Tafsiri ya Sura At-Takasur kwa السواحلية kutoka الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس
Verse 1
ﮣﮤ
ﮥ
Kumewashughulisha kujifahiri kwa mali na watoto mkawacha kumtii Mwenyezi Mungu
Verse 2
ﮦﮧﮨ
ﮩ
Kujishughulisha kwenu na hilo kumeendelea mpaka mkawa makaburini na mkazikwa humo.
Verse 3
ﮪﮫﮬ
ﮭ
Siyo namna hii inatakiwa iwapumbaze kushindana kwa wingi wa mali. Itawadhihirikia kuwa Nyumba ya Akhera ni bora kwenu.
Verse 4
ﮮﮯﮰﮱ
ﯓ
Kisha tahadharini mtajua mwisho mbaya wa kutojishughulisha na Akhera.
Verse 5
ﯔﯕﯖﯗﯘ
ﯙ
Siyo namna hii inatakiwa iwashughulishe kushindana kwa wingi wa mali.Lau mnajua kikweli, mngalirudi nyuma na mngaliangusiliza kuokoa nafsi zenu kutoka kwenye maangamivu.
Verse 6
ﯚﯛ
ﯜ
Mtauona Moto!
Verse 7
ﯝﯞﯟﯠ
ﯡ
Kisha mtauona bila shaka!
Verse 8
ﯢﯣﯤﯥﯦ
ﯧ
Kisha mtaulizwa kuhusu kila aina ya starehe mliyokuwa nayo.
تقدم القراءة