Tafsiri ya Sura Al-Mursalat kwa السواحلية kutoka Ali Muhsin Al - Swahili translation
Verse 1
ﮑﮒ
ﮓ
Al-Mursalat
Naapa kwa zinazo tumwa kwa upole!
Verse 2
ﮔﮕ
ﮖ
Na zinazo vuma kwa kasi!
Verse 3
ﮗﮘ
ﮙ
Na zikaeneza maeneo yote!
Verse 4
ﮚﮛ
ﮜ
Na zinazo farikisha zikatawanya!
Verse 5
ﮝﮞ
ﮟ
Na zinazo peleka mawaidha!
Verse 6
ﮠﮡﮢ
ﮣ
Kwa kuudhuru au kuonya,
Verse 7
ﮤﮥﮦ
ﮧ
Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka yatakuwa!
Verse 8
ﮨﮩﮪ
ﮫ
Wakati nyota zitakapo futwa,
Verse 9
ﮬﮭﮮ
ﮯ
Na mbingu zitakapo pasuliwa,
Verse 10
ﮰﮱﯓ
ﯔ
Na milima itakapo peperushwa,
Verse 11
ﯕﯖﯗ
ﯘ
Na Mitume watakapo wekewa wakati wao,
Verse 12
ﯙﯚﯛ
ﯜ
Kwa siku gani hiyo wamewekewa muda huo?
Verse 13
ﯝﯞ
ﯟ
Kwa siku ya kupambanua!
Verse 14
ﯠﯡﯢﯣﯤ
ﯥ
Na nini kitakacho kujuulisha siku ya kupambanua ni nini?
Verse 15
ﯦﯧﯨ
ﯩ
Ole wao, siku hiyo hao wanao kanusha!
Verse 16
ﯪﯫﯬ
ﯭ
Kwani hatukuwaangamiza walio tangulia?
Verse 17
ﯮﯯﯰ
ﯱ
Kisha tukawafuatilizia walio fuatia?
Verse 18
ﯲﯳﯴ
ﯵ
Ndio kama hivi tuwatendavyo wakosefu!
Verse 19
ﯶﯷﯸ
ﯹ
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
Verse 20
ﭑﭒﭓﭔﭕ
ﭖ
Kwani hatukukuumbeni kwa maji ya kudharauliwa?
Verse 21
ﭗﭘﭙﭚ
ﭛ
Kisha tukayaweka mahali pa utulivu madhubuti?
Verse 22
ﭜﭝﭞ
ﭟ
Mpaka muda maalumu?
Verse 23
ﭠﭡﭢ
ﭣ
Tukakadiria na Sisi ni wabora wa kukadiria.
Verse 24
ﭤﭥﭦ
ﭧ
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
Verse 25
ﭨﭩﭪﭫ
ﭬ
Kwani hatukuifanya ardhi yenye kukusanya
Verse 26
ﭭﭮ
ﭯ
Walio hai na maiti?
Verse 27
Na ndani yake tukaweka milima mirefu yenye kuthibiti, na tunakunywesheni maji matamu?
Verse 28
ﭸﭹﭺ
ﭻ
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
Verse 29
ﭼﭽﭾﭿﮀﮁ
ﮂ
Nendeni kwenye adhabu mliyo kuwa mkiikanusha!
Verse 30
ﮃﮄﮅﮆﮇﮈ
ﮉ
Nendeni kwenye kivuli chenye mapande matatu!
Verse 31
ﮊﮋﮌﮍﮎﮏ
ﮐ
Hakikingi moto, wala hakiwaepushi na mwako.
Verse 32
ﮑﮒﮓﮔ
ﮕ
Hakika Moto huo unatoa macheche kama majumba!
Verse 33
ﮖﮗﮘ
ﮙ
Kama kwamba ni ngamia wa rangi ya manjano!
Verse 34
ﮚﮛﮜ
ﮝ
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
Verse 35
ﮞﮟﮠﮡ
ﮢ
Hii ni siku ambayo hawatatamka kitu,
Verse 36
ﮣﮤﮥﮦ
ﮧ
Wala hawataruhusiwa kutoa udhuru.
Verse 37
ﮨﮩﮪ
ﮫ
Ole wao siku hiyo hao walio kanusha!
Verse 38
ﮬﮭﮮﮯﮰﮱ
ﯓ
Hii ndiyo siku ya kupambanua. Tumekukusanyeni nyinyi na walio tangulia.
Verse 39
ﯔﯕﯖﯗﯘ
ﯙ
Ikiwa mnayo hila, nifanyieni hila Mimi!
Verse 40
ﯚﯛﯜ
ﯝ
Ole wao siku hiyo hao walio kanusha!
Verse 41
ﯞﯟﯠﯡﯢ
ﯣ
Hakika wachamngu watakuwa katika vivuli na chemchem,
Verse 42
ﯤﯥﯦ
ﯧ
Na matunda wanayo yapenda,
Verse 43
ﯨﯩﯪﯫﯬﯭ
ﯮ
Kuleni na kunyweni kwa furaha kwa yale mliyo kuwa mkiyatenda.
Verse 44
ﯯﯰﯱﯲ
ﯳ
Hakika ndio kama hivyo tunavyo walipa watendao mema.
Verse 45
ﯴﯵﯶ
ﯷ
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
Verse 46
ﯸﯹﯺﯻﯼ
ﯽ
Kuleni na mjifurahishe kidogo tu. Hakika nyinyi ni wakosefu!
Verse 47
ﯾﯿﰀ
ﰁ
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
Verse 48
ﰂﰃﰄﰅﰆﰇ
ﰈ
Na wakiambiwa: Inameni! Hawainami.
Verse 49
ﰉﰊﰋ
ﰌ
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
Verse 50
ﰍﰎﰏﰐ
ﰑ
Basi maneno gani baada ya haya watayaamini?
تقدم القراءة