Tafsiri ya Sura Al-Inshikak kwa السواحلية kutoka الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس
Verse 1
ﭣﭤﭥ
ﭦ
Pindi mbingu itakapopasuka na kudhihiri mawingu katika pasuko zake Siku ya Kiyama.
Verse 2
ﭧﭨﭩ
ﭪ
Na ikatii amri ya Mola wake ya kuwa ipasuke, na inastahili kufuata amri hiyo.
Verse 3
ﭫﭬﭭ
ﭮ
Na pindi ardhi itakapotandikwa na kukunjuliwa.
Verse 4
ﭯﭰﭱﭲ
ﭳ
Na milima yake kuvunjwa-vunjwa Siku hiyo.
Verse 5
ﭴﭵﭶ
ﭷ
Na ikatii amri ya Mola wake ya kuwa ifanye hivyo, na inastahili kufuata amri hiyo.
Verse 6
Ewe binadamu, wewe unaenda kwa Mwenyezi Mungu na unafanya amali nzuri na mbaya, kisha utakutana na Yeye Siku ya Kiyama. Na huna budi kupata kutoka Kwake malipo mazuri zaidi ya amali yako njema au yanayolingana na amali yako mbaya.
Verse 7
ﮁﮂﮃﮄﮅ
ﮆ
Yule mwenye kupewa waraka wa amali zake kwa mkono wake wa kulia,
Verse 8
ﮇﮈﮉﮊ
ﮋ
naye ni yule aliyemuamini Mola wake, atahesabiwa hesabu pesi.
Verse 9
ﮌﮍﮎﮏ
ﮐ
Na atarudi kwa watu wake Peponi akiwa ni mwenye furaha.
Verse 10
ﮑﮒﮓﮔﮕﮖ
ﮗ
Na yule mwenye kupewa waraka wa amali zake kwa nyuma ya mgongo wake,
Verse 11
ﮘﮙﮚ
ﮛ
naye ni yule aliyemkanusha Mwenyezi Mungu, ataita maangamvu na hasara,
Verse 12
ﮜﮝ
ﮞ
na ataingia Motoni.
Verse 13
ﮟﮠﮡﮢﮣ
ﮤ
Hakika yeye alikuwa kwa watu wake ulimwenguni ni mwenye furaha na majivuno, hafikirii mwisho wake utakuwa namna gani.
Verse 14
ﮥﮦﮧﮨﮩ
ﮪ
Alidhani hatarudi kwa Muumba wake, akiwa hai, kwa kuhesabiwa.
Verse 15
Sivyo hivyo! Mwenyezi Mungu Atamrudisha kama alivomuumba na kumlipa kwa amali zake. Kwani Yeye kwake ni Mtambuzi na kwa hali yake ni Mjuzi kuanzia Alipomuumba mpaka kumfufua.
Verse 16
ﯔﯕﯖ
ﯗ
Mwenyezi Mungu Ameapa kwa wekundu wa pambizo za mbingu wakati wa kutwa jua.
Verse 17
ﯘﯙﯚ
ﯛ
Na kwa usiku na viunbe tofauti - tofauti vya kutambaa, kuruka na kutembea kwa miguu, uliokusanya.
Verse 18
ﯜﯝﯞ
ﯟ
Na kwa mwezi ukamilikapo mwangaza wake.
Verse 19
ﯠﯡﯢﯣ
ﯤ
Mtapitia, enyi watu, miongo mbalimbali na hali tofauti :kutoka kwenye tone la manii, kuptia pande la damu, nofu la nyama hadi kutiwa roho, mpaka kufa na mpaka kufufuliwa. Haifai kwa kiumbe kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu, afanyapo hilo atakuwa ameingia kwenye ushirikina.
Verse 20
ﯥﯦﯧﯨ
ﯩ
Ni kitu gani kinachowazuia kumwamini baada ya aya zake kufafanuliwa kwao?
Verse 21
Na wana nini wao wanaposomewa Qur’ani hawamsujudii Mwenyezi Mungu wala hawajisalimishi kufuata yaliyokuja ndani yake?
Verse 22
ﯲﯳﯴﯵ
ﯶ
Hakika tabia ya waliokufuru ni kuikanusha na kuikataa haki.
Verse 23
ﯷﯸﯹﯺ
ﯻ
Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi zaidi wa ukaidi wao wanaouficha kwenye nyoyo zao hali wao wanajua kuwa yale yaliyoletwa na Qur’ani ni kweli.
Verse 24
ﯼﯽﯾ
ﯿ
Basi wape bishara, ewe Mtume, kuwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka na kuwa juu, Amewaandalia adhabu yenye uchungu.
Verse 25
Lakini wale wanaomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wakatekeleza amri waliyofaradhiwa na Mwenyezi Mungu watakuwa na malipo, Siku ya Akhera, yasiyokatika wala kupungua.
تقدم القراءة