Tafsiri ya Sura Al-Mutaffifin kwa السواحلية kutoka الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس
Verse 1
ﯖﯗ
ﯘ
Adhabu kali ni ya wale wanaopunja vipimo vya vibaba na mezani.
Verse 2
ﯙﯚﯛﯜﯝﯞ
ﯟ
Ambao wakinunua kwa watu cha kupimwa kwa vibaba au kwa mizani hujikamilishia wao wenyewe.
Verse 3
ﯠﯡﯢﯣﯤ
ﯥ
Na wakiwauzia watu kinachouzwa kwa vibaba au mizani wanapunguza vipimo.
Verse 4
ﯦﯧﯨﯩﯪ
ﯫ
Basi itakuwaje hali ya yule anayeiba na kupunja katika vipimo vyote hivyo, au yule anayeiba katika vipimo hivyo na huku awapunja watu vitu vyao? Hakika huyo yuwastahiki mateso zaidi kuliko wapunguzaji wa vipimo vya vibaba na mizani. Kwani hawaamini wale wapunjaji ya kwamba Mwenyezi Mungu Mtukufu ni Mwenye kuwafufua na kuwahesabu juu ya vitendo vyao.
Verse 5
ﭑﭒ
ﭓ
katika Siku itakapokuwa na kitisho?
Verse 6
ﭔﭕﭖﭗﭘ
ﭙ
Siku watakaposimama watu mbele ya Mweyezi Mungu ili Awahesabu kwa machache na mengi walioyatenda, hali ya kuwa wao Siku Hiyo ni wenye kumnyenyekea Mwenyezi Mungu, Mlezi wa viumbe vyote.
Verse 7
ﭚﭛﭜﭝﭞﭟ
ﭠ
Hakika marejeo ya watu waovu na makazi yao yatakuwa katika hali ya dhiki.
Verse 8
ﭡﭢﭣﭤ
ﭥ
Na ni kipi kinachokujulidha dhiki hii ni ipi?
Verse 9
ﭦﭧ
ﭨ
Hakika hiyo itakuwa ni jela ya kudumu na adhabu iliyo na uchungu. Penye jela hiyo ni pale walipoandikiwa kuwa watakwenda. Wameandikiwa na imepitishwa. Hapana kitakachozidishwa wala kupunguzwa.
Verse 10
ﭩﭪﭫ
ﭬ
Adhabu kali Siku Hiyo ni ya wale wenye kukanusha.
Verse 11
ﭭﭮﭯﭰ
ﭱ
Wale ambao wanakanusha kuwako tukio la Siku ya Malipo.
Verse 12
Na wala haikanushi Siku Hiyo isipokuwa kila dhalimu mwenye madhambi mengi.
Verse 13
Anaposomewa aya za Qur’ani, husema, «Hizi ni hadithi za urongo za watu wa kale.» Mambo yalivyo si kama wanavyodai!
Verse 14
Bali hayo ni maneno ya Mwenyezi Mungu na Wahyi Wake kwa Mtume Wake.
Verse 15
ﮍﮎﮏﮐﮑﮒ
ﮓ
Na hakika zimezibwa nyoyo zao zikawa hazimkubali Mwenyezi Mungu. Na kile kilichoziziba nyoyo hizo ni kufinikwa na wingi wa madhambi wanayoyafanya. Mambo hayako kama vile wanavyodai makafiri! Bali hakika wao, Siku ya Kiyama watazibwa wasimuone Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka na kushinda. Aya hii ni ushahidi kwamba Waumini watamuona Mola Wao Peponi.
Verse 16
ﮔﮕﮖﮗ
ﮘ
Kisha hakika hao makafiri ni wenye kuingia Motoni, na wataziona na kuzihisi dharubu zake.
Verse 17
Kisha wataambiwa,»Haya ndiyo malipo ya yale ambayo mlikuwa mnayakanusha.»
Verse 18
ﮡﮢﮣﮤﮥﮦ
ﮧ
Ni kweli kabisa kwamba kitabu cha watu wema, nao ni wachamungu, kiko katika ngazi za juu Peponi.
Verse 19
ﮨﮩﮪﮫ
ﮬ
Na ni kipi kinachokujulisha ni zipi hizi ngazi za juu?
Verse 20
ﮭﮮ
ﮯ
Ni kitabu cha watu wema kilichopitishwa mambo yake, hakizidishwi kitu humo wala hakipunguzwi.
Verse 21
ﮰﮱ
ﯓ
Wanayatazama yaliyomo ndani yake Malaika waliokurubishwa, wa kila mbingu.
Verse 22
ﯔﯕﯖﯗ
ﯘ
Hakika wale wenye ukweli na kufuata amri za Mwenyezi Mungu watakuwa Peponi wnaneemeka,
Verse 23
ﯙﯚﯛ
ﯜ
juu ya viti vya fahari wanamwangalia Mola wao na wanaangalia yale waliyoandaliwa miongoni mwa kheri nyingi.
Verse 24
ﯝﯞﯟﯠﯡ
ﯢ
Unaonekana katika nyuso zao mng’aro wa neema.
Verse 25
ﯣﯤﯥﯦ
ﯧ
Watanyweshwa tembo safi, lililotengezewa vyombo kwa ustadi na mwishowe kuna harufu ya miski.
Verse 26
Katika kuzipata neema hizo, nawashindane wenye kushindana.
Verse 27
ﯰﯱﯲ
ﯳ
Na kinywaji hiki, mchanganyo wake watokana na chemchemi iliyoko Peponi linalojulikana, kwa ubora wake, kwa jina la Tasnīm.
Verse 28
ﯴﯵﯶﯷ
ﯸ
Hiyo ni chemchemi iliyoandaliwa wale waliokurubishwa kwa Mwenyezi Mungu na watajiburudisha nayo.
Verse 29
Hakika wale waliotenda maovu walikuwa duniani wakiwacheza shere Waumini.
Verse 30
ﰂﰃﰄﰅ
ﰆ
Na wanapowapitia wanakonyezana kwa kuwakejeli.
Verse 31
ﰇﰈﰉﰊﰋﰌ
ﰍ
Na wnaporudi, hawa waovu, kwa watu wao na jamaa zao, huwa na vihunzi na wao kwa kuwafanyia maskhara Waumini.
Verse 32
ﰎﰏﰐﰑﰒﰓ
ﰔ
Na hawa makafiri wanapowaona Maswahaba wa Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, wamefuata uongofu, huwa wakisema, «Hakika hawa wamepotea kwa kumfuata Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie.
Verse 33
ﰕﰖﰗﰘ
ﰙ
Na wala waovu hawa hawakutumwa wawe ni wachunguzi kwa Maswahaba na Mtume , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie.
Verse 34
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖ
ﭗ
Basi Siku ya Kiyama wale waliomkubali Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wakafanya vitendo vinavyolingana na sheria Zake, watawafanyia maskhara makafiri kama makafiri walivyokuwa wakiwafanyia mashara duniani.
Verse 35
ﭘﭙﭚ
ﭛ
Juu ya viti vya fahari, watakuwa Waumini wanaangalia yale Aliyowapa Mwenyezi Mungu miongoni mwa mambo matukufu na neema, wakiwa Peponi. Na neema kubwa ya zote ni kuangalia Uso wa Mwenyezi Mungu Mtukufu.
Verse 36
ﭜﭝﭞﭟﭠﭡ
ﭢ
Je, wamelipwa makafiri, pindi watakapo kufanyiwa hayo, malipo muwafaka na yale waliyoyafanya duniani ya shari na madhambi?
تقدم القراءة