Tafsiri ya Sura An-Naba'i kwa السواحلية kutoka Ali Muhsin Al - Swahili translation
Verse 1
ﭑﭒ
ﭓ
An-Naba'i
WANAULIZANA nini?
Verse 2
ﭔﭕﭖ
ﭗ
Ile khabari kuu,
Verse 3
ﭘﭙﭚﭛ
ﭜ
Ambayo kwayo wanakhitalifiana.
Verse 4
ﭝﭞ
ﭟ
La! Karibu watakuja jua.
Verse 5
ﭠﭡﭢ
ﭣ
Tena la! Karibu watakuja jua.
Verse 6
ﭤﭥﭦﭧ
ﭨ
Kwani hatukuifanya ardhi kama tandiko?
Verse 7
ﭩﭪ
ﭫ
Na milima kama vigingi?
Verse 8
ﭬﭭ
ﭮ
Na tukakuumbeni kwa jozi?
Verse 9
ﭯﭰﭱ
ﭲ
Na tukakufanya kulala kwenu ni mapumziko?
Verse 10
ﭳﭴﭵ
ﭶ
Na tukaufanya usiku ni nguo?
Verse 11
ﭷﭸﭹ
ﭺ
Na tukaufanya mchana ni wa kuchumia maisha?
Verse 12
ﭻﭼﭽﭾ
ﭿ
Na tukajenga juu yenu saba zenye nguvu?
Verse 13
ﮀﮁﮂ
ﮃ
Na tukaifanya taa yenye mwanga na joto;
Verse 14
ﮄﮅﮆﮇﮈ
ﮉ
Na tukateremsha maji yanayo anguka kwa kasi kutoka mawinguni,
Verse 15
ﮊﮋﮌﮍ
ﮎ
Ili tutoe kwayo nafaka na mimea,
Verse 16
ﮏﮐ
ﮑ
Na mabustani yenye miti iliyo kamatana.
Verse 17
ﮒﮓﮔﮕﮖ
ﮗ
Hakika siku ya uamuzi imewekewa wakati wake,
Verse 18
ﮘﮙﮚﮛﮜﮝ
ﮞ
Siku litapo pulizwa barugumu, nanyi mtakuja kwa makundi,
Verse 19
ﮟﮠﮡﮢ
ﮣ
Na mbingu zitafunguliwa, ziwe milango,
Verse 20
ﮤﮥﮦﮧ
ﮨ
Na milima itaondolewa na itakuwa kama sarabi.
Verse 21
ﮩﮪﮫﮬ
ﮭ
Hakika Jahannamu inangojea!
Verse 22
ﮮﮯ
ﮰ
Kwa walio asi ndio makaazi yao,
Verse 23
ﮱﯓﯔ
ﯕ
Wakae humo karne baada ya karne,
Verse 24
ﯖﯗﯘﯙﯚﯛ
ﯜ
Hawataonja humo chochote kibaridi wala kinywaji,
Verse 25
ﯝﯞﯟ
ﯠ
Ila maji yamoto sana na usaha,
Verse 26
ﯡﯢ
ﯣ
Ndio jaza muwafaka.
Verse 27
ﯤﯥﯦﯧﯨ
ﯩ
Hakika hao hawakuwa wakitaraji kuwa kuna hisabu.
Verse 28
ﯪﯫﯬ
ﯭ
Na wakikanusha Aya zetu kwa nguvu.
Verse 29
ﯮﯯﯰﯱ
ﯲ
Na kila kitu Sisi tumekidhibiti kwa kukiandika.
Verse 30
ﯳﯴﯵﯶﯷ
ﯸ
Basi onjeni! Nasi hatutakuzidishieni ila adhabu!
Verse 31
ﭑﭒﭓ
ﭔ
Hakika wachamngu wanastahiki kufuzu,
Verse 32
ﭕﭖ
ﭗ
Mabustani na mizabibu,
Verse 33
ﭘﭙ
ﭚ
Na wake walio lingana nao,
Verse 34
ﭛﭜ
ﭝ
Na bilauri zilizo jaa,
Verse 35
ﭞﭟﭠﭡﭢﭣ
ﭤ
Hawatasikia humo upuuzi wala uwongo -
Verse 36
ﭥﭦﭧﭨﭩ
ﭪ
Malipo kutoka kwa Mola wako Mlezi, kipawa cha kutosha.
Verse 37
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilio baina yao, Arrahman, Mwingi wa rehema; hawamiliki usemi mbele yake!
Verse 38
Siku atakapo simama Roho na Malaika kwa safu. Hawatasema ila Mwingi wa rehema aliye mruhusu, na atasema yaliyo sawa tu.
Verse 39
Hiyo ndiyo Siku ya haki. Basi anaye taka na ashike njia arejee kwa Mola wake Mlezi.
Verse 40
Hakika tumekuhadharisheni adhabu iliyo karibu kufika; Siku ambayo mtu atakapo ona yaliyo tangulizwa na mikono yake; na kafiri atasema: Laiti ningeli kuwa udongo!
تقدم القراءة