Tafsiri ya Sura Al-Lail kwa السواحلية kutoka الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس
Verse 1
ﮡﮢﮣ
ﮤ
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa usiku unapoifinika ardhi na vilivyoko juu yake kwa giza lake.
Verse 2
ﮥﮦﮧ
ﮨ
Na kwa mchana unapofunuka mwangaza wake kutoka kwenye giza la usiku.
Verse 3
ﮩﮪﮫﮬ
ﮭ
Na kwa kuumba mbea mbili: ya kiume na ya kike,
Verse 4
ﮮﮯﮰ
ﮱ
Kuwa vitendo vyenu vinatofautiana: kuna wenye kufanyia dunia na wenye kufanyia Akhera.
Verse 5
ﯓﯔﯕﯖ
ﯗ
Ama mwenye kutoa kwenye mali yake, akamcha Mwenyezi Mungu katika huko kutoa,
Verse 6
ﯘﯙ
ﯚ
akaamini «Lā Ilāha Illā Allāh» na yanayotakiwa na Imani hiyo na akaamini malipo yanayofungamana nayo,
Verse 7
ﯛﯜ
ﯝ
Tutamuongoza na kumuafikia njia za kheri na wema na kumsahilishia mambo yake.
Verse 8
ﯞﯟﯠﯡ
ﯢ
Na ama mwenye kuyafanyia ubakhili mali yake, asiwe na haja ya malipo ya Mola wake,
Verse 9
ﯣﯤ
ﯥ
akakanusha neno la «Lā Ilāha Illā Allāh» na yanayotakiwa na neno hilo na akakanusha malipo yanayofungamana nalo,
Verse 10
ﭑﭒ
ﭓ
Tutamnyoshea njia za mateso.
Verse 11
ﭔﭕﭖﭗﭘﭙ
ﭚ
Wala hayatamfaa yeye mali yake aliyoyafanyia ubakhili atakapotumbukia Motoni.
Verse 12
ﭛﭜﭝ
ﭞ
Ni juu Yetu, kwa fadhila Zetu na busara Yetu, kueleza njia ya uongofu yenye kufikisha kwa Mwenyezi Mungu na ya upotevu.
Verse 13
ﭟﭠﭡﭢ
ﭣ
Na Sisi Tuna mamlaka ya maisha ya Akhera na maisha ya ulimwenguni.
Verse 14
ﭤﭥﭦ
ﭧ
Ndipo nikawaonya , enyi watu, na kuwatisha moto wenye kuwaka, nao ni moto wa Jahanamu.
Verse 15
ﭨﭩﭪﭫ
ﭬ
Hataingia Moto huo isipokuwa aliyekuwa mbaya sana. Mwenye kumkanusha Nabii Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie,
Verse 16
ﭭﭮﭯ
ﭰ
na akakataa kumwamini na kumtii Mwenyezi Mungu na Mtume wake.
Verse 17
ﭱﭲ
ﭳ
Na ataepushwa nao mchaji Mwenyezi Mungu sana.
Verse 18
ﭴﭵﭶﭷ
ﭸ
Ambaye hutoa mali yake kwa kutaka nyongeza za kheri
Verse 19
ﭹﭺﭻﭼﭽﭾ
ﭿ
kutoa Kwake si kwa kulipa zema alizofanyiwa na mtu.
Verse 20
ﮀﮁﮂﮃﮄ
ﮅ
Lakini anatoa kwa kutaka uso wa Mola wake na radhi zake. Basi Mwenyezi Mungu atampa,
Verse 21
ﮆﮇ
ﮈ
huko Peponi, malipo ya kumridhisha.
تقدم القراءة