Tafsiri ya Sura Al-Ghashiyah kwa السواحلية kutoka Ali Muhsin Al - Swahili translation
Verse 1
ﭽﭾﭿﮀ
ﮁ
Al-Ghashiyah
Je! Imekufikia khabari ya msiba wa kufudikiza?
Verse 2
ﮂﮃﮄ
ﮅ
Siku hiyo nyuso zitainama,
Verse 3
ﮆﮇ
ﮈ
Zikifanya kazi, nazo taabani.
Verse 4
ﮉﮊﮋ
ﮌ
Ziingie katika Moto unao waka -
Verse 5
ﮍﮎﮏﮐ
ﮑ
Zikinyweshwa kutoka chemchem inayo chemka.
Verse 6
ﮒﮓﮔﮕﮖﮗ
ﮘ
Hawatakuwa na chakula isipo kuwa kichungu chenye miba.
Verse 7
ﮙﮚﮛﮜﮝﮞ
ﮟ
Hakinenepeshi wala hakiondoi njaa.
Verse 8
ﮠﮡﮢ
ﮣ
Siku hiyo nyuso nyengine zitakuwa kunjufu.
Verse 9
ﮤﮥ
ﮦ
Zitakuwa radhi kwa juhudi yao,
Verse 10
ﮧﮨﮩ
ﮪ
Katika Bustani ya juu.
Verse 11
ﮫﮬﮭﮮ
ﮯ
Hawatasikia humo upuuzi.
Verse 12
ﮰﮱﯓ
ﯔ
Humo imo chemchem inayo miminika.
Verse 13
ﯕﯖﯗ
ﯘ
Humo vimo viti vilivyo nyanyuliwa,
Verse 14
ﯙﯚ
ﯛ
Na bilauri zilizo pangwa,
Verse 15
ﯜﯝ
ﯞ
Na matakia safu safu,
Verse 16
ﯟﯠ
ﯡ
Na mazulia yaliyo tandikwa.
Verse 17
ﯢﯣﯤﯥﯦﯧ
ﯨ
Je! Hawamtazami ngamia jinsi alivyo umbwa?
Verse 18
ﯩﯪﯫﯬ
ﯭ
Na mbingu jinsi ilivyo inuliwa?
Verse 19
ﯮﯯﯰﯱ
ﯲ
Na milima jinsi ilivyo thibitishwa?
Verse 20
ﯳﯴﯵﯶ
ﯷ
Na ardhi jinsi ilivyo tandazwa?
Verse 21
ﯸﯹﯺﯻ
ﯼ
Basi kumbusha! Hakika wewe ni Mkumbushaji.
Verse 22
ﯽﯾﯿ
ﰀ
Wewe si mwenye kuwatawalia.
Verse 23
ﭑﭒﭓﭔ
ﭕ
Lakini anaye rudi nyuma na kukataa,
Verse 24
ﭖﭗﭘﭙ
ﭚ
Basi Mwenyezi Mungu atamuadhibu kwa adhabu iliyo kubwa kabisa!
Verse 25
ﭛﭜﭝ
ﭞ
Hakika ni kwetu Sisi ndio marejeo yao.
Verse 26
ﭟﭠﭡﭢ
ﭣ
Kisha hakika ni juu yetu Sisi hisabu yao!
تقدم القراءة