Tafsiri ya Sura As-Saffat kwa السواحلية kutoka الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس
Verse 1
ﭑﭒ
ﭓ
Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Anaapa kwa Malaika wanaojipanga, katika kuabudu kwao, mistari iliyofuatana na kushikana,
Verse 2
ﭔﭕ
ﭖ
na kwa Malaika wanaofukuza mawingu na kuyaongoza kwa amri ya MwenyeziMungu,
Verse 3
ﭗﭘ
ﭙ
na kwa Malaika wanaosoma utajo wa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, na maneno Yake,
Verse 4
ﭚﭛﭜ
ﭝ
kwamba muabudiwa wenu, enyi watu, ni Mmoja, Asiye na mshirika. Hivyo basi mtakasieni ibada na utiifu. Na Anaapa Mwenyezi Mungu kwa Anachotaka miongoni mwa viumbe Vyake. Ama kiumbe, hafai kuapa isipokuwa kwa Mwenyezi Mungu, kwani kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu ni ushirikina.
Verse 5
Yeye Ndiye Muumba mbingu na ardhi na vilivyoko baina ya hivyo viwili, na Ndiye Mpelekeshaji jua katika sehemu zake za kuchomozea na zile za kuchwea.
Verse 6
ﭦﭧﭨﭩﭪﭫ
ﭬ
Sisi tumeupamba uwingu wa karibu kwa pambo la nyota.
Verse 7
ﭭﭮﭯﭰﭱ
ﭲ
Na tumeuhifadhi huo uwingu, kwa nyota, na kila shetani mwenye kuasi, mjeuri, aliyefukuzwa (kwenye rehema ya Mwenyezi Mungu).
Verse 8
Hawawezi hao Mashetani kufika kwenye viumbe vya juu, navyo ni mbingu na Malaika waliyomo ndani yake, wakapata kuwasikiliza wanapoutamka wahyi ambao Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Anauleta, unaokusanya sheria Yake na makadirio Yake, na wanavurumizwa vimondo katika kila upande,
Verse 9
ﭽﭾﭿﮀﮁ
ﮂ
kwa kuwafukuza ili wasipate kusikiliza. Na huko kwenye Nyumba ya Akhera watakuwa na adhabu ya daima yenye kuumiza.
Verse 10
Isipokuwa yule aliyenyakuwa, miongoni mwa Mashetani, mnyakuo wa haraka, nao ni lile neno analolisikia mbinguni kwa haraka, akamtupia aliyekuwa chini yake, na yule mwingine akamtupia aliyekuwa chini yake. Basi pengine huenda akafikiwa na kimondo chenye kutoa mwangaza kabla hajalitupa, na pengine huwa amelitupa kwa makadirio ya Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, kabla ya kujiwa na kimondo kikamchoma, na yule mwingine akaenda nalo hadi kwa makuhani wakaongeza juu ya neno hilo maneno mia moja ya urongo.
Verse 11
Basi waulize, ewe Mtume, wenye kukanusha Kufufuliwa: Je kuumbwa kwao ni kugumu zaidi au ni hivyi viumbe tulivyoviumba? Kwa hakika, tulimuumba baba yao Ādam kwa udongo ulioshikana na kuambatana.
Verse 12
ﮙﮚﮛ
ﮜ
Bali ulistaajabu, ewe Mtume, kwa ukanushaji wao na kukataa kwao Kufufuliwa. Na la kustaajabiwa zaidi na lililo kubwa zaidi kuliko lile la kukataa kwao ni kwamba wao wanakucheza shere na kulidharau neno lako.
Verse 13
ﮝﮞﮟﮠ
ﮡ
Na wanapokumbushwa walichokisahau au walichoghafilika nacho, hawanufaiki kwa huo ukumbusho wala hawazingatii.
Verse 14
ﮢﮣﮤﮥ
ﮦ
Na wanapoiona miujiza yenye kutolea dalili unabii wako, wanakufanyia shere na wanastaajabu.
Verse 15
ﮧﮨﮩﮪﮫﮬ
ﮭ
Na wanasema, «Halikuwa hili ulilotuletea isipokuwa ni uchawi uliojitokeza waziwazi.
Verse 16
Je, tunapokufa na tukawa ni mchanga na mifupa iliyochakaa, je sisi ni wenye kufufuliwa kutoka makaburini mwetu tukiwa hai?
Verse 17
ﯗﯘ
ﯙ
au pia watafufuliwa baba zetu waliopita kabla yetu?»
Verse 18
ﯚﯛﯜﯝ
ﯞ
Waambie, ewe Mtume, «Ndio mtafufuliwa hali mkiwa wanyonge, watwevu.»
Verse 19
Hakika ni kwamba huo utakuwa ni Mvuvio mmoja, wakitahamaki wao wamesimama kutoka makaburini mwao, wanatazama vituko vya Kiyama.
Verse 20
ﯧﯨﯩﯪﯫ
ﯬ
Na watasema, «Ewe maangamivu yetu! Hii ni siku ya kuhesabiwa na kulipwa!»
Verse 21
Hapo wataambiwa, «Hii ndiyo Siku ya Uamuzi wa haki baina ya viumbe, ambayo mlikuwa mkiikanusha duniani na mkiikataa.»
Verse 22
Na Malaika wataambiwa, «Wakusanyeni wale waliomkanusha Mwenyezi Mungu na wafananao na wao na waungu wao waliokuwa wakiwaabudu
Verse 23
badala ya Mwenyezi Mungu, na muwasukume kwa nguvu hadi kwenye moto wa Jahanamu.
Verse 24
ﰆﰇﰈﰉ
ﰊ
«Na muwafunge kabla hawajafika kwenye moto wa Jahanamu, kwa kuwa wao ni wenye kuulizwa kuhusu matendo yao na maneno yao yaliyotokana na wao duniani, kwa namna ya kumshtukia kuwakaripia.»
Verse 25
ﭑﭒﭓﭔ
ﭕ
Na wataambiwa kwa kulaumiwa, «Kwa nini hamsaidiani nyinyi kwa nyinyi?»
Verse 26
ﭖﭗﭘﭙ
ﭚ
Bali wao Leo ni wenye kufuata amri ya Mwenyezi Mungu, hawataenda kinyume nayo wala hawataepukana nayo, hawajisaidii wao wenyewe.
Verse 27
ﭛﭜﭝﭞﭟ
ﭠ
Na hapo makafiri watakabiliana wao kwa wao wakilaumiana na wakigombana.
Verse 28
ﭡﭢﭣﭤﭥﭦ
ﭧ
Wafuasi watasema kuwaambia wafuatwa, «Nyinyi mlikuwa mkitujia kwa upande wa dini na haki, mkiifanya Sheria ni twevu kwetu, mkitutia chuki nayo na mkitupambia upotevu.»
Verse 29
ﭨﭩﭪﭫﭬ
ﭭ
Hapo watasema wafuatwa kuwaabia wafuasi, «Mambo si kama vile mnavyodai, bali ni nyoyo zenu zilikuwa zimekataa kuamini, zimeuelekea ukafiri na uasi.
Verse 30
«Na sisi hatukuwa na hoja juu yenu wala nguvu, tukaweza kwa hizo kuwazuilia kuamini. Bali nyinyi wenyewe, enyi washirikina, mlikuwa waasi wenye kupita mipaka ya haki.
Verse 31
«Hivyo basi ndio sisi sote ikalazimu tupate onyo la Mola wetu kuwa ni wenye kuonja adhabu, sisi na nyinyi, kwa yale tuliyoyatanguliza ya madhambi na maasia duniani.
Verse 32
ﮂﮃﮄﮅ
ﮆ
« Ndipo tukawapoteza na njia ya Mwenyezi Mungu na ya kumuamini, kwa kuwa sisi wenyewe tulikuwa ni wapotevu kabla yenu. Na kwa hivyo tukapotea kwa sababu ya ukafiri wetu na tukawaangamiza nyinyi pamoja na sisi.»
Verse 33
ﮇﮈﮉﮊﮋ
ﮌ
Basi wafuasi na wafuatwa watashirikiana katika adhabu Siku ya Kiyama, kama walivyoshirikiana ulimwenguni katika kumuasi Mwenyezi Mungu.
Verse 34
ﮍﮎﮏﮐ
ﮑ
Hivi ndivyo sisi tunavyowafanyia waliochagua mambo ya kumuasi Mwenyezi Mungu ulimwenguni na wakaacha kumtii, basi tutawaonjesha adhabu kali.
Verse 35
Hakika wale washirikina walikuwa duniani wakiambiwa, «Hapana mola anayepasa kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu,» na wakaitwa kwenye mwito huo na wakaamrishwa kuyaacha yanayopingana nao, wanaufanyia kiburi na kumfanyia kiburi aliyekuja nao.
Verse 36
ﮝﮞﮟﮠﮡﮢ
ﮣ
Na wanasema, «Je, tuache kuwaabudu waungu wetu kwa maneno ya mshairi mwenye wazimu?» wakimkusudia Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie.
Verse 37
ﮤﮥﮦﮧﮨ
ﮩ
Wamesema urongo! Muhammad sivyo vile walivyomueleza. Bali amekuja na Qur’ani na upwekeshaji Mwenyezi Mungu, na akathibitisha ukweli wa Mitume katika kile walichokitolea habari kuhusu sheria ya Mwenyezi Mungu na kumpwekesha Yeye.
Verse 38
ﮪﮫﮬﮭ
ﮮ
Hakika yenu nyinyi, enyi washirikina, kwa neno lenu, ukafiri wenu na kukanusha kwenu, ni wenye kuonja adhabu iliyo kali yenye uchungu.
Verse 39
ﮯﮰﮱﯓﯔﯕ
ﯖ
Na hamtalipwa huko Akhera isipokuwa kwa lile la maasia mliokuwa mkilifanya duniani.
Verse 40
ﯗﯘﯙﯚ
ﯛ
Isipokuwa waja wa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, waliomtakasia Ibada Yake, Akawatakasa na Akawahusu wao kwa rehema Yake, basi hao kwa hakika ni wenye kuokoka na adhabu yenye uchungu.
Verse 41
ﯜﯝﯞﯟ
ﯠ
Hao waliotakaswa watapata riziki ijulikanayo isiyokatika ndani ya Pepo.
Verse 42
ﯡﯢﯣ
ﯤ
Riziki hiyo ni matunda aina mbalimbali. Na wao ni wenye kukirimiwa kwa takrima ya Mwenyezi Mungu
Verse 43
ﯥﯦﯧ
ﯨ
kuwafanyia wao ndani ya mabustani ya Pepo ya starehe ya milele.
Verse 44
ﯩﯪﯫ
ﯬ
Na miongoni mwa takrima yao watakayoipata kwa Mola wao, na kukirimiana wao kwa wao, ni kuwa wao watakuwa kwenye vitanda wameelekeana.
Verse 45
ﯭﯮﯯﯰﯱ
ﯲ
Zinazungushwa kwao gilasi za Pombe inayotoka kwenye mito inayotembea, hawachelei kuwa itamalizika,
Verse 46
ﯳﯴﯵ
ﯶ
ni nyeupe rangi yake, ni tamu katika kuinywa,
Verse 47
haina madhara yoyote ya akili wala ya mwili.
Verse 48
ﯿﰀﰁﰂ
ﰃ
Na hapo kwao kwenye makao yao watakuwako wanawake waliojihifadhi, hawawatazami isipokuwa waume zao, wazuri wa macho,
Verse 49
ﰄﰅﰆ
ﰇ
kama kwamba wao ni mayai yaliyotunzwa ambayo hayajaguswa na mikono.
Verse 50
ﰈﰉﰊﰋﰌ
ﰍ
Hapo wataelekeana wakiulizana kuhusu hali zao za duniani na mambo ya usumbufu waliokuwa wakikutana nayo huko, na yale ambayo Mwenyezi Mungu Aliwaneemesha nayo Peponi. Na huku ndiko kuliwazika kuliotimia.
Verse 51
Atasema msemaji miongoni mwa watu wa Peponi, «Kwa kweli, nilikuwa na rafiki duniani aliyeshikana na mimi.
Verse 52
ﭑﭒﭓﭔ
ﭕ
«Aliyekuwa akisema, ‘Ni vipi wewe unaamini Ufufuzi ambao ni upeo wa kustaajabisha?
Verse 53
Je, tunapokufa, tukakatika vipande- vipande na tukawa mchanga na mifupa, kwani ni wenye kufufuliwa, kuhesabiwa na kulipwa kwa matendo yetu?’»
Verse 54
ﭞﭟﭠﭡ
ﭢ
Atasema huyu Muumini aliyetiwa Peponi akiwaambia wenzake, «Je, nyinyi ni wenye kuchungulia mpate kuona mwisho wa yule rafiki?»
Verse 55
ﭣﭤﭥﭦﭧ
ﭨ
Hapo akachungulia na akamuona rafiki yake katikati ya Moto.
Verse 56
ﭩﭪﭫﭬﭭ
ﭮ
Muumini atasema kumwambia rafiki yake mwenye kukanusha kufufuliwa, «Ulikaribia kuniangamiza kwa kunizuia nisiamini lau nilikutii.
Verse 57
ﭯﭰﭱﭲﭳﭴ
ﭵ
Na lau si wema wa Mola wangu kwa kuniongoza mimi kwenye Imani na kunithibitisha juu yake, ningalikuwa ni mwenye kuhudhurishwa kwenye adhabu pamoja na wewe.
Verse 58
ﭶﭷﭸ
ﭹ
«Je, ni kweli sisi ni wenye kukalishwa milele na kuneemeshwa, si wenye kufa
Verse 59
ﭺﭻﭼﭽﭾﭿ
ﮀ
isipokuwa kifo chetu cha mwanzo huko ulimwenguni, na sisi si wenye kuadhibiwa baada ya kuingia kwetu Peponi?
Verse 60
ﮁﮂﮃﮄﮅ
ﮆ
Hakika starehe hii tuliyo nayo ndiyo kufaulu kukubwa.
Verse 61
ﮇﮈﮉﮊ
ﮋ
«Basi kwa kupata mfano wa starehe hizi kamilifu, makazi ya daima na kufaulu kukubwa, na watende wenye kutenda duniani ili wazifikie huko Akhera.»
Verse 62
ﮌﮍﮎﮏﮐﮑ
ﮒ
Je, hayo yaliyotangulia kuelezwa ya starehe za Pepo ni makaribisho bora na vipewa vya Mwenyezi Mungu, au ni mti mbaya uliolaaniwa wa zaqqūm, ambao ni chakula cha watu wa Motoni?
Verse 63
ﮓﮔﮕﮖ
ﮗ
Sisi tumeufanya ni mtihani waliotahiniwa nao madhalimu kwa ukanushaji na kufanya mambo ya uasi na wakasema kwa njia ya kiburi, «Mtu wenu anawapa habari kwamba motoni kuna mti, na moto unakula miti.»
Verse 64
ﮘﮙﮚﮛﮜﮝ
ﮞ
Hakika huo ni mti ambao unaota kwenye uketo wa moto wa Jahanamu, matunda yake yana sura mbaya
Verse 65
ﮟﮠﮡﮢ
ﮣ
kama vichwa vya Mashetani.
Verse 66
ﮤﮥﮦﮧﮨﮩ
ﮪ
Basi yanapokuwa hivyo, usiulize baada ya haya kuhusu utamu wake. Kwani washirikina ni wenye kula kutoka mti huo na ni wenye kujaza matumbo yao kwa matunda hayo.
Verse 67
Kisha wao, baada ya kuyala ni wenye kunywa kinywaji mchanganyiko kilicho kibaya na kilicho moto.
Verse 68
ﯔﯕﯖﯗﯘ
ﯙ
Kisha marejeo yao baada ya adhabu hii ni kuishia (hukohuko) kwenye adhabu ya Moto.
Verse 69
ﯚﯛﯜﯝ
ﯞ
Hakika wao waliwakuta baba zao kwenye ushirikina na upotevu,
Verse 70
ﯟﯠﯡﯢ
ﯣ
na wakakimbilia kuwafuata katika hilo.
Verse 71
ﯤﯥﯦﯧﯨ
ﯩ
na kwa hakika, kabla ya watu wako, ewe Mtume, walipotea na kuwa kando na haki ummah wengi waliotangulia.
Verse 72
ﯪﯫﯬﯭ
ﯮ
Na kwa hakika, tuliwatumiliza kwa ummah hao Mitume waliowaonya adhabu, lakini wakakanusha.
Verse 73
ﯯﯰﯱﯲﯳ
ﯴ
Basi fikiria: ulikuwa vipi mwisho wa ummah hao walioonywa na wakakanusha? Waliadhibiwa na wakawa ni mazingatio kwa watu.
Verse 74
ﯵﯶﯷﯸ
ﯹ
Isipokuwa waja wa Mwenyezi Mungu Aliyowasafisha na Akawachagua kwa kuwapa rehema Yake kwa kule kumtakasa kwao Yeye.
Verse 75
ﯺﯻﯼﯽﯾ
ﯿ
Na kwa hakika Alituita kwa kutuomba Nabii wetu Nūḥ tumlinde na watu wake, basi bora wa wenye kumuitikia tulikuwa ni sisi.
Verse 76
ﰀﰁﰂﰃﰄ
ﰅ
Na tukamuokoa yeye na watu wa nyumbani kwake na Waumini pamoja naye kutokana na maudhi ya washirikina na kutokana na kuzamishwa kwa mafuriko makubwa.
Verse 77
ﭑﭒﭓﭔ
ﭕ
Na tukawafanya watoto wa Nūḥ ndio wenye kusalia baada ya kuzamishwa watu wake.
Verse 78
ﭖﭗﭘﭙ
ﭚ
Na tukamuwekea utajo mwema na sifa nzuri kwa watu waliokuja baada yake wakawa wanamtaja nazo.
Verse 79
ﭛﭜﭝﭞﭟ
ﭠ
Amani imfikie Nūḥ na asalimike na kutajwa kwa ubaya katika kipindi cha watu wa mwisho, bali asifiwe na watu wa vizazi vinavyokuja baada yake.
Verse 80
ﭡﭢﭣﭤ
ﭥ
Mfano wa malipo mema tuliomlipa Nūḥ, tutamlipa kila aliyefanya vizuri, miongoni mwa waja, katika kumtii Mwenyezi Mungu.
Verse 81
ﭦﭧﭨﭩ
ﭪ
Hakika Nūḥ ni miongoni mwa waja wetu wenye kuamini, wenye kumtakasia Mwenyezi Mungu na wenye kufuata amri za Mwenyezi Mungu kivitendo.
Verse 82
ﭫﭬﭭ
ﭮ
Kisha tukawazamisha wengine, wenye kukanusha kati ya watu wake, kwa mafuriko, kisisalie chochote, miongoni mwao, hata jicho lenye kupepesa.
Verse 83
ﭯﭰﭱﭲﭳ
ﭴ
Na miongoni mwa waliokuwa katika nyendo za Nūḥ, njia yake na mila yake ni Nabii wa Mwenyezi Mungu Ibrāhīm,
Verse 84
ﭵﭶﭷﭸﭹ
ﭺ
alipomjia Mola wake kwa moyo uliyojitenga na kila itikadi ya ubatilifu na tabia ya kujitukanisha,
Verse 85
ﭻﭼﭽﭾﭿﮀ
ﮁ
alipomwambia babake na watu wake kwa njia ya kuwakanya, «Ni kitu gani hiko mnachokiabudu badala ya Mwenyezi Mungu?
Verse 86
ﮂﮃﮄﮅﮆ
ﮇ
Je, mnataka kuabudu waungu wa kuzuliwa na mnaacha kumuabudu Mwenyezi Mungu Anayestahiki kuabudiwa Peke Yake?
Verse 87
ﮈﮉﮊﮋ
ﮌ
Mnamdhani Mola wa viumbe vyote Atawafanya nini mkimshirikisha Yeye na mkamuabudu asiyekuwa Yeye?
Verse 88
ﮍﮎﮏﮐ
ﮑ
Akatazama mtazamo mmoja kwenye nyota kulingana na mila ya watu wake kuhusu hilo, huku akifikiria udhuru wa kuutoa ili asipate kutoka na wao kwenda kwenye sherehe zao,
Verse 89
ﮒﮓﮔ
ﮕ
akawaambia, «Mimi ni mgonjwa.» Hii ilikuwa ni ishara ya mbali kutoka kwake.
Verse 90
ﮖﮗﮘ
ﮙ
Basi wakamuacha nyuma yao.
Verse 91
ﮚﮛﮜﮝﮞﮟ
ﮠ
Akabeta kwa haraka kuelekea kwenye masanamu wa watu wake, akasema kwa njia ya kuwakejeli, «Si mkile chakula hiki ambacho washika mlango wenu wanawapatia?
Verse 92
ﮡﮢﮣﮤ
ﮥ
Muna nini nyinyi mbona hamsemi wala hamumjibu mwenye kuwaomba?
Verse 93
ﮦﮧﮨﮩ
ﮪ
Akawaelekea waungu wao kuwapiga na kuwavunja-vunja kwa mkono wake wa kulia, ili kuwathibitishia makosa ya kuwaabudu.
Verse 94
ﮫﮬﮭ
ﮮ
Wakaja kumkabili kwa haraka na mbio huku wana hasira.
Verse 95
ﮯﮰﮱﯓ
ﯔ
Ibrāhīm akakutana na wao akiwa imara kwa kusema, «Vipi mtaabudu masanamu mnaowachonga nyinyi wenyewe na mnaowatengeneza kwa mikono yenu,
Verse 96
ﯕﯖﯗﯘ
ﯙ
na mnaacha kumuabudu Mola wenu Aliyewaumba nyinyi na Akayaumba matendo yenu?»
Verse 97
Hoja ilipowasimamia, waliamua kutumia nguvu na wakasema, «Jengeni jengo kwa ajili yake, mlijaze kuni kisha mumtupe ndani yake»
Verse 98
ﯢﯣﯤﯥﯦ
ﯧ
Watu wa Ibrāhīm wakataka kumfanyia vitimbi ili wamuangamize, tukawafanya wao kuwa ndio wenye kutendeshwa nguvu na kushindwa. Mwenyezi Mungu Akavirudisha vitimbi vyao kwenye shingo zao na akaufanya ule moto uwe baridi na salama kwa Ibrāhīm.
Verse 99
ﯨﯩﯪﯫﯬﯭ
ﯮ
Akasema Ibrāhīm, «Mimi nahamia kwa Mola wangu kutoka kwenye mji wa watu wangu kuelekea pale ambapo nitamakinika kumuabudu Mola wangu, kwani Yeye Atanielekeza kwenye kheri ya Dini yangu na dunia yangu.
Verse 100
ﯯﯰﯱﯲﯳ
ﯴ
Mola wangu! Nipe mtoto mwema.»
Verse 101
ﯵﯶﯷ
ﯸ
Tukamkubalia ombi lake na tukambashiria kuwa atapata mtoto wa kiume atakayekuwa mpole ukubwani mwake, naye ni Ismā'īl.
Verse 102
Alipokuwa mkubwa Ismā'īl, akawa anatembea na babake, babake alimwambia, «Mimi nimeona usingizini kuwa ninakuchinja, je, una maoni gani?» (na ndoto za Manabii ni za kweli). Ismā'īl akasema, kwa kumridhisha Mola wake, kumtii mzazi wake na kumsaidia juu ya utiifu wa Mwenyezi Mungu, «Endelea katika jambo Alilokuamrisha Mwenyezi Mungu la kunichinja mimi. Utanikuta, Mwenyezi Mungu Akitaka, ni mvumilivu, mtiifu na ni mwenye kutarajia malipo mema (kutoka kwa Mwenyezi Mungu)».
Verse 103
ﭑﭒﭓﭔ
ﭕ
Walipojisalimisha wao wawili kwa kuifuata amri ya Mwenyezi Mungu na kuiandama, na Ibrāhīm akambwaga Ismā'īl chini, kwa upande wa paji la uso, ili kumchinja.
Verse 104
ﭖﭗﭘ
ﭙ
Na tukamuita Ibrāhīm katika hali hiyo ngumu kwamba: Ewe Ibrāhīm! Umeshalifanya uliloamrishwa na, kwa hivyo,
Verse 105
umeisadikisha ndoto yako. Hakika yetu sisi kama vile tulivyokulipa mema kwa kuamini kwako , ndivyo tunavyowalipa wale waliofanya wema mfano wako, tuwaepushie shida duniani na Akhera.
Verse 106
ﭣﭤﭥﭦﭧ
ﭨ
Hakika amri ya kuwa wewe umuue mwano ndio mtihani mgumu uliodhihirisha ukweli wa Imani yako.
Verse 107
ﭩﭪﭫ
ﭬ
Na tukamuokoa Ismā'īl, na tukamuekea kondoo mkubwa kuwa ni badala yake.
Verse 108
ﭭﭮﭯﭰ
ﭱ
Na tukambakishia Ibrāhīm baada yake sifa njema kwa watu.
Verse 109
ﭲﭳﭴ
ﭵ
Maamkizi kwa Ibrāhīm kutoka kwa Mola wake na kumuombea asalimike na kila dhara.
Verse 110
ﭶﭷﭸ
ﭹ
Kama tulivyomlipa malipo mema Ibrāhīm kwa utiifu wake kwetu na kufuata kwake amri yetu, ndivyo tutakavyowalipa wenye kufanya wema miongoni mwa waja wetu.
Verse 111
ﭺﭻﭼﭽ
ﭾ
Hakika yeye ni miongoni mwa waja wetu Waumini waliyoipa hiyo sifa ya uja haki yake.
Verse 112
ﭿﮀﮁﮂﮃ
ﮄ
Na tukampa bishara Ibrāhīm ya mtoto wake, Isḥāq, kuwa atakuwa Nabii, miongoni mwa watu wema. Hayo yakiwa ni malipo ya uvumilivu wake na kuridhika kwake na amri ya Mola wake na utiifu wake Kwake.
Verse 113
Na tukawateremshia baraka. Na miongoni mwa wale wanaotokana na kizazi chao kuna anayemtii Mola wake, anayeifanyia wema nafsi yake, na kuna anayeidhulumu (nafsi yake) dhulma iliyo wazi kwa ukafiri wake na utendaji wake maasia.
Verse 114
ﮑﮒﮓﮔﮕ
ﮖ
Na kwa hakika tuliwafanyia wema Mūsā na Hārūn kwa kuwapa unabii na utume.
Verse 115
ﮗﮘﮙﮚﮛ
ﮜ
Na tukawaokoa wao wawili na watu wao kutokana na gharika, utumwa na unyonge waliokuwa nao.
Verse 116
ﮝﮞﮟﮠ
ﮡ
Na tukawanusuru, wakawa na enzi, usaidizi na ushindi juu ya Fir'awn na jamaa zake.
Verse 117
ﮢﮣﮤ
ﮥ
Na tukawapa wao wawili Taurati yenye ufafanuzi,
Verse 118
ﮦﮧﮨ
ﮩ
na tukawaongoza njia iliyonyoka isiyokuwa na upotovu, nayo ni Uislamu, Dini ya Mwenyezi Mungu ambayo Amewatumiliza Manabii Wake kwayo,
Verse 119
ﮪﮫﮬﮭ
ﮮ
na tukazifanya sifa zao nzuri na utajo wao mwema ni vyenye kusalia baada yao.
Verse 120
ﮯﮰﮱﯓ
ﯔ
Maamkizi kwa Mūsā na Hārūn kutoka kwa Mwenyezi Mungu, na sifa njema na kuwaombea wao wasalimike na kila dhara.
Verse 121
ﯕﯖﯗﯘ
ﯙ
Kama tulivyowalipa wao malipo mema , ndivyo tutakavyowalipa wenye kufanya wema miongoni mwa waja wetu wenye kututakasia kwa ukweli, kuamini na kutenda.
Verse 122
ﯚﯛﯜﯝ
ﯞ
Hakika ya wao wawili ni miongoni mwa waja wetu waliojikita katika Imani.
Verse 123
ﯟﯠﯡﯢ
ﯣ
Na hakika mja wetu Ilyas ni miongoni mwa wale ambao tuliwakirimu kwa unabii na utume.
Verse 124
ﯤﯥﯦﯧﯨ
ﯩ
Kumbuka na utaja pindi aliposema kuwaambia watu wake, kati ya Wana wa Isrāīl, «Mcheni Mwenyezi Mungu, Peke Yake, na mumuogope, na msimshirikishe mwengine pamoja na Yeye.
Verse 125
ﯪﯫﯬﯭﯮ
ﯯ
Vipi nyinyi mtaliabudu sanamu ambalo ni kiumbe dhaifu na mtamuacha Mzuri wa kuumba, Mwenye sifa nzuri na kamilifu kabisa,
Verse 126
ﯰﯱﯲﯳﯴ
ﯵ
mkawa hamtamuabudu Mwenyezi Mungu Ambaye ni Mola wenu Aliyewaumba nyinyi na Akawaumba baba zenu waliopita kabla yenu?»
Verse 127
ﭑﭒﭓ
ﭔ
Watu wa Ilyas walimkanusha Nabii wao. Basi Mwenyezi Mungu , kwa hakika, Atawakusanya Siku ya Kiyama ili wahesabiwe na wateswe.
Verse 128
ﭕﭖﭗﭘ
ﭙ
Isipokuwa wale waja wa Mwenyezi Mungu waliomtakasia Mwenyezi Mungu Dini yao, basi hao ni wenye kuokoka na adhabu Yake.
Verse 129
ﭚﭛﭜﭝ
ﭞ
Tulimfanya Ilyas awe na sifa nzuri kwa ummah waliokuja baada yake.
Verse 130
ﭟﭠﭡﭢ
ﭣ
Maamkizi kutoka kwa Mwenyezi Mungu na sifa njema kwa Ilyas.
Verse 131
ﭤﭥﭦﭧ
ﭨ
Na kama tulivyomlipa Ilyas malipo mema kwa utiifu wake, ndivyo tutakavyowalipa walio wema miongoni mwa waja wetu Waumini.
Verse 132
ﭩﭪﭫﭬ
ﭭ
Hakika yake yeye ni miongoni mwa waja wa Mwenyezi Mungu waliomtakasia wenye kufuata amri zake kivitendo.
Verse 133
ﭮﭯﭰﭱ
ﭲ
Na hakika mja wetu Lūṭ tulimchagua na tukamfanya ni miongoni mwa Mitume.
Verse 134
ﭳﭴﭵﭶ
ﭷ
Tulipomuokoa yeye na watu wa nyumbani kwake wote,
Verse 135
ﭸﭹﭺﭻ
ﭼ
isipokuwa mkongwe aliyezeeka, naye ni mke wake, ambaye aliangamia pamoja na wale walioangamia miongoni mwa watu wake kwa ukafiri wake.
Verse 136
ﭽﭾﭿ
ﮀ
Kisha tukawaangamiza wakanushaji waliosalia miongoni mwa watu wake.
Verse 137
ﮁﮂﮃﮄ
ﮅ
Na hakika yenu nyinyi, enyi watu wa Makkah mnazipitia katika safari zenu nyumba za watu wa Lūṭ na athari zao katika kipindi cha asubuhi,
Verse 138
ﮆﮇﮈﮉ
ﮊ
na pia mnazipitia katika kipindi cha usiku. Basi hamtii akilini, mkaogopa kisije kikawafika nyinyi kile kilichowafika wao?
Verse 139
ﮋﮌﮍﮎ
ﮏ
Hakika mja wetu Yūnus, tulimchagua na tukamfanya ni miongoni mwa Mitume.
Verse 140
ﮐﮑﮒﮓﮔ
ﮕ
Alipokimbia kutoka mji wake, akiwa na hasira juu ya watu wake, akapanda jahazi iliyojaa abiria na vyombo.
Verse 141
ﮖﮗﮘﮙ
ﮚ
Mawimbi makubwa yakaizunguka jahazi hiyo kila upande. Na watu waliokuwa wamepanda jahazi wakapiga kura ili kupunguza shehena ili wasizame. Yūnus akawa ni miongoni mwa wale walioshindwa kwa kura.
Verse 142
ﮛﮜﮝﮞ
ﮟ
Hivyo basi akatupwa baharini na chewa akammeza, na hali ni kwamba Yūnus, amani imshukie, ameleta jambo la kumfanya alaumiwe.
Verse 143
ﮠﮡﮢﮣﮤ
ﮥ
Lau si yale yaliyotangulia kwake, ya wingi wa Ibada na matendo mema kabla ya kuingia ndani ya tumbo la chewa kwa kusema, «Hapana Mola anayepasa kuabudiwa kwa haki isipokuwa wewe, kutakasika na sifa za upungufu ni kwako, mimi nimekuwa miongoni mwa wenye kudhulumu,»
Verse 144
ﮦﮧﮨﮩﮪﮫ
ﮬ
angalikaa ndani ya tumbo la chewa, na lingalikuwa ni kaburi lake mpaka Siku ya Kiyama.
Verse 145
ﮭﮮﮯﮰﮱ
ﯓ
Tukamtoa kwenye tumbo la chewa na tukamtupa kwenye ardhi tupu, isiyokuwa na miti wala majengo, akiwa dhaifu wa mwili.
Verse 146
ﯔﯕﯖﯗﯘ
ﯙ
Na tukamuoteshea mmea wa matango ili umfinike na anufaike nao.
Verse 147
ﯚﯛﯜﯝﯞﯟ
ﯠ
Tukamtumiliza aende kwa watu wake wanaofikia elfu mia moja, bali wanazidi idadi hiyo.
Verse 148
ﯡﯢﯣﯤ
ﯥ
Wakamuamini na wakafuata aliyokuja nayo kivitendo, na kwa hivyo tukawastarehesha maishani mwao mpaka wakati wa kufika ajali zao.
Verse 149
ﯦﯧﯨﯩﯪ
ﯫ
Basi waulize watu wako, ewe Mtume, «Ni vipi wamemfanya Mwenyezi Mungu ana watoto wa kike ambao wao wenyewe wanawachukia, na wao wana watoto wa kiume wanaowataka?»
Verse 150
ﯬﯭﯮﯯﯰﯱ
ﯲ
Na waulize wao, «Je, tuliwaumba Malaika wakiwa wanawake, na hali wao wapo (wakishuhudia uumbaji huo)?»
Verse 151
ﯳﯴﯵﯶﯷ
ﯸ
Na miongoni mwa urongo wao ni kule kusema kwao, «Mwenyezi Mungu Amezaa!
Verse 152
ﯹﯺﯻﯼ
ﯽ
Na kwa hakika, wao ni warongo, kwa kuwa wanakisema wasichokijua.»
Verse 153
ﯾﯿﰀﰁ
ﰂ
Ni kwa kitu gani Mwenyezi Mungu Achague watoto wa kike na sio wa kiume?
Verse 154
ﭑﭒﭓﭔ
ﭕ
Ni uamuzi mbaya sana mnaoutoa, enyi watu, wa kuwa Mwenyezi Mungu Ana watoto wa kike na nyinyi mna watoto wa kiume, na hali nyinyi hamridhiki nafsi zenu kuwa na watoto wa kike.
Verse 155
ﭖﭗ
ﭘ
Je, hamkumbuki kwamba haifai wala haitakikani Awe na mtoto? Ametukuka Mwenyezi Mungu na kuwa mbali na hilo, umbali ulio juu sana.
Verse 156
ﭙﭚﭛﭜ
ﭝ
Lakini je, mna hoja ya wazi juu ya hilo neno lenu na uzushi wenu?
Verse 157
ﭞﭟﭠﭡﭢ
ﭣ
Iwapo mna hoja ndani ya kitabu kitokacho kwa Mwenyezi Mungu, basi kileteni, mkiwa ni wa kweli katika hilo neno lenu.
Verse 158
Na washirikina walifanya kuwa kuna uhusiano wa kizazi baina ya Mwenyezi Mungu na Malaika, na hakika ni kwamba Malaika washajua kuwa washirikina ni wenye kuletwa Siku ya Kiyama ili kuadhibiwa.
Verse 159
ﭰﭱﭲﭳ
ﭴ
Ametakasika Mwenyezi Mungu na kila lisilofaa asifike nalo miongoni mwa yale wanaomsifu nayo washirikina.
Verse 160
ﭵﭶﭷﭸ
ﭹ
Lakini wale waja wa Mwenyezi Mungu wanaomtakasia katika kumuabudu hawamsifu isipokuwa kwa sifa zinazolingana na utukufu Wake, kutakasika ni Kwake.
Verse 161
ﭺﭻﭼ
ﭽ
Hakika yenu nyinyi, enyi wenye kumshirikisha Mwenyezi Mungu, na kile mnachokiabudu badala ya Mwenyezi Mungu miongoni mwa waungu,
Verse 162
ﭾﭿﮀﮁ
ﮂ
hamkuwa ni wenye kumpoteza yoyote
Verse 163
ﮃﮄﮅﮆﮇ
ﮈ
isipokuwa yule Aliyemkadiria Mwenyezi Mungu aingie kwenye Moto wa Jaḥīm kwa sababu ya ukafiri wake na udhalimu wake.
Verse 164
ﮉﮊﮋﮌﮍﮎ
ﮏ
Malaika wanasema, «Hakuna yoyote miongoni mwetu isipokuwa ana makao maalumu mbinguni.
Verse 165
ﮐﮑﮒ
ﮓ
Na sisi ndio tunaosimama kwa kujipanga kwa safu katika kumuabudu Mwenyezi Mungu na kumtii.
Verse 166
ﮔﮕﮖ
ﮗ
Na sisi ndio tunaomtakasa Mwenyezi Mungu na kila kisichofaa kunasibishwa nacho.»
Verse 167
ﮘﮙﮚ
ﮛ
Na hakika makafiri wa Makkah walikuwa wakisema kabla hujatumilizwa,
Verse 168
ﮜﮝﮞﮟﮠﮡ
ﮢ
«Ewe Mtume! Lau vingalitujia vitabu na Manabii vile vilivyowajia wa mwanzo kabla yetu,
Verse 169
ﮣﮤﮥﮦ
ﮧ
tungalikuwa waja wa Mwenyezi Mungu wakweli katika Imani, waliotakaswa kwa kufanya Ibada.»
Verse 170
ﮨﮩﮪﮫﮬ
ﮭ
Ulipowajia wao utajo wa watu wa mwanzo na utajo wa watu wa mwisho na kitabu kikamilifu kabisa na bora wa Mitume, naye ni Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, walimkanusha. Basi wataijua adhabu watakayopatiwa Siku ya Mwisho.
Verse 171
ﮮﮯﮰﮱﯓ
ﯔ
Kwa hakika lishatangulia neno letu, ambalo halina namna ya kurudi, la kuwaahidi waja wetu waliopewa utume
Verse 172
ﯕﯖﯗ
ﯘ
kwamba watapata usaidizi juu ya maadui zao, kwa hoja na nguvu,
Verse 173
ﯙﯚﯛﯜ
ﯝ
na kwamba askari wetu wanaopigana jihadi katika njia yetu ndio wenye kuwashinda maadui zao kila mahali, kuzingatia mwishoni na marejeo.
Verse 174
ﯞﯟﯠﯡ
ﯢ
Basi wape mgongo, ewe Mtume, wale walioshindana na wasiikubali haki mpaka ukamalizika muda waliopatiwa muhula na ikaja amri ya Mwenyezi Mungu ya wao kuadhibiwa,
Verse 175
ﯣﯤﯥ
ﯦ
wangojee na subiri uone: ni adhabu gani itakayowashukia wao kwa kuenda kinyume nawe? Basi wataiona adhabu ya Mwenyezi Mungu itakayowashukia.
Verse 176
ﯧﯨ
ﯩ
Je kuteremkiwa kwao na adhabu yetu ndilo jambo wanalokuharakishia, ewe Mtume?
Verse 177
ﯪﯫﯬﯭﯮﯯ
ﯰ
Basi adhabu yetu itakapowashukia, asubuhi mbaya zaidi ni asubuhi yao!
Verse 178
ﯱﯲﯳﯴ
ﯵ
Na uwape mgongo mpaka Mwenyezi Mungu Atoe idhini ya wao kuadhibiwa.
Verse 179
ﯶﯷﯸ
ﯹ
Na uwangojee, kwani wataiona adhabu itakayowashukia na mateso.
Verse 180
ﯺﯻﯼﯽﯾﯿ
ﰀ
Mola wa enzi na utukufu Ameepukana na kuwa juu ya kila kile ambacho wanaomzulia urongo wanamsifu nacho.
Verse 181
ﰁﰂﰃ
ﰄ
Na maamkizi ya Mwenyezi Mungu ya daima,sifa Zake na amani Yake ziwafikie Mitume wote.
Verse 182
ﰅﰆﰇﰈ
ﰉ
Na shukrani na sifa njema ni za Mola wa viumbe wote ulimwenguni na Akhera. Yeye Ndiye Mstahiki wa hilo Peke Yake, Hana mshirika Wake.
تقدم القراءة