سورة الليل

الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس

Tafsiri ya Sura Al-Lail kwa السواحلية kutoka الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس

الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس

Verse 1
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa usiku unapoifinika ardhi na vilivyoko juu yake kwa giza lake.
Verse 2
Na kwa mchana unapofunuka mwangaza wake kutoka kwenye giza la usiku.
Verse 4
Kuwa vitendo vyenu vinatofautiana: kuna wenye kufanyia dunia na wenye kufanyia Akhera.
Verse 5
Ama mwenye kutoa kwenye mali yake, akamcha Mwenyezi Mungu katika huko kutoa,
Verse 6
akaamini «Lā Ilāha Illā Allāh» na yanayotakiwa na Imani hiyo na akaamini malipo yanayofungamana nayo,
Verse 7
Tutamuongoza na kumuafikia njia za kheri na wema na kumsahilishia mambo yake.
Verse 8
Na ama mwenye kuyafanyia ubakhili mali yake, asiwe na haja ya malipo ya Mola wake,
Verse 9
akakanusha neno la «Lā Ilāha Illā Allāh» na yanayotakiwa na neno hilo na akakanusha malipo yanayofungamana nalo,
Verse 12
Ni juu Yetu, kwa fadhila Zetu na busara Yetu, kueleza njia ya uongofu yenye kufikisha kwa Mwenyezi Mungu na ya upotevu.
Verse 13
Na Sisi Tuna mamlaka ya maisha ya Akhera na maisha ya ulimwenguni.
Verse 14
Ndipo nikawaonya , enyi watu, na kuwatisha moto wenye kuwaka, nao ni moto wa Jahanamu.
Verse 15
Hataingia Moto huo isipokuwa aliyekuwa mbaya sana. Mwenye kumkanusha Nabii Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie,
Verse 16
na akakataa kumwamini na kumtii Mwenyezi Mungu na Mtume wake.
Verse 17
Na ataepushwa nao mchaji Mwenyezi Mungu sana.
Lakini anatoa kwa kutaka uso wa Mola wake na radhi zake. Basi Mwenyezi Mungu atampa,
Verse 21
huko Peponi, malipo ya kumridhisha.
تقدم القراءة