Tafsiri ya Sura An-Naba'i kwa السواحلية kutoka الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس
Verse 1
ﭑﭒ
ﭓ
Kuhusu kitu gani baadhi ya makafiri wa Kikureshi wanaulizana?
Verse 2
ﭔﭕﭖ
ﭗ
Wanaulizana kuhusu habari iliyo na uzito mkubwa kabisa,
Verse 3
ﭘﭙﭚﭛ
ﭜ
nayo ni Qur’ani tukufu inayotoa habari za kufufuliwa ambako makafiri wa Kikureshi wana shaka nako na wanakukanusha.
Verse 4
ﭝﭞ
ﭟ
Mambo sivyo kama wanavyodhania hawa washirikina. Hapo watajua hawa washirikina upeo wa kukanusha kwao na kitawadhihirikia waziwazi kile Atakachowatenda Mwenyezi Mungu Siku ya Kiyama.
Verse 5
ﭠﭡﭢ
ﭣ
Kisha litahakikishika kwao jambo hilo na utahakikishika kwao ukweli wa yale aliyokuja nayo Mtume Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, kuhusu Qur’ani na kufufuliwa. Huu ni utisho na makemeo kwao.
Verse 6
ﭤﭥﭦﭧ
ﭨ
Kwani hatukuwatandazia ardhi kama tandiko?
Verse 7
ﭩﭪ
ﭫ
Na Tukawafanyia majabali kuwa ni vigingi, ili isitisike nanyi?
Verse 8
ﭬﭭ
ﭮ
Na Tukawaumba aina mbali-mbali, mume na mke.
Verse 9
ﭯﭰﭱ
ﭲ
Na Tukafanya usingizi wenu ni mapumziko kwa viwiliwili vyenu: ndani yake mnatulia na kupumzika?
Verse 10
ﭳﭴﭵ
ﭶ
Na Tukaufanya usiku kuwa ni vazi, unawavisha giza lake na kuwafinika, kama nguo inavyomsitiri mwenye kuivaa.
Verse 11
ﭷﭸﭹ
ﭺ
Na Tukaufanya mchana ni kipindi cha kutafuta maisha, mnaenea humo kwa ajili ya maisha yenu na mnatembea humo kwa ajili ya maslahi yenu?
Verse 12
ﭻﭼﭽﭾ
ﭿ
Na Tukajenga juu yenu mbingu saba, madhubuti jengo lake, lilioumbwa kwa uzuri, halina mapasuko wala nyufa?
Verse 13
ﮀﮁﮂ
ﮃ
Na Tukalifanya jua kuwa ni taa iwakayo na kung’ara?
Verse 14
ﮄﮅﮆﮇﮈ
ﮉ
Na Tukateremsha kutoka kwenye mawingu yanyeshayo maji yamiminikayo kwa wingi,
Verse 15
ﮊﮋﮌﮍ
ﮎ
ili Tutoe kwa maji hayo nafaka inayoliwa na watu,
Verse 16
ﮏﮐ
ﮑ
nyasi zinazoliwa na wanyama na miti iliyosongamana kwa kutawanyika tagaa zake?
Verse 17
ﮒﮓﮔﮕﮖ
ﮗ
Hakika Siku ya Uamuzi kati ya viumbe,
Verse 18
ﮘﮙﮚﮛﮜﮝ
ﮞ
nayo ni Siku ya Kiyama, imekuwa ni wakati na ahadi iliyowekewa muda maalimu kwa watu wa mwanzo na wa mwisho.
Verse 19
ﮟﮠﮡﮢ
ﮣ
Na zikafunguliwa mbingu zikawa ni zenye milango mingi kwa ajili ya kuteremka Malaika.
Verse 20
ﮤﮥﮦﮧ
ﮨ
Na yakalipuliwa majabali baada ya kuwa yamekita, yakawa ni kama mangati.
Verse 21
ﮩﮪﮫﮬ
ﮭ
Hakika Jahanamu, Siku Hiyo, itawalindiza wenye ukafiri ambao Moto huo umeandaliwa wao.
Verse 22
ﮮﮯ
ﮰ
Kwa makafiri ndio marejeo.
Verse 23
ﮱﯓﯔ
ﯕ
Watabakia humo muda mrefu ufuatanao, usiokoma.
Verse 24
ﯖﯗﯘﯙﯚﯛ
ﯜ
Hawatakula humo chochote kitakachozizimisha joto la moto kwao.
Verse 25
ﯝﯞﯟ
ﯠ
Wala kinywaji kitakachowaondolea kiu yao. Isipokuwa maji moto na usaha wa watu wa motoni.
Verse 26
ﯡﯢ
ﯣ
Watakuwa wanalipwa kwa hilo malipo ya sawa yanayolingana na vitendo vyao walivyovitenda duniani
Verse 27
ﯤﯥﯦﯧﯨ
ﯩ
Hakika wao walikuwa hawaiyogopi Siku ya Hesabu, na kwa hivyo hawakujitayarisha nayo kwa kufanya matendo ya kuwafaa.
Verse 28
ﯪﯫﯬ
ﯭ
Na waliyakanusha waziwazi yaliyoletwa na Mitume.
Verse 29
ﯮﯯﯰﯱ
ﯲ
Na kila kitu Tulikijua na Tukakiandika katika Ubao uliohifadhiwa (Al-Lawḥ Al-Maḥfūd).
Verse 30
ﯳﯴﯵﯶﯷ
ﯸ
Basi Onjeni, enyi makafiri, hayo yakiwa ni malipo ya vitendo vyenu, Hatutawazidishia isipokuwa adhabu juu ya adhabu yenu.
Verse 31
ﭑﭒﭓ
ﭔ
Hakika kwa wale ambao wanamuogopa Mola wao na huku wanatenda mema kuna kufaulu kwa kuingia Peponi.
Verse 32
ﭕﭖ
ﭗ
Hakika watapata Mabustani makubwa na zabibu.
Verse 33
ﭘﭙ
ﭚ
Na watapata wanawake wenye umri mdogo, wenye vifua vilivyojaza, marika na waume zao.
Verse 34
ﭛﭜ
ﭝ
Na watapata glasi zlizojaa pombe.
Verse 35
ﭞﭟﭠﭡﭢﭣ
ﭤ
Hawatasikia katika Pepo hiyo maneno ya upotofu wala kudanganyana.
Verse 36
ﭥﭦﭧﭨﭩ
ﭪ
Watayapata yote hayo yakiwa ni malipo na zawadi na kipewa kingi cha kuwatosha kutoka kwa Mwenyezi Mungu,
Verse 37
Mola wa mbingu na ardhi na vilivyomo kati ya hizo, Mwenye kuwarehemu duniani na Akhera. Hawataweza kumuomba isipokuwa kile walichopewa ruhusa kumuomba.
Verse 38
Siku atakaposimama Jibrili na Malaika wengine hali ya kujipanga mlolongo. Hawatamuombea isipokuwa yule aliyetolewa ruhusa na Mwingi wa Rehema ya kuombewa na akasema maneno ya haki na ya sawa.
Verse 39
Hiyo ndiyo siku ya haki isiyokuwa na shaka kuja kwake. Kwa hivyo, yule atakaye kuokoka na vituko vya Siku hiyo, na ajifanyie njia ya marejeo kwa Mola wake kutenda vitendo vyema.
Verse 40
Sisi Tunawaonya nyinyi adhabu ya Siku ya mwisho iliyo karibu. Siku ambayo atayaona kila mtu aliyoyatenda katika kheri au aliyoyachuma miongoni mwa madhambi. Na kafiri atasema, kwa kitisho cha Hesabu, «Laiti mimi nilikuwa mchanga na sikufufuliwa.»
تقدم القراءة