Tafsiri ya Sura Al-Kiyama kwa السواحلية kutoka الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس
Verse 1
ﮊﮋﮌﮍ
ﮎ
Anaapa Mwenyezi Mungu kwa Siku ya Hesabu na Malipo,
Verse 2
ﮏﮐﮑﮒ
ﮓ
na Anaapa kwa nafsi yenye kuamini na kuchamungu, inayomlaumu mwenyewe kwa kuacha matendo ya utiifu na kufanya matendo yenye kuangamiza, kwamba watu watafufuliwa.
Verse 3
ﮔﮕﮖﮗﮘ
ﮙ
Je anadhanihuyu binadamu kafiri kuwa sisi hatutaweza kuikusanya mifupa yake baada ya kuwa mbalimbali.?
Verse 4
ﮚﮛﮜﮝﮞﮟ
ﮠ
Ndio! Tutaikusanya na tunaweza kufanya vidole vyake au ncha za vidole vyake- baada ya kuvikusanya na kuzioanisha- viwe kwenye umbo la sawasawa, kama vilivyokuwa kabla ya kufa.
Verse 5
ﮡﮢﮣﮤﮥ
ﮦ
Bali binadamu anakanusha kufufuliwa, anataka asalie kwenye kufanya ubaya kwa siku za mbeleni za maisha yake.
Verse 6
ﮧﮨﮩﮪ
ﮫ
Kafiri huyu huwa akiuliza, akiliona jambo la kusimama Kiyama kuwa liko mbali, «Ni lini Siku ya Kiyama?’
Verse 7
ﮬﮭﮮ
ﮯ
Basi macho yatakapoduwaa na yakashituka kwa kutishika na kile yalichokiona cha vituko vya Siku ya Kiyama,
Verse 8
ﮰﮱ
ﯓ
na ukafutika mwangaza wa mwezi,
Verse 9
ﯔﯕﯖ
ﯗ
na vikakusanywa jua na mwezi katika kukosa mwangaza, kikawa kila mojawapo ya hivyo viwili hakina mwangaza,
Verse 10
ﯘﯙﯚﯛﯜ
ﯝ
wakati huo binadamu atasema, «Pa kukimbilia ni wapi kuiepuka adhabu?»
Verse 11
ﯞﯟﯠ
ﯡ
Mambo sivyo kama unavyotamani yawe, ewe binadamu, ya kutaka kukimbia. Huna mahali pa kukimbilia wala pa kupata uokozinfsi yake.
Verse 12
ﯢﯣﯤﯥ
ﯦ
Kwa Mwenyezi Mungu Peke Yake ndio mwisho wa viumbe Siku ya Kiyama na ndipo mahali pao pa kutulia, na hapo Amlipe kila mtu kwa kile alichostahiki.
Verse 13
ﯧﯨﯩﯪﯫﯬ
ﯭ
Atapashwa habari binadamu Siku hiyo kwa matendo yake yote, mema na mabaya, aliyoyatanguliza miongoni mwa hayo katika maisha yake na aliyoyachelewesha.
Verse 14
ﯮﯯﯰﯱﯲ
ﯳ
Bali binadamu ni hoja iliyo wazi juu ya nafsi yake, yenye kumfuata kwa alichokitenda na alichokiacha,
Verse 15
ﯴﯵﯶ
ﯷ
hata kama atakuja na kila udhuru wa kuelezea sababu ya uhalifu wake, hilo halitamfaa.
Verse 16
ﯸﯹﯺﯻﯼﯽ
ﯾ
Usitikise, ewe Nabii, ulimi wako kwa Qur’ani wakati wahyi unapoteremka ili ufanye haraka kuihifadhi kwa kuogopa isikuponyoke.
Verse 17
ﯿﰀﰁﰂ
ﰃ
Kwani ni juu yetu sisi kuikusanya kwenye kifua chako kisha uisome kwa ulimi wako wakati utakapo. Mjumbe wetu Jibrili akikusomea,
Verse 18
ﰄﰅﰆﰇ
ﰈ
basi kisikilize kisomo chake na umpulikize. Kisha isome kama alivyokusomea,
Verse 19
ﰉﰊﰋﰌ
ﰍ
kisha ni juu yetu kukuelezea kilichokutatiza kukifahamu katika maana yake na hukumu zake.
Verse 20
ﭑﭒﭓﭔ
ﭕ
Mambo sivyo kama mlivyodai, enyi mkusanyiko wa washirikina, kuwa hakuna kufufuliwa wala kulipwa.
Verse 21
ﭖﭗ
ﭘ
Bali nyinyi ni watu mnaopenda dunia na pambo lake na mnaacha Akhera na starehe zake.
Verse 22
ﭙﭚﭛ
ﭜ
Nyuso za watu wema Siku ya Kiyama zitakuwa ni zenye kung’ara, nzuri na zenye furaha,
Verse 23
ﭝﭞﭟ
ﭠ
zitamuona Mola Aliyeziumba na Anayezimiliki, na zitastarehe kwa hilo.
Verse 24
ﭡﭢﭣ
ﭤ
Nyuso za watu wabaya Silku ya Kiyama zitakuwa ni zenye kukunjana na kusinyaa,
Verse 25
ﭥﭦﭧﭨﭩ
ﭪ
zinatazamia kushukiwa na msiba mkubwa wenye kuvunja.
Verse 26
ﭫﭬﭭﭮ
ﭯ
Ni kweli! Pindi roho itakapofika sehemu za juu za kifua,
Verse 27
ﭰﭱﭲﭳ
ﭴ
na wakasema baadhi ya waliohudhuria kuwaambia wengine, «Je kuna mtu wa kumzungua na kumpoza kutokana na hali hii aliyonayo?»
Verse 28
ﭵﭶﭷ
ﭸ
Na yule ambaye yuko katika hali ya kufa akajua kwamba lile lililomshukia ni kuaga dunia, kwa kuwa anawaona Malaika wa mauti.
Verse 29
ﭹﭺﭻ
ﭼ
Na ikashikana shida ya mwisho wa duniani na shida ya mwanzo wa Akhera. Kwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka.
Verse 30
ﭽﭾﭿﮀ
ﮁ
Watu watapelekwa Siku ya Kiyama: ima Peponi au Motoni.
Verse 31
ﮂﮃﮄﮅ
ﮆ
Hakuwa kafiri ni mwenye kumuamini Mtume na Qur’ani, wala hakuwa ni mwenye kumtekelezea Mwenyezi Mungu Aliyetukuka Swala za faradhi.
Verse 32
ﮇﮈﮉ
ﮊ
Lakini aliikanusha Qur’ani na akaipa mgongo Imani,
Verse 33
ﮋﮌﮍﮎﮏ
ﮐ
kisha akaenda kwa watu wake akijiona hali ya kujigamba katika kutembea kwake. Basi maangamivu
Verse 34
ﮑﮒﮓ
ﮔ
ni yako baada ya maangamivu!
Verse 35
ﮕﮖﮗﮘ
ﮙ
Kisha maangamivu ni yako baada ya maangamivu!
Verse 36
ﮚﮛﮜﮝﮞ
ﮟ
Je anadhani huyu binadamu anayekanusha kufufuliwa kuwa ataachwa bure: haamrishwi wala hakatazwi, hahesabiwi wala hateswi?
Verse 37
ﮠﮡﮢﮣﮤﮥ
ﮦ
Kwani hakuwa binadamu huyu ni tone la manii dhaifu linalotokana na maji matwevu yanayomwagwa na kumiminwa kwenye kizazi,
Verse 38
ﮧﮨﮩﮪﮫ
ﮬ
kisha yakawa ni kipande cha damu iliyo kavu. Mwenyezi Mungu Akaliumba kwa uweza Wake na Akazilinganisha sura zake katika umbo la mwili lililo zuri kabisa?
Verse 39
ﮭﮮﮯﮰﮱ
ﯓ
Akafanya kutokana na binadamu huyu jinsi mbili: ya kiume na ya kike. Je kwani hakuwa Mola huyo Muumba wa vitu hivyo ni Muweza wa kuwarudisha viumbe wakiwa hai baada ya kutoweka kwao.
Verse 40
Ndio! Anaweza. Yeye, kutakasika na sifa za upungufu ni Kwake, kwa hakika ni Muweza wa hilo.
تقدم القراءة