Tafsiri ya Sura Kuraish kwa السواحلية kutoka الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس
Verse 1
ﭑﭒ
ﭓ
Oneni ajabu ya mazowea ya Makureshi, amani walionayo, kuwaendea uzuri mambo yao,
Verse 2
ﭔﭕﭖﭗ
ﭘ
kupangika na kusahilika misafara yao ya kwenda Yamani kipindi cha kusi na kwenda Shamu kipindi cha kaskazi, ili kuleta vitu wanavyohitajia.
Verse 3
ﭙﭚﭛﭜ
ﭝ
Basi, wamshukuru na kumuabudu Bwana wa Nyumba hii ya Alkaba, Ambaye kwa ajili Yake wametukuzwa, na wampwekeshe na kumtakasia ibada.
Verse 4
Ambaye Amewapa wao chakula wakati wa njaa kali na akawapa amani na utulivu kutokana na kicho kikubwa na babaiko.
تقدم القراءة