Tafsiri ya Sura Al-Balad kwa السواحلية kutoka Ali Muhsin Al - Swahili translation
Verse 1
ﭽﭾﭿﮀ
ﮁ
Al-Balad
Naapa kwa Mji huu!
Verse 2
ﮂﮃﮄﮅ
ﮆ
Nawe unaukaa Mji huu.
Verse 3
ﮇﮈﮉ
ﮊ
Na naapa kwa mzazi na alicho kizaa.
Verse 4
ﮋﮌﮍﮎﮏ
ﮐ
Hakika tumemuumba mtu katika taabu.
Verse 5
ﮑﮒﮓﮔﮕﮖ
ﮗ
Ati anadhani hapana yeyote ataye muweza?
Verse 6
ﮘﮙﮚﮛ
ﮜ
Anasema: Nimeteketeza chungu ya mali.
Verse 7
ﮝﮞﮟﮠﮡ
ﮢ
Ati anadhani ya kuwa hapana yeyote anaye mwona?
Verse 8
ﮣﮤﮥﮦ
ﮧ
Kwani hatukumpa macho mawili?
Verse 9
ﮨﮩ
ﮪ
Na ulimi, na midomo miwili?
Verse 10
ﮫﮬ
ﮭ
Na tukambainishia zote njia mbili?
Verse 11
ﮮﮯﮰ
ﮱ
Lakini hakujitoma kwenye njia ya vikwazo vya milimani.
Verse 12
ﯓﯔﯕﯖ
ﯗ
Na nini kitakujuvya ni nini njia ya vikwazo vya milimani?
Verse 13
ﯘﯙ
ﯚ
Kumkomboa mtumwa;
Verse 14
ﯛﯜﯝﯞﯟﯠ
ﯡ
Au kumlisha siku ya njaa
Verse 15
ﯢﯣﯤ
ﯥ
Yatima aliye jamaa,
Verse 16
ﯦﯧﯨﯩ
ﯪ
Au masikini aliye vumbini.
Verse 17
Tena awe miongoni mwa walio amini na wakausiana kusubiri na wakausiana kuhurumiana.
Verse 18
ﯵﯶﯷ
ﯸ
Hao ndio watu wa kheri wa kuliani.
Verse 19
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖ
ﭗ
Lakini walio zikataa Ishara zetu, hao ndio watu wa shari wa kushotoni.
Verse 20
ﭘﭙﭚ
ﭛ
Juu yao utakuwa Moto ulio fungiwa kila upande.
تقدم القراءة