Tafsiri ya Sura An-Nazi'at kwa السواحلية kutoka الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس
Verse 1
ﮢﮣ
ﮤ
Anaapa Mwenyezi Mungu kwa Malaika ambao huzing’oa roho za makafiri mng’oo mkali.
Verse 2
ﮥﮦ
ﮧ
Na kwa Malaika ambao huzitukua roho za Waumini kwa uchangamfu na upole.
Verse 3
ﮨﮩ
ﮪ
Na kwa Malaika wanaoogelea katika kushuka kwao kutoka mbinguni na kupaa kwao kwenda mbinguni.
Verse 4
ﮫﮬ
ﮭ
Na kwa Mlaika ambao wanakimbilia kutekeleza amri za Mwenyezi Mungu.
Verse 5
ﮮﮯ
ﮰ
Na kwa Malaika wanaopitisha amri za Mola wao katika mambo ya ulimwengu waliowakilishwa kuyafanya na kuyasimamia, - Wala haifai kwa kiumbe kukiapia chochote kile, bali yapasa kiapo chake kiwe ni kwa jina la Mola wake Muumba au sifa Zake. Na lau ataapa kwa asiye Muumba wake, basi huyo amekuwa mshirikina - Watafufuliwa viumbe bila shaka na watahesabiwa.
Verse 6
ﮱﯓﯔ
ﯕ
Siku ambayo ardhi itatetemeka kwa mvuvuo wa kwanza:
Verse 7
ﯖﯗ
ﯘ
mvuvio wa kufisha, ukifuatiwa na mvuvio mwingine wa kuhuisha.
Verse 8
ﯙﯚﯛ
ﯜ
Nyoyo za makafiri, Siku hiyo, zitakuwa na papatiko kwa kicho kikubwa.
Verse 9
ﯝﯞ
ﯟ
Macho ya makafiri hao yatakuwa madhalilifu kwa kitisho watakachokiona.
Verse 10
ﯠﯡﯢﯣﯤ
ﯥ
Wanasema hawa wakanushao kufufuliwa:
Verse 11
ﯦﯧﯨﯩ
ﯪ
«Je, tutarudishwa baada ya kufa kwetu kwenye yale tuliyokuwa nayo katika ardhi? Je, tutarudishwa na hali tushakuwa mifupa iliochakaa?»
Verse 12
ﯫﯬﯭﯮﯯ
ﯰ
Wakasema: «Kurejea kwetu huko kutakuwa kutupu kusikokuwa kweli.’
Verse 13
ﯱﯲﯳﯴ
ﯵ
Hakika tukio hilo litakuwa kwa mvivio mmoja tu.
Verse 14
ﯶﯷﯸ
ﯹ
Wakitahamaki wao wako hai juu ya ardhi baada ya kuwa walikuwa ndani yake.
Verse 15
ﯺﯻﯼﯽ
ﯾ
Je imekujilia, ewe Mtume, habari ya Mūsā?
Verse 16
ﯿﰀﰁﰂﰃﰄ
ﰅ
Pindi Mola wake Alipomwita katika bonde lililotakaswa na kubarikiwa, la Ṭuwā. Akamwambia:
Verse 17
ﭑﭒﭓﭔﭕ
ﭖ
«Enda kwa Firauni. Hakika yeye amekiuka mno katika kuasi.
Verse 18
ﭗﭘﭙﭚﭛﭜ
ﭝ
Ukamwambie, ‘Je, unapendelea kuitakasa nafsi yako na upungufu na kuipamba na imani?
Verse 19
ﭞﭟﭠﭡ
ﭢ
Na nikuelekeze njia ya kumtii Mola wako, upate kumcha na kumuogopa?’»
Verse 20
ﭣﭤﭥ
ﭦ
Mūsā alimuonyesha Firauni alama kubwa: fimbo na mkono.
Verse 21
ﭧﭨ
ﭩ
Hapo Firauni alimkanusha Nabii wa Mwenyezi Mungu , naye ni Mtume Mūsā, amani imshukie, na alimuasi Mola wake Aliyetukuka.
Verse 22
ﭪﭫﭬ
ﭭ
Kisha alikengeuka hali ya kuipa mgongo Imani na kufanya bidii katika kumpinga Mūsā.
Verse 23
ﭮﭯ
ﭰ
Hapo aliwakusanya raia wa utawala wake na akawaita kwa
Verse 24
ﭱﭲﭳﭴ
ﭵ
kuwaambia,»Mimi ndiye mola wenu ambaye hakuna mola mwengine aliye juu yake.»
Verse 25
ﭶﭷﭸﭹﭺ
ﭻ
Hapo Mwenyezi Mungu Alimtesa kwa adhabu ya duniani na ya Akhera.
Verse 26
ﭼﭽﭾﭿﮀﮁ
ﮂ
Na Akaifanya adhabu hiyo iwe ni mazingatio na ni onyo kwa watu mfano wake kati ya wale waasi. Hakika Firauni na kile kilichompata cha adhabu ni mawaidha kwa mwenye kuwaidhika na kutishika.
Verse 27
Je, kufufuliwa kwenu, enyi watu, baada ya kufa ni kugumu zaidi, katika vipimo vyenu, au ni kuumbwa kwa mbingu?
Verse 28
ﮋﮌﮍ
ﮎ
Amezipanga juu yenu kama jengo. Na Ameinua sakafu yake angani, haina tofauti wala nyufa.
Verse 29
ﮏﮐﮑﮒ
ﮓ
Na Ameutia giza usiku wake kwa kutwa kwa jua lake. Na Ameweka wazi mchana wake kwa kuchomoza kwake.
Verse 30
ﮔﮕﮖﮗ
ﮘ
Na ardhi baada ya kuumba mbingu Ameitandaza. Na Ameweka humo manufaa yake.
Verse 31
ﮙﮚﮛﮜ
ﮝ
Na Ametumbua humo chemchemu za maji. Na Ameotesha humo mimea inayolishwa.
Verse 32
ﮞﮟ
ﮠ
Na Ameyakita humo majabali yakiwa ni vigingi vyake. Ameumba, Aliyetakasika na kila upungufu,
Verse 33
ﮡﮢﮣ
ﮤ
neema zote hizi zikiwa ni manufaa kwenu na kwa wanyama wenu. (Hakika kurudisha kuumbwa kwenu, Siku ya Kiyama, ni sahali kwa Mwenyezi Mungu kushinda kuumba viumbe hivyo vyingine. Na vyote hivyo, kwa Mwenyezi Mungu, ni rahisi na ni vipesi).
Verse 34
ﮥﮦﮧﮨ
ﮩ
Pindi kitakapokuja Kiyama Kikubwa na balaa nzito, nao ni Mvuvio wa pili. Kipindi hicho zitaoneshwa kwa binadamu vitendo vyake vyote, za kheri na za shari.
Verse 35
ﮪﮫﮬﮭﮮ
ﮯ
Hapo atazikumbuka na kuzitambua.
Verse 36
ﮰﮱﯓﯔ
ﯕ
Na utaoneshwa Moto wa Jahanamu kwa kila aonaye, uwe waonekana waziwazi.
Verse 37
ﯖﯗﯘ
ﯙ
Ama yule atakayekiuka amri ya Mwenyezi Mungu
Verse 38
ﯚﯛﯜ
ﯝ
na akapendelea maisha ya ulimwenguni kuliko ya Akhera,
Verse 39
ﯞﯟﯠﯡ
ﯢ
basi kwa kweli marejeo yake ni Motoni.
Verse 40
Na ama yule atakayeogopa kusimama mbele ya Mwenyezi Mungu kuhesabiwa na akaikanya nafsi yake na matamanio mapotofu,
Verse 41
ﯭﯮﯯﯰ
ﯱ
basi Peponi ndiko makazi yake.
Verse 42
ﯲﯳﯴﯵﯶ
ﯷ
Wanakuuliza washirikina, ewe Mtume, kwa madharau, kuhusu wakati wa kuanzia Kiyama unachowaonya.
Verse 43
ﯸﯹﯺﯻ
ﯼ
Wewe huna kamwe ujuzi nacho.
Verse 44
ﯽﯾﯿ
ﰀ
Bali mambo ya ujuzi huo yarejeshwe kwa Mwenyezi Mungu, Mwenye Sifa Tukufu.
Verse 45
ﰁﰂﰃﰄﰅ
ﰆ
Wewe linalokuhusu katika habari zake ni kumuonya nacho yule anayekiogopa.
Verse 46
Kama kwamba wao siku watakapouona Kiyama kimesimama, watakuwa hawakukaa katika maisha yao ya duniani, kwa vituko vya hiko Kiyama, isipokuwa ni kama kwamba wamkaa kati ya adhuhuri mpaka kutwa juwa, au ni kama kati ya kuchomoza jua mpaka nusu ya mchana.
تقدم القراءة