Tafsiri ya Sura Al-Kiyama kwa السواحلية kutoka Ali Muhsin Al - Swahili translation
Verse 1
ﮊﮋﮌﮍ
ﮎ
Al-Kiyama
Ninaapa kwa Siku ya Kiyama!
Verse 2
ﮏﮐﮑﮒ
ﮓ
Na ninaapa kwa nafsi inayo jilaumu!
Verse 3
ﮔﮕﮖﮗﮘ
ﮙ
Anadhani mtu kuwa Sisi hatutaikusanya mifupa yake?
Verse 4
ﮚﮛﮜﮝﮞﮟ
ﮠ
Kwani! Sisi tunaweza hata kuziweka sawa sawa ncha za vidole vyake!
Verse 5
ﮡﮢﮣﮤﮥ
ﮦ
Lakini mtu anataka tu kuendelea na maasi kwa siku zilioko mbele yake.
Verse 6
ﮧﮨﮩﮪ
ﮫ
Anauliza: Lini itakuwa hiyo Siku ya Kiyama?
Verse 7
ﮬﮭﮮ
ﮯ
Basi jicho litapo dawaa,
Verse 8
ﮰﮱ
ﯓ
Na mwezi utapo patwa,
Verse 9
ﯔﯕﯖ
ﯗ
Na likakusanywa jua na mwezi,
Verse 10
ﯘﯙﯚﯛﯜ
ﯝ
Siku hiyo mtu atasema: Yako wapi makimbilio?
Verse 11
ﯞﯟﯠ
ﯡ
La! Hapana pa kukimbilia!
Verse 12
ﯢﯣﯤﯥ
ﯦ
Siku hiyo pa kutua ni kwa Mola wako Mlezi tu.
Verse 13
ﯧﯨﯩﯪﯫﯬ
ﯭ
Siku hiyo ataambiwa aliyo yatanguliza na aliyo yaakhirisha.
Verse 14
ﯮﯯﯰﯱﯲ
ﯳ
Bali mtu ni hoja juu ya nafsi yake.
Verse 15
ﯴﯵﯶ
ﯷ
Na ingawa atatoa chungu ya udhuru.
Verse 16
ﯸﯹﯺﯻﯼﯽ
ﯾ
Usiutikisie huu wahyi ulimi wako kwa kuufanyia haraka.
Verse 17
ﯿﰀﰁﰂ
ﰃ
Hakika ni juu yetu kuukusanya na kuusomesha.
Verse 18
ﰄﰅﰆﰇ
ﰈ
Tunapo usoma, basi nawe fuatiliza kusoma kwake.
Verse 19
ﰉﰊﰋﰌ
ﰍ
Kisha ni juu yetu kuubainisha.
Verse 20
ﭑﭒﭓﭔ
ﭕ
Hasha! Bali nyinyi mnapenda maisha ya duniani,
Verse 21
ﭖﭗ
ﭘ
Na mnaacha maisha ya Akhera.
Verse 22
ﭙﭚﭛ
ﭜ
Zipo nyuso siku hiyo zitao ng'ara,
Verse 23
ﭝﭞﭟ
ﭠ
Zinamwangallia Mola wao Mlezi.
Verse 24
ﭡﭢﭣ
ﭤ
Na zipo nyuso siku hiyo zitakao kunjana.
Verse 25
ﭥﭦﭧﭨﭩ
ﭪ
Zitajua ya kuwa zitafikiwa na livunjalo uti wa mgongo.
Verse 26
ﭫﭬﭭﭮ
ﭯ
La, hasha! (Roho) itakapo fikia kwenye mafupa ya koo,
Verse 27
ﭰﭱﭲﭳ
ﭴ
Na pakasemwa: Nani wa kumganga?
Verse 28
ﭵﭶﭷ
ﭸ
Na mwenyewe akajua kwa hakika kuwa huko ndiko kufariki;
Verse 29
ﭹﭺﭻ
ﭼ
Na utapo ambatishwa muundi kwa muundi,
Verse 30
ﭽﭾﭿﮀ
ﮁ
Siku hiyo ndiyo kuchungwa kupelekwa kwa Mola wako Mlezi!
Verse 31
ﮂﮃﮄﮅ
ﮆ
Kwa sababu hakusadiki, wala hakusali.
Verse 32
ﮇﮈﮉ
ﮊ
Bali alikanusha, na akageuka.
Verse 33
ﮋﮌﮍﮎﮏ
ﮐ
Kisha akenda kwa ahali zake kwa matao.
Verse 34
ﮑﮒﮓ
ﮔ
Ole wako, ole wako!
Verse 35
ﮕﮖﮗﮘ
ﮙ
Kisha Ole wako, ole wako!
Verse 36
ﮚﮛﮜﮝﮞ
ﮟ
Ati anadhani binaadamu kuwa ataachwa bure?
Verse 37
ﮠﮡﮢﮣﮤﮥ
ﮦ
Kwani hakuwa yeye tone ya manii lilio shushwa?
Verse 38
ﮧﮨﮩﮪﮫ
ﮬ
Kisha akawa kidonge cha damu, tena Mwenyezi Mungu akamuumba na akamtengeneza vilivyo.
Verse 39
ﮭﮮﮯﮰﮱ
ﯓ
Kisha akamfanya namna mbili, mwanamume na mwanamke.
Verse 40
Je! Huyo hakuwa ni Muweza wa kufufua wafu?
تقدم القراءة