Tafsiri ya Sura As-Shams kwa السواحلية kutoka الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس
Verse 1
ﭜﭝ
ﭞ
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa jua na mchana wake na mwangaza wake wa asubuhi.
Verse 2
ﭟﭠﭡ
ﭢ
Na kwa mwezi unapolifuata wakati wa kucha na kutwa.
Verse 3
ﭣﭤﭥ
ﭦ
Na kwa mchana unapoliondoa giza na kulifunua.
Verse 4
ﭧﭨﭩ
ﭪ
Na kwa usiku unapoifinika ardhi ikawa giza.
Verse 5
ﭫﭬﭭ
ﭮ
Na kwa mbingu na kujengeka kwake kiimara.
Verse 6
ﭯﭰﭱ
ﭲ
Na kwa ardhi na kutandikika kwake.
Verse 7
ﭳﭴﭵ
ﭶ
Na kwa kila nafsi na namna Mwenyezi Mungu alivyoikamilisha umbo lake ili itekeleze kazi iliyoumbiwa nayo.
Verse 8
ﭷﭸﭹ
ﭺ
Akaibainishia njia ya shari na njia ya kheri.
Verse 9
ﭻﭼﭽﭾ
ﭿ
Amefaulu mwenye kuisafisha na kuikuza kwa kheri.
Verse 10
ﮀﮁﮂﮃ
ﮄ
Na ameingia kwenye hasara mwenye kuitia nafsi yake kwenye maasia.
Verse 11
ﮅﮆﮇ
ﮈ
Kabila la Thamūd lilimkanusha Nabii wake kwa kuvama kwenye uasi.
Verse 12
ﮉﮊﮋ
ﮌ
Pindi walipotoka wabaya zaidi wa kabila hilo kumchinja Ngamia. Mtume wa Mwenyezi Mungu’ Ṣāliḥ, amani imshukie,
Verse 13
akawaambia: «Tahadharini kumgusa kwa ubaya ngamia ambaye ni miujiza ilioletwa na Mwenyezi Mungu kwenu inayoonyesha ukweli wa Nabii wenu, na msizuie kinywaji chake. Yeye ana siku yake ya kunywa na nyinyi mna siku yenu maalumu ya kunywa.» Hilo likawa zito kwao.
Verse 14
Wakamkanusha na kulipuza onyo lake wakamchinja.Mola wao Akawafinika kwa adhabu, akaisawazisha juu yao na hakuna aliyeweza kuponyoka.
Verse 15
ﮝﮞﮟ
ﮠ
Wala Haogopi, Mwenye uwezo uliotukuka, athari ya adhabu kali Aliywateremshia.
تقدم القراءة