Tafsiri ya Sura Al-Infitar kwa السواحلية kutoka الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس
Verse 1
ﭑﭒﭓ
ﭔ
Pindi mbingu zitakapopasuka na ukaharibika mpango wake.
Verse 2
ﭕﭖﭗ
ﭘ
Na pindi nyota zitakapoangukiana.
Verse 3
ﭙﭚﭛ
ﭜ
Na pindi Mwenyezi Mungu Atakapozifanya bahari kulipuka na maji yake kutoweka.
Verse 4
ﭝﭞﭟ
ﭠ
Na pindi makaburi yatakapogeuzwa kwa kufufuliwa waliokuwamo ndani yake.
Verse 5
ﭡﭢﭣﭤﭥ
ﭦ
Wakati huo itajua kila nafsi vitendo vyake vyote ilivyovifanya, vilivyotangulia na vilivyoahirika na italipwa kwa vitendo hivyo.
Verse 6
ﭧﭨﭩﭪﭫﭬ
ﭭ
Ewe binadamu unayekanusha kufufuliwa! Ni kipi kilichokufanya uhadaike na ughurike kuhusu Mola wako Mpaji Mwenye kheri nyingi, Anayestahiki kushukuriwa na kutiiwa?
Verse 7
ﭮﭯﭰﭱ
ﭲ
Kwani si Yeye Aliyekuumba, Akalisawazisha umbo lako, Akakuweka katika hali ya sawa na Akakurekibisha ili uweze kutekeleza nyadhifa zako,
Verse 8
ﭳﭴﭵﭶﭷﭸ
ﭹ
katika sura yoyote ile Aliyoitaka Akakuumba?
Verse 9
ﭺﭻﭼﭽ
ﭾ
Mambo hayako kama vile mnavyosema kwamba nyinyi mna haki ya kumuabudu asiyekuwa Mwenyezi Mungu. Bali nyinyi mnaikanusha Siku ya Hesabu na Malipo.
Verse 10
ﭿﮀﮁ
ﮂ
Na mjue kuwa wako na nyinyi Malaika wachunguzi,
Verse 11
ﮃﮄ
ﮅ
watukufu kwa Mwenyezi Mungu, waandishi wa yale waliyowakilishwa kuyadhibiti. Hakiwapiti, katika vitendo vyenu na siri zenu, chochote.
Verse 12
ﮆﮇﮈ
ﮉ
Wanayajua mnayoyafanya, ya kheri au ya shari.
Verse 13
ﮊﮋﮌﮍ
ﮎ
Hakika wachamungu wanaotekeleza haki za Mwenyezi Mungu na haki za waja wake watakuwa kwenye neema.
Verse 14
ﮏﮐﮑﮒ
ﮓ
Hakika watu waovu waliopuuza haki za Mwenyezi Mungu na haki za waja wake watakuwa katika Moto mkali.
Verse 15
ﮔﮕﮖ
ﮗ
Ukali wake, Moto huo, utawapata Siku ya Malipo.Na wala wao hawatakuwa ni wenye kughibu,
Verse 16
ﮘﮙﮚﮛ
ﮜ
wakawa hawamo ndani ya Moto wa Jahanamu, si kwa kutoka wala kwa kufa.
Verse 17
ﮝﮞﮟﮠﮡ
ﮢ
Ni kipi kinachokujuza ni upi utukufu wa Siku ya Hesabu?
Verse 18
ﮣﮤﮥﮦﮧﮨ
ﮩ
Kisha ni kipi kinachokujuza ni upi utukufu wa Siku ya Hesabu?
Verse 19
Siku ya Hesabu, hataweza yoyote kumnufaisha yoyote. Na amri zote Siku Hiyo ni za Mwenyezi Mungu Peke yake Ambaye hakuna mwenye kumshinda, wala hakuna mwenye kumtendesha nguvu, wala hakuna mwenye kushindana na Yeye.
تقدم القراءة