﭓ
ﭔ
Al-Muminu
HAKIKA wamefanikiwa Waumini,
Verse 2
ﭕﭖﭗﭘﭙ
ﭚ
Ambao ni wanyenyekevu katika Sala zao,
Verse 3
ﭛﭜﭝﭞﭟ
ﭠ
Na ambao hujiepusha na mambo ya upuuzi,
Verse 4
ﭡﭢﭣﭤ
ﭥ
Na ambao wanatoa Zaka,
Verse 5
ﭦﭧﭨﭩ
ﭪ
Na ambao wanazilinda tupu zao,
Verse 6
Isipo kuwa kwa wake zao au kwa iliyo wamiliki mikono yao ya kulia. Kwani hao si wenye kulaumiwa.
Verse 7
Lakini anaye taka kinyume cha haya, basi hao ndio warukao mipaka.
Verse 8
ﭾﭿﮀﮁﮂ
ﮃ
Na ambao wanazitimiza amana zao na ahadi zao,
Verse 9
ﮄﮅﮆﮇﮈ
ﮉ
Na ambao Sala zao wanazihifadhi -
Verse 10
ﮊﮋﮌ
ﮍ
Hao ndio warithi,
Verse 11
ﮎﮏﮐﮑﮒﮓ
ﮔ
Ambao watairithi Pepo ya Firdausi, wadumu humo.
Verse 12
Na kwa yakini tumemuumba mtu kutokana na asli ya udongo.
Verse 13
ﮝﮞﮟﮠﮡﮢ
ﮣ
Kisha tukamjaalia awe tone ya mbegu ya uzazi katika kalio madhubuti.
Verse 14
Kisha tukaiumba tone kuwa damu iliyo ganda, na tukaiumba damu kuwa pande la nyama, kisha tukaliumba pande la nyama kuwa mifupa, na mifupa tukaivika nyama. Kisha tukamfanya kiumbe mwengine. Basi ametukuka Mwenyezi Mungu Mbora wa waumbaji.
Verse 15
ﯜﯝﯞﯟﯠ
ﯡ
Kisha hakika nyinyi baada ya hayo mtakufa.
Verse 16
ﯢﯣﯤﯥﯦ
ﯧ
Kisha hakika nyinyi Siku ya Kiyama mtafufuliwa.
Verse 17
Na kwa yakini tumeziumba juu yenu njia saba. Nasi hatukuwa wenye kughafilika na viumbe.
Verse 18
Na tumeteremsha kutoka mbinguni maji kwa kiasi na tukayatuliza katika ardhi. Na hakika Sisi tunaweza kuyaondoa.
Verse 19
Kwa maji hayo tukakufanyieni bustani za mitende na mizabibu, mnapata humo matunda mengi, na katika hayo mnakula;
Verse 20
Na mti utokao katika mlima wa Sinai, unatoa mafuta na kuwa kitoweo kwa walao.
Verse 21
Na hakika mnayo mazingatio makubwa katika nyama hoa - tunakunywesheni katika vile viliomo matumboni mwao, na nyinyi mnapata katika hao manufaa mengi, na pia mnawala.
Verse 22
ﮉﮊﮋﮌ
ﮍ
Na juu yao na juu ya marikebu mnabebwa.
Verse 23
Na hakika tulimtuma Nuhu kwa watu wake, akasema: Enyi watu wangu! Muabuduni Mwenyezi Mungu. Nyinyi hamna mungu asiye kuwa Yeye. Basi je! Hamwogopi?
Verse 24
Walisema wale wakuu walio kufuru katika watu wake: Huyu si chochote ila ni mtu tu kama nyinyi. Anataka kujipa ubora juu yenu. Na lau kuwa Mwenyezi Mungu amependa basi yakini angeli teremsha Malaika. Hatukusikia haya kwa baba zetu wa zamani.
Verse 25
Huyu si lolote ila ni mtu mwenye wazimu. Basi mngojeeni tu kwa muda.
Verse 26
ﯧﯨﯩﯪﯫ
ﯬ
Akasema (Nuhu): Mola wangu Mlezi! Ninusuru kwa kuwa wamenikanusha.
Verse 27
Tukampa wahyi: Unda jahazi mbele ya macho yetu na uwongozi wetu! Basi itapo fika amri yetu na ikafurika tanuri, hapo waingize ndani yake wa kila namna dume na jike, na ahali zako, isipo kuwa yule ambaye katika wao juu yake imekwisha tangulia kauli. Wala usinitajie hao walio dhulumu. Kwani hao bila ya shaka watazamishwa.
Verse 28
Basi utakapo tulia wewe na walio pamoja nawe humo marikebuni, sema: Alhamdulillahi Sifa zote njema ni za Mwenyezi Mungu, aliye tuokoa na watu madhaalimu!
Verse 29
Na sema: Mola wangu Mlezi! Niteremshe mteremsho wenye baraka, na Wewe ni Mbora wa wateremshaji.
Verse 30
Hakika katika hayo yapo mazingatio. Na kwa yakini Sisi ni wenye kuwafanyia mtihani.
Verse 31
ﭲﭳﭴﭵﭶﭷ
ﭸ
Kisha baada yao tukaanzisha kizazi kingine.
Verse 32
Tukawapelekea Mtume miongoni mwao, kuwaambia: Muabuduni Mwenyezi Mungu! Hamna mungu asiye kuwa Yeye. Jee, hamwogopi?
Verse 33
Na wakubwa katika watu wake walio kufuru na wakakanusha mkutano wa Akhera, na tukawadekeza kwa starehe katika maisha ya dunia, walisema: Huyu si chochote ila ni binaadamu kama nyinyi; anakula mlacho, na anakunywa mnywacho.
Verse 34
Na nyinyi mkimt'ii mtu kama nyinyi basi hakika mtakuwa khasarani.
Verse 35
Hivyo anakuahidini ati ya kwamba mtakapo kufa na mkawa udongo na mifupa kuwa mtatolewa?
Verse 36
ﯖﯗﯘﯙﯚ
ﯛ
Hayawi! Hayawi hayo mnayo ahidiwa.
Verse 37
Hapana ila uhai wetu wa duniani tu, tunakufa na kuishi basi. Wala sisi hatutafufuliwa.
Verse 38
Huyu si lolote ila ni mtu anaye mzulia Mwenyezi Mungu uwongo, wala sisi sio wa kumuamini.
Verse 39
ﯴﯵﯶﯷﯸ
ﯹ
Akasema: Mola wangu Mlezi! Ninusuru kwa sababu wananikanusha.
Verse 40
ﯺﯻﯼﯽﯾ
ﯿ
(Mwenyezi Mungu) akasema: Baada ya muda mchache watakuwa wenye kujuta.
Verse 41
Basi ukawanyakua ukelele kwa haki, na tukawafanya kama takataka zinazo elea juu ya maji. Ikapotelea mbali kaumu ya madhaalimu!
Verse 42
ﰊﰋﰌﰍﰎﰏ
ﰐ
Kisha tukaleta baada yao vizazi vingine.
Verse 43
Hapana umma uwezao kutanguliza ajali yake wala kuikawiza.
Verse 44
Kisha tukawatuma Mitume wetu, mmoja baada ya mmoja. Kila umma alipo wafikia Mtume wao walimkanusha. Tukawafuatanisha hawa baada ya hawa, na tukawafanya ni hadithi za kusimuliwa. Wakapotelea mbali watu wasio amini.
Verse 45
Kisha tukamtuma Musa na nduguye, Haaruni, pamoja na ishara zetu na hoja zilizo wazi.
Verse 46
Kumwendea Firauni na wakuu wake. Lakini walijivuna, nao walikuwa watu majeuri.
Verse 47
Wakasema: Je, tuwaamini wanaadamu wawili hawa kama sisi, na ambao watu wao ni watumwa wetu?
Verse 48
ﮉﮊﮋﮌ
ﮍ
Basi wakawakanusha, na wakawa miongoni mwa walio angamizwa.
Verse 49
ﮎﮏﮐﮑﮒﮓ
ﮔ
Na hakika tulimpa Musa Kitabu ili wapate kuongoka.
Verse 50
Na tukamfanya mwana wa Mariamu na mama yake kuwa ni Ishara, na tukawapa makimbilio kwenda mahali palipo inuka penye utulivu na chemchem za maji.
Verse 51
Enyi Mitume! Kuleni vyakula vizuri na tendeni mema. Hakika Mimi ni Mjuzi wa mnayo yatenda.
Verse 52
Na kwa yakini huu Umma wenu ni Umma mmoja, na Mimi ni Mola wenu Mlezi, basi nicheni Mimi.
Verse 53
Lakini walikatiana jambo lao mapande mbali mbali. Kila kundi likifurahia kwa waliyo nayo.
Verse 54
ﯣﯤﯥﯦﯧ
ﯨ
Basi waache katika ghafla yao kwa muda.
Verse 55
Je! Wanadhani ya kuwa kwa vile tunavyo wapa mali na watoto
Verse 56
Ndio tunawahimizia kheri? Lakini wenyewe hawatambui.
Verse 57
Kwa hakika hao ambao kwa kumwogopa Mola wao Mlezi wananyenyekea,
Verse 58
ﰂﰃﰄﰅﰆ
ﰇ
Na wale ambao Ishara za Mola wao Mlezi wanaziamini,
Verse 59
ﰈﰉﰊﰋﰌ
ﰍ
Na wale ambao Mola wao Mlezi hawamshirikishi,
Verse 60
Na wale ambao wanatoa walicho pewa, na hali nyoyo zao zinagopa kwa kuwa watarejea kwa Mola wao Mlezi,
Verse 61
Basi wote hao ndio wanao kimbilia katika mambo ya kheri, na ndio watakao tangulia kuyafikia.
Verse 62
Na hatuilazimishi nafsi ila kwa kadri ya uwezo wake. Na tunacho kitabu kisemacho kweli. Nao hawatadhulumiwa.
Verse 63
Lakini nyoyo zao zimeghafilika na hayo, na wanavyo vitendo vinginevyo wanavyo vifanya.
Verse 64
Hata tutakapo watia katika adhabu wale walio dekezwa kwa starehe kati yao, hapo ndipo watapo yayatika.
Verse 65
Msiyayatike leo! Hakika nyinyi hamtanusurika nasi.
Verse 66
Hakika zilikuwa Aya zangu mkisomewa, nanyi mkirudi nyuma juu ya visigino vyenu,
Verse 67
ﮝﮞﮟﮠ
ﮡ
Na huku mkitakabari na usiku mkiizungumza (Qur'ani) kwa dharau.
Verse 68
Je, hawakuifikiri kauli, au yamewajia yasiyo wafikia baba zao wa zamani?
Verse 69
Au hawakumjua Mtume wao, ndio maana wanamkataa?
Verse 70
Au wanasema: Ana wazimu? Bali amewajia kwa Haki, na wengi wao wanaichukia Haki.
Verse 71
Na lau kuwa Haki ingeli fuata matamanio yao, basi zingeli haribika mbingu na ardhi na waliomo ndani. Bali tumewaletea ukumbusho wao, nao wanajitenga mbali na ukumbusho wao.
Verse 72
Au unawaomba ujira? Lakini ujira wa Mola wako Mlezi ni bora, na Yeye ndiye Mbora wa wanao ruzuku.
Verse 73
ﯿﰀﰁﰂﰃ
ﰄ
Na kwa yakini wewe unawaita kwenye Njia Iliyo Nyooka.
Verse 74
Na hakika wale wasio iamini Akhera wanajitenga na Njia hiyo.
Verse 75
Na lau tungeli warehemu na tukawaondolea shida waliyo nayo bila ya shaka wangeli endelea katika upotofu wao vile vile, wakitangatanga.
Verse 76
Na hakika tuliwatia adhabu kali; lakini hawakuelekea kwa Mola wao Mlezi wala hawakunyenyekea.
Verse 77
Mpaka tulipo wafungulia mlango wa adhabu kali, hapo ndipo wakawa wenye kukata tamaa.
Verse 78
Na Yeye ndiye aliye kuumbieni kusikia na kuona na nyoyo za kufahamu. Ni kuchache mno kushukuru kwenu.
Verse 79
Na Yeye ndiye aliye kuenezeni katika ardhi, na kwake Yeye mtakusanywa.
Verse 80
Na Yeye ndiye anaye huisha na kufisha, na yake Yeye mabadiliko ya usiku na mchana. Basi je! Hamfahamu?
Verse 81
ﮔﮕﮖﮗﮘﮙ
ﮚ
Bali wanasema kama walivyo sema watu wa kwanza.
Verse 82
Walisema: Je! Tukisha kufa tukawa udongo na mifupa ndio tutafufuliwa?
Verse 83
Tuliahidiwa haya sisi na baba zetu zamani. Hayakuwa haya ila ni visa vya uwongo vya watu wa zamani.
Verse 84
Sema: Ni ya nani ardhi na viliomo ndani yake, kama nyinyi mnajua?
Verse 85
ﯛﯜﯝﯞﯟﯠ
ﯡ
Watasema: Ni vya Mwenyezi Mungu! Sema: Basi, je, hamkumbuki?
Verse 86
Sema: Ni nani Mola Mlezi wa mbingu saba na Mola Mlezi wa A'rshi Kuu?
Verse 87
ﯫﯬﯭﯮﯯﯰ
ﯱ
Watasema: Ni vya Mwenyezi Mungu. Sema: Basi je, hamwogopi?
Verse 88
Sema: Ni nani mkononi mwake umo Ufalme wa kila kitu, naye ndiye anaye linda, wala hakilindwi asicho taka, kama mnajua?
Verse 89
ﰁﰂﰃﰄﰅﰆ
ﰇ
Watasema: (Ufalme huo) ni wa Mwenyezi Mungu. Sema: Basi vipi mnadanganyika?
Verse 90
ﭑﭒﭓﭔﭕ
ﭖ
Bali tumewaletea Haki, na kwa yakini hao ni waongo.
Verse 91
Mwenyezi Mungu hana mwana yeyote, wala hanaye mungu mwengine. Inge kuwa hivyo basi kila mungu angeli chukua alivyo umba, na baadhi yao wangeli washinda wengine. Mwenyezi Mungu ameepukana na sifa wanazo msifu.
Verse 92
ﭲﭳﭴﭵﭶﭷ
ﭸ
Mjuzi wa siri na dhaahiri, na ametukuka juu ya hayo wanayo mshirikisha nayo.
Verse 93
ﭹﭺﭻﭼﭽﭾ
ﭿ
Sema: Mola wangu Mlezi! Ukinionyesha adhabu waliyo ahidiwa,
Verse 94
ﮀﮁﮂﮃﮄﮅ
ﮆ
Mola wangu Mlezi! Usinijaalie katika watu madhaalimu hao.
Verse 95
Na hakika Sisi ni waweza wa kukuonyeshsa tuliyo waahidi.
Verse 96
Kinga maovu kwa kutenda yaliyo mema zaidi. Sisi tunajua wayasemayo.
Verse 97
Na sema: Mola wangu Mlezi! Najikinga kwako na wasiwasi wa mashet'ani.
Verse 98
ﮢﮣﮤﮥﮦ
ﮧ
Na najikinga kwako, Mola wangu Mlezi, wasinikaribie.
Verse 99
Mpaka yanapo mfikia mmoja wao mauti, husema: Mola wangu Mlezi! Nirudishe.
Verse 100
Ili nitende mema sasa badala ya yale niliyo yaacha. Wapi! Hii ni kauli aisemayo yeye tu. Na nyuma yao kipo kizuizi mpaka siku watapo fufuliwa.
Verse 101
Basi litapo pulizwa baragumu hapo hautakuwapo ujamaa baina yao siku hiyo, wala hawataulizana.
Verse 102
ﯱﯲﯳﯴﯵﯶ
ﯷ
Ama wale ambao mizani zao zitakuwa nzito, hao ndio wenye kufanikiwa.
Verse 103
Na wale ambao mizani zao zitakuwa nyepesi, hao ndio walio zitia khasarani nafsi zao, na katika Jahannamu watadumu.
Verse 104
ﰃﰄﰅﰆﰇﰈ
ﰉ
Moto utababua nyuso zao, nao watakuwa na nyuso zilizo kunjana.
Verse 105
Je! Hazikuwa Aya zangu mkisomewa, na nyinyi mkizikanusha?
Verse 106
Mola wetu Mlezi! Tulizidiwa na uovu wetu na tukawa watu tulio potea.
Verse 107
Mola wetu Mlezi! Tutoe humu Motoni. Na tufanyapo tena basi kweli sisi ni wenye kudhulumu.
Verse 108
ﭫﭬﭭﭮﭯ
ﭰ
Atasema Mwenyezi Mungu: Tokomeeni humo, wala msinisemeze.
Verse 109
Bila ya shaka lilikuwapo kundi katika waja wangu likisema: Mola wetu Mlezi! Tumeamini; basi tusamehe na uturehemu, nawe ndiwe Mbora wa wanao rehemu.
Verse 110
Lakini nyinyi mliwakejeli hata wakakusahaulisheni kunikumbuka, na mlikuwa mkiwacheka.
Verse 111
Hakika Mimi leo nimewalipa kwa vile walivyo subiri. Bila ya shaka hao ndio wenye kufuzu.
Verse 112
Atasema: Mlikaa muda gani katika ardhi kwa hisabu ya miaka?
Verse 113
Watasema: Tulikaa siku moja au sehemu ya siku. Basi waulize wanao weka hisabu.
Verse 114
Atasema: Nyinyi hamkukaa huko duniani ila kidogo, laiti ingeli kuwa mnajua.
Verse 115
Je! Mlidhani ya kwamba tulikuumbeni bure na ya kwamba nyinyi kwetu hamtarudishwa?
Verse 116
Ametukuka Mwenyezi Mungu, Mfalme wa Haki, hapana mungu ila Yeye, Mola Mlezi wa A'rshi Tukufu.
Verse 117
Na anaye muomba - pamoja na Mwenyezi Mungu - mungu mwenginewe hana ushahidi wa hili; basi bila ya shaka hisabu yake iko kwa Mola wake Mlezi. Kwa hakika makafiri hawafanikiwi.
Verse 118
Nawe sema: Mola wangu Mlezi! Samehe na urehemu nawe ni Mbora wa wanao rehemu.
تقدم القراءة