Tafsiri ya Sura Al-Waki'ah kwa السواحلية kutoka الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس
Verse 1
ﮃﮄﮅ
ﮆ
Kitakaposimama Kiyama.
Verse 2
ﮇﮈﮉ
ﮊ
Hakutakuwa na yoyote mwenye kukanusha kusimama kwake.
Verse 3
ﮋﮌ
ﮍ
Ni chenye kuwainamisha chini maadui wa Mwenyezi Mungu ndani ya Moto na ni chenye kuwainua juu Peponi wale wenye kumtegemea.
Verse 4
ﮎﮏﮐﮑ
ﮒ
Itakapotikiswa ardhi mtikiso wa nguvu.
Verse 5
ﮓﮔﮕ
ﮖ
Na yakamumunyuliwa majabali mmumunyuo wa kina.
Verse 6
ﮗﮘﮙ
ﮚ
Yakawa vumbi lenye kuruka angani lililosukumwa na upepo.
Verse 7
ﮛﮜﮝ
ﮞ
Na mkawa, enyi viumbe, makundi matatu:
Verse 8
ﮟﮠﮡﮢﮣ
ﮤ
Kundi la watu wa upande wa kulia, wenye daraja kubwa. Ni kikubwa kilioje cheo chao!
Verse 9
ﮥﮦﮧﮨﮩ
ﮪ
Kuna na kundi la watu wa upande wa kushoto, wenye daraja duni. Ni mbaya iliyoje hali yao!
Verse 10
ﮫﮬ
ﮭ
Na wale waliotangulia mbele kwenye kheri duniani ndio wenye kutangulia mbele kwenye daraja za juu huko Akhera.
Verse 11
ﮮﮯ
ﮰ
Wao ndio walioletwa karibu kwa Mwenyezi Mungu,
Verse 12
ﮱﯓﯔ
ﯕ
Mola wao Atawatia kwenye mabustani ya Pepo ya starehe.
Verse 13
ﯖﯗﯘ
ﯙ
Watayaingia watu wengi watu wa mwanzo wa ummah huu, na ummah wengineo wasiokuwa wao,
Verse 14
ﯚﯛﯜ
ﯝ
na wachache miongoni mwa watu mwisho wa ummah huu,
Verse 15
ﯞﯟﯠ
ﯡ
wakiwa juu ya vitanda vilivyofumwa kwa dhahabu,
Verse 16
ﯢﯣﯤ
ﯥ
na wakiwa katika hali ya kuvitegemea na huku wanaelekeana na kukutana.
Verse 17
ﭑﭒﭓﭔ
ﭕ
Wanawazunguka wao kuwatumikia watumishi vijana wasiozeeka wala kufa,
Verse 18
ﭖﭗﭘﭙﭚ
ﭛ
wakiwa na vikombe, mabirika na gilasi kutoka kwenye chemchemi ya pombe yenye kupita ndani ya Pepo,
Verse 19
ﭜﭝﭞﭟﭠ
ﭡ
na hawaumwi na vichwa kutokana nayo wala hawarukwi na akili.
Verse 20
ﭢﭣﭤ
ﭥ
Na watawazunguka wao watumishi vijana na kila kitu wanachokichagua miongoni mwa matunda,
Verse 21
ﭦﭧﭨﭩ
ﭪ
nyama ya ndege ambayo nafsi zao inavutika nayo.
Verse 22
ﭫﭬ
ﭭ
Na watakuwa na wanawake wenye macho makubwa kama kwamba wao,
Verse 23
ﭮﭯﭰ
ﭱ
kwa usafi wao na uzuri wao, ni lulu iliyohifadhiwa ndani ya mashaza yake,
Verse 24
ﭲﭳﭴﭵ
ﭶ
hali hayo yakiwa ni malipo yao kwa yale waliokuwa wakiyafanya duniani.
Verse 25
ﭷﭸﭹﭺﭻﭼ
ﭽ
Hawatasikia humo Peponi ubatilifu wala yale ya kuwatia madhambini kuyasikia,
Verse 26
ﭾﭿﮀﮁ
ﮂ
isipokuwa maneno yasiyokuwa na kasoro hizi na kusalimiana wao kwa wao.
Verse 27
ﮃﮄﮅﮆﮇ
ﮈ
Na watu wa upande wa kulia,
Verse 28
ﮉﮊﮋ
ﮌ
ni kikubwa kilioje cheo chao na malipo yao!
Verse 29
ﮍﮎ
ﮏ
Watakuwa kwenye mikunazi isiyo na miba, na ndizi zilizopandana na kupangika,
Verse 30
ﮐﮑ
ﮒ
kila ndizi juu ya nyingine, na vivuli vya daima visivyoondoka,
Verse 31
ﮓﮔ
ﮕ
na maji yanayotembea yasiyokatika,
Verse 32
ﮖﮗ
ﮘ
na matunda mengi
Verse 33
ﮙﮚﮛﮜ
ﮝ
yasiyomalizika wala kuwaishia wala hakuna kizuizi chochote kinachowazuia wao kuyafikia,
Verse 34
ﮞﮟ
ﮠ
na matandiko yaliyoinuliwa juu ya vitanda.
Verse 35
ﮡﮢﮣ
ﮤ
Sisi tumewaumba wanawake wa watu wa Peponi umbile ambalo silo lile umbile lililokuwa duniani, umbile lililokamilika lisilokubali kutoweka,
Verse 36
ﮥﮦ
ﮧ
na tumewafanya ni wanawali wenye kujipendekeza kwa waume zao,
Verse 37
ﮨﮩ
ﮪ
hali ya kuwa ni marika na wao kimiaka.
Verse 38
ﮫﮬ
ﮭ
Tumewaumbia wanawake hao watu wa upande wa kulia.
Verse 39
ﮮﮯﮰ
ﮱ
Nao ni kundi la watu wengi wa mwanzo
Verse 40
ﯓﯔﯕ
ﯖ
na kundi la watu wengi wa mwisho.
Verse 41
ﯗﯘﯙﯚﯛ
ﯜ
Na watu wa upande wa kushoto, ni mbaya iliyoje hali yao na malipo yao!
Verse 42
ﯝﯞﯟ
ﯠ
Watakuwa kwenye upepo ulio moto utokanao na joto la Moto wa Jahanamu utakaozuia pumzi zao, na maji moto yanayochemka,
Verse 43
ﯡﯢﯣ
ﯤ
na kivuli cha moshi mweusi sana,
Verse 44
ﯥﯦﯧﯨ
ﯩ
usio na mashukio baridi wala mandhari mazuri.
Verse 45
ﯪﯫﯬﯭﯮ
ﯯ
Kwani wao walikuwa duniani wakijistarehesha kwa vitu vya haramu wakijiepusha na yale ambayo Mitume walikuja nayo.
Verse 46
ﯰﯱﯲﯳﯴ
ﯵ
Na walikuwa wamesimama wima katika kumkanusha Mwenyezi Mungu na kumshirikisha na kumuasi, na hawakuwa na nia ya kutubia kwa hayo.
Verse 47
Na walikuwa wakisema hali ya kukanusha Ufufuzi, «Je hivi sisi tutafufuliwa tutakapokufa na tukawa mchanga na mifupa iliyochakaa?» Maneno yao hayo yanaonesha kuwa wao walikuwa wakiliona jambo hili la kufufuliwa kuwa liko mbali na ukweli na wakilikanusha.
Verse 48
ﰀﰁ
ﰂ
«Je tutafufuliwa sisi na hali baba zetu waliotangulia wamekuwa mchanga uliotapakaa kwenye ardhi?»
Verse 49
ﰃﰄﰅﰆ
ﰇ
Sema uwaambie, «Hakika wa mwanzo na wa mwisho miongoni mwa binadamu
Verse 50
ﰈﰉﰊﰋﰌ
ﰍ
watakusanywa katika Siku iliyowekewa wakati maalumu, nayo ni Siku ya Kiyama.
Verse 51
ﭑﭒﭓﭔﭕ
ﭖ
«Kisha nyinyi, enyi mliopotea njia ya uongofu mnaokanusha onyo la Mwenyezi Mungu na agizo Lake,
Verse 52
ﭗﭘﭙﭚﭛ
ﭜ
ni wenye kula kutokana na mti wa zaqqūm,
Verse 53
ﭝﭞﭟ
ﭠ
nao ni katika miti mibaya zaidi, na ni wenye kujaza matumbo yenu kutokana nao kwa sababu ya ukali wa njaa,
Verse 54
ﭡﭢﭣﭤ
ﭥ
na ni wenye kunywa juu yake maji yaliyo moto hadi ya mwisho, yasiyomaliza kiu.
Verse 55
ﭦﭧﭨ
ﭩ
Mtayanywa maji hayo kwa wingi kama vile ngamia wenye kiu wasioshiba maji kwa ugonjwa uliowapata.»
Verse 56
ﭪﭫﭬﭭ
ﭮ
Adhabu hii watakayoipata ndiyo zawadi Aliyowaandalia Siku ya Kiyama. Katika haya kuna kuwalaumu na kuwacheza shere.
Verse 57
ﭯﭰﭱﭲ
ﭳ
Sisi tumewaumba, enyi watu, na hamkuwa kitu chochote. Basi si msadiki kuwa kuna kufufuliwa?
Verse 58
ﭴﭵﭶ
ﭷ
Mnayaonaje maji ya manii mnayoyatupa ndani ya vizazi vya wake zenu,
Verse 59
ﭸﭹﭺﭻﭼ
ﭽ
je nyinyi ndio mnaomuumba mwanadamu kutokana na hayo au ni sisi ndio wenye kuumba?
Verse 60
Sisi tumekadiria kifo kwenu,
Verse 61
na sisi si wenye kushindwa kubadilisha umbo lenu Siku ya Kiyama na kuwaumba kwa sifa na namna msizozijua.
Verse 62
ﮐﮑﮒﮓﮔﮕ
ﮖ
Na hakika mlijua kuwa Mwenyezi Mungu Aliwaumba uumbaji wa kwanza na hamkuwa kitu chochote. Basi si mkumbuke uweza wa Mwenyezi Mungu wa kuwaumba mara nyingine?
Verse 63
ﮗﮘﮙ
ﮚ
Mnazionaje mbegu mnazozipanda?
Verse 64
ﮛﮜﮝﮞﮟ
ﮠ
Je ni nyinyi mnaoziotesha kutoka ardhini? Sisi ndio tuaozituliza na kuziotesha ardhini.
Verse 65
ﮡﮢﮣﮤﮥﮦ
ﮧ
Lau tungalitaka tungaliifanya mimea inayotokana na mbegu hizo kuwa mapepe, haimkiniki kunufaika nayo kwa kula,
Verse 66
ﮨﮩ
ﮪ
mkawa mnaona ajabu kwa kilichoshukia mimea yenu na mnasema, «Sisi tumepata hasara na ni wenye kuungulika.
Verse 67
ﮫﮬﮭ
ﮮ
Bali sisi tumekoseshwa riziki.»
Verse 68
ﮯﮰﮱﯓ
ﯔ
Mnayaonaje maji mnayokunywa ili mhuike kwayo?
Verse 69
Je ni nyinyi mliyoyateremsha kutoka kwenye mawingu hadi kwenye kituo cha ardhi au ni sisi tuliyoyateremsha ili kuwarehemu nyinyi?
Verse 70
ﯝﯞﯟﯠﯡﯢ
ﯣ
Lau tungalitaka tungaliyafanya maji haya yawe na chumvi sana, ikiwa haiwezekani kunufaika nayo kwa kunywa wala kwa mimea. Basi si mumshukuru Mola wenu kwa kuteremsha maji tamu kwa kuwanufaisha nyinyi.
Verse 71
ﯤﯥﯦﯧ
ﯨ
Mnaouonaje moto mnaouwasha?
Verse 72
ﯩﯪﯫﯬﯭﯮ
ﯯ
Je ni nyinyi mlioufanya mti wake, unaozalisha moto kwa kukwaruzwa, upatikane au ni sisi tulioufanya upatikane?
Verse 73
ﯰﯱﯲﯳﯴ
ﯵ
Sisi tumeufanya moto wenu mnaouwasha ni ukumbusho kwenu wa Moto wa Jahanamu na pia ni manufaa kwa wasafiri.
Verse 74
ﯶﯷﯸﯹ
ﯺ
Basi mtakase Mola wako, ewe Nabii, Aliye mtukufu Mwenye ukamilifu wa majina na sifa, Mwingi wa wema na kheri.
Verse 75
ﯻﯼﯽﯾﯿ
ﰀ
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa mapomoko ya nyota nyakati za kuzama kwake mbinguni.
Verse 76
ﰁﰂﰃﰄﰅ
ﰆ
Nacho ni kiapo kikubwa lau mnajua kadiri yake.
Verse 77
ﭑﭒﭓ
ﭔ
Hakika hii Qur’ani iliyoteremshiwa Muhammad ni Qur’ani yenye manufaa makubwa, yenye kheri nyingi na yenye elimu tele,
Verse 78
ﭕﭖﭗ
ﭘ
iliyo ndani ya Kitabu kilichohifadhiwa, kilichofichwa na macho ya viumbe, nacho ni Kitabu ambacho kiko mikononi mwa Malaika.
Verse 79
ﭙﭚﭛﭜ
ﭝ
Hawaigusi Qur’ani isipokuwa malaika watukufu ambao Mwenyezi Mungu Amewasafisha na aibu na madhambi. Na pia hawaigusi isipokuwa watu waliojitohirisha na ushirikina na janaba na ukosefu wa udhu.
Verse 80
ﭞﭟﭠﭡ
ﭢ
Na hii Qur’ani tukufu imeteremshwa kutoka kwa Mola wa viumbe vyote, kwani hiyo ndiyo haki isiyo na shaka ndani yake.
Verse 81
ﭣﭤﭥﭦ
ﭧ
je hii Qur’ani, enyi washirikina, mnaikanusha?
Verse 82
ﭨﭩﭪﭫ
ﭬ
Na je mnaifanya shukrani yenu kwa neema za Mola wenu ni kuwa nyinyi mnazikanusha na kukufuru? Hapa pana makaripio kwa anayedharau amri za Qur’ani na kutojali mwito wake.
Verse 83
ﭭﭮﭯﭰ
ﭱ
Basi je mnaweza pindi roho ya mmoja wenu inapofika kwenye koo katika uchungu wa kifo,
Verse 84
ﭲﭳﭴ
ﭵ
na hali nyinyi mmehudhuria mnamtazama, kuizuia roho yake ndani ya mwili wake? Hamtaweza hilo!
Verse 85
Na sisi tuko karibu na yeye zaidi, kupitia Malaika wetu, kuliko nyinyi, lakini nyinyi hamuwaoni.
Verse 86
ﭾﭿﮀﮁﮂ
ﮃ
Na je mnaweza, iwapo nyinyi si wenye kuhesabiwa wala kulipwa kwa matendo yenu,
Verse 87
ﮄﮅﮆﮇ
ﮈ
kuirudisha roho kwenye mwili, iwapo nyinyi ni wakweli? Hamtaweza kuirudisha.
Verse 88
ﮉﮊﮋﮌﮍ
ﮎ
Basi iwapo yule anayekufa ni kati ya watu wa upande wa kulia, atapata rehema kunjufu na furaha,
Verse 89
ﮏﮐﮑﮒ
ﮓ
wakati wa kufa kwake, na kila kinachoifurahisha nafsi yake, Na atapata Pepo ya starehe huko Akhera.
Verse 90
ﮔﮕﮖﮗﮘﮙ
ﮚ
Na iwapo yule anayekufa ni kati ya watu wa upande wa kulia,
Verse 91
ﮛﮜﮝﮞﮟ
ﮠ
ataambiwa, «Umesalimika na kuwa kwenye amani, kwa kuwa wewe ni miongoni mwa watu wa upande wa kulia.»
Verse 92
ﮡﮢﮣﮤﮥﮦ
ﮧ
Na iwapo yule anayekufa ni miongoni mwa wenye kukanusha kufufuliwa, waliopotoka na njia ya uongofu,
Verse 93
ﮨﮩﮪ
ﮫ
basi atapata makaribisho ya kinywaji cha moto wa Jahanamu kilichochemshwa, kilicho na joto hadi ya mwisho,
Verse 94
ﮬﮭ
ﮮ
na atachomwa na Moto na aungulike na adhabu yake kali.
Verse 95
ﮯﮰﮱﯓﯔ
ﯕ
Hakika habari hii tumezokuelezea, ewe Mtume, ni ukweli wa yakini usio na shaka.
Verse 96
ﯖﯗﯘﯙ
ﯚ
Basi litakase jina la Mola wako Aliyetukuka na umtakase na yale ambayo madhalimu na wenye kukanusha wanayasema. Mwenyezi Mungu Yuko juu ya yale wanayoyasema ujuu mkubwa sana.
تقدم القراءة