سورة عبس

الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس

Tafsiri ya Sura Abasa kwa السواحلية kutoka الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس

الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس

Verse 1
Yalidhihiri mabadiliko na mkunjiko katika uso wa Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie,
Verse 2
na akapa nyongo kwa sababu ya kwamba Abdallah bin Ummi Maktum alimjilia akitaka aelekezwe. Na alikuwa Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, ameshughulika kuwalingania miamba wa Kikureshi katika Uislamu.
Verse 3
Ni kitu gani kinakufanya wewe ujue uhakika wa jambo lake? Kwani huenda ikawa, kwa kuuliza kwake, nafsi yake itatakasika na kusafika.
Verse 5
Basi yule alijyejitosheleza na kutouhitajia uongozi wako,
Verse 6
wewe ndiye unayemjali na wapulikiza maneno yake.
Verse 7
Na ni kitu gani kinachokupa jukumu kwako iwapo hakusafika na ukafiri wake?
Verse 9
na huku anamuogopa Mwenyezi Mungu asiwe na kasoro katika kupata uongofu,
Verse 10
wewe unampuuza. Ilivyotakikana ufanye si kama ulivyofanya, ewe Mtume.
Verse 11
Hakika Sura hii ni mawaidha kwako na kwa kila anayetaka kuwaidhika.
Verse 12
Basi atakaye atamkumbuka Mwenyezi Mungu na kumtaja na atafuata Wahyi Wake.
Verse 13
Wahyi huu, nao ni Qur’ani, uko katika kurasa zilizotukuzwa,
Verse 14
zenye kuheshimiwa, zenye cheo cha juu,
Verse 15
zilizosafishwa na uchafu, uongezaji na upunguzaji.
Verse 16
Zilizoko mikononi mwa Malaika waandishi, mabalozi kati ya Mwenyezi Mungu na viumbe Wake, wenye maumbile mema, tabia zao ni nzuri na njema na pia matendo yao.
Verse 17
Amelaaniwa mtu kafiri na ataadhibiwa. Ni uovu ulioje wa ukafiri wake kwa Mola wake!
Verse 18
Kwani hajui ni kwa kitu gani Mwenyezi Mungu Alimuumba kwacho mwanzo wake?
Verse 19
Mwenyezi Mungu Alimuumba kwa maji machache, nayo ni manii. Akayakadiria miongo yake.
Verse 20
Kisha Akambainishia njia ya kheri na ya shari.
Verse 21
Kisha humkosesha uhai, na Amemuekea mahali pa kuzikiwa.
Verse 22
Kisha Akitaka Mwenyezi Mungu, Aliyetakasika na sifa mbaya, Atamhuisha na kumfufua baada ya kifo chake, kwa ajili ya kuhesabiwa na kulipwa.
Mambo siyo kama yale anayoyasema kafiri na anayoyafanya. Bado hajatakeleza Aliyomuamrisha kwayo Mwenyezi Mungu katika kuamini na kutenda wema kwa kumtii.
Verse 24
Na azingatie binadamu, vipi Mwenyezi Mungu Amekiumba chakula chake ambacho ndicho kinachoendeleza maisha yake?
Verse 25
Aone kwamba Sisi Tumeyamimina maji ya mvua juu ya ardhi kwa wingi.
Verse 26
Kisha Tumeipasua ardhi kwa Tulivyo vitoa kutoka humo miongoni mwa mimea tofauti.
Verse 28
na zabibu, na nyasi za wanyama.Na mizaituni na mitende.
Verse 32
Mnajistareheshea kwazo, nyinyi na wanyama wenu.
Verse 33
Utakapokuja Ukelele wa Siku ya Kiyama, ambao utayatia uziwi, kwa kitisho chake, masikizi.
Verse 38
Nyuso za wenye neema, Siku Hiyo, zitakuwa ni zenye kung’ara,
Verse 42
Hao wenye kusifika na sifa hiyo ndiwo wale waliozikufuru neema za Mwenyezi Mungu na wakazikanusha aya zake na wakayakeuka Aliyoyaharamisha kwa kutenda maovu na kukiuka mipaka.
تقدم القراءة